Prof Decentman
JF-Expert Member
- Jul 14, 2013
- 276
- 140
Nianze na kukupa pole katika kashkashi unazokumbana nazo katika kutimiza ndoto yako ya kuwa kiongozi katika taasisi za michezo katika nchi ya Tanzania.
Kwanza mimi binafsi si mwana michezo na sina interest zozote na michezo, sina timu ninayoshabikia japo ninatamani nchi yangu na timu zetu zifike mbali katika michezo. Yaani hata sasa kombe la dunia linapoendelea ninalala zako usingizi mzuri habari sina zaidi ya kusikia matokeo baada ya mechi kwisha.
Lakini nina kipande kidogo cha ushauri ambacho waweza kukitumia na ninajua yawezekana umeshaambiwa na mimi naongezea tu kidogo japo nilitamani kutoa ushauri huu mapema lakini nikasema ngoja nisubiri part three ya hii muvi sijui ndo ya mwisho au tusubiri kuna part 4 na 5, sijui.
Unajua najaribu kuwaza au kuingia katika viatu vyako. Nakuona ukiwa na ndoto, pengine uliianza hapo kabla (maana najua ulishawahi kuwa kiongozi wa soka) na unatamani kuimalizia au kuboresha zaidi.
Pengine una kitu ambacho umekiona na ukatamani sana sana kukitimiza kupitia nafasi yako kama kiongozi. Na kama mtu yeyote anayetaka jambo lake lifanikiwe haliishii katika ndoto hivyo umejaribu kuliweka katika vitendo.
Lakini bahati mbaya umekutana na 'rejection' ama kukataliwa. Najaribu kuwaza jinsi unavyojisikia kwa hao wanao kukataa ama kukuwekea mizengwe. Nina uhakika kwa hulka za kibinadam hakuna mtu ambaye atajisikia vizuri anapo kataliwa ama kupata changamoto za kufanya kile anachotamani.
1. Nina amini kuwa unayo dhamira ya dhati toka moyoni mwako kufanya mabadiliko ama kutimiza ndoto zako hizo. Ila kabla hujafanya jambo lolote unapaswa kufanya 'SWOC' ninajua wewe kama msomi unalijua hili.
Angalia (Kile unachoweza) strength zako, weakness zako (Udhaifu), Fursa zilizopo ( Opportunity) na Changamoto zilizopo (Challenge) ili ufanye maamuzi sahihi kabisa.
a. Strength zako: Nina imani hichi unachokiamini unaweza ndicho kinacho kusukuma kupambana miaka yote hii kutafuta uongozi katika vyama vya soka, yawezekana ni uzoefu wako a uongozi wa soka, yawezekana una network na wadau wa soka nje, yawezekana ni kutokupenda rushwa na kutenda haki katika mambo ya soka etc.
Cha kufanya: Endelea kujiimarisha katika mambo hayo na tafuta vitu bora zaidi ili uwe bora zaidi.
b.Wewe kama binadamu yawezekana una madhaifu yako ambayo hayo wenzanko au wanao kufahamu wamewekeza katika hayo kuhakikisha unashindwa kutimiza ndoto zako.
Cha kufanya: Anza sasa kujitathmini uone ni wapi kuna shida hivyo jipange upya kwa namna nyingine yoyote kutimiza ndoto yako.
c.Fursa: Nikitazama katika mambo ya michezo japo mimi sio mtaalam naona zipo fursa nyingi sana. Naona yapo maeneo makubwa nchi hii na ukanda huu wa pwani vinaweza kujengwa viwanja vikubwa vya michezo, naona vijana wengi wenye vipaji ambao wanaweza kutengeneza timu nzuri kwa mtu yeyote kumiliki tena bila gharama kubwa, naona maduka ya vifaa vya michezo na fursa nyingine nyingi katika sanaa, naona fursa ya kutengeneza shule za michezo ukauza wachezaji etc.
Cha kufanya: Achana na changamoto za simba na yannga zisikupotezee muda, ni wakati muafaka sasa uanzishe timu yako. Haitakuchukua miaka 10 - 20 utafurahia matunda ya timu yako na wewe mwenyewe ukiwa ni kiongozi mwenye kutimiza ndoto uliyo nayo kupitia watu wengine, angalia mfano wa Azam. Wapo vijana wengi sana wenye mapenzi na michezo watakachohitaji toka kwako ni uhakika wa chakula tu na mahitaji madogo madogo, nina uhakika timu yako itakuwa miongoni mwa timu nzuri Tanzania mnamo 2020.
Yawezekana unalo duka la vifaa vya michezo au gym ni muda muafaka wa kuendelea kuwekeza katika hayo.
Anzisha shule ya michezo, najua kwa network uliyo nayo na resource zako utafanikiwa sana katika hili.
Tafuta maeneo yapo mengi nunua na utafute mwekezaji mjenge kiwanja kizuri, simba na yanga hakika wana weza kuwa wateja wako, hope utawahudumia bila kinyongo.
d. Changamoto (Challenge) Angalia ni changamoto zipi zinaweza kufanya usifanikiwe. Ukiendelea kuwepo huko nadhani nafasi ya kufanikiwa ni ndogo kwa kuwa soka letu limetawaliwa na fitina, uzandiki na namna zote mbaya.
Zipo changamoto nyingi za ndani na nje unaweza kupitia ikiwemo kukosa fedha, kupata wa kukusapoti wenye ndoto kama zako, vifaa vya michezo, taratibu za kisheria, kutumia muda wako mwingi kufatilia mambo haya.
Cha kufanya: Tengeneza mkakati mzuri kukabiliana na changamoto zote hizi, tafuta best people wanaoweza kuelewa una maana gani kurisk muda wako, fedha zako, mali zako na akili yako simply because unataka kutimiza ndoto zako.Jiunge na wafadhiri wapenda michezo wenye mitaji yao waambie kama ilivyo Afrika magharibi, Afrika mashariki wapo vijana wengi wazuri wacheza soka wana oweza kuuzika katika soko la kimataifa.
Ili mwanadamu yoyote afanikiwe anahitaji mambo matatu:
1. Apende sana na kuwa na nia ya kitu anachokifanya (interest kubwa sana)
2. Awe na ujuzi ( technical know how) ya hicho anacho kifanya
3. Awe angalau na uzoefu wa hicho anachokifanya.
Ukiwa na vitu hivi hata kama huna mtaji fedha ni lazima ufanikiwe.
Mwisho nikukumbushe wapo watu walishindwa mara nyingi kuliko hata wewe, wengine ni katika siasa lakini kwa sababu walikuwa focused na ndoto zao mwisho walifanikiwa. Usikubali watu wa kukatishe tamaa, as long as you want to achieve your dream.
Kwa leo niishie hapo.
Kwanza mimi binafsi si mwana michezo na sina interest zozote na michezo, sina timu ninayoshabikia japo ninatamani nchi yangu na timu zetu zifike mbali katika michezo. Yaani hata sasa kombe la dunia linapoendelea ninalala zako usingizi mzuri habari sina zaidi ya kusikia matokeo baada ya mechi kwisha.
Lakini nina kipande kidogo cha ushauri ambacho waweza kukitumia na ninajua yawezekana umeshaambiwa na mimi naongezea tu kidogo japo nilitamani kutoa ushauri huu mapema lakini nikasema ngoja nisubiri part three ya hii muvi sijui ndo ya mwisho au tusubiri kuna part 4 na 5, sijui.
Unajua najaribu kuwaza au kuingia katika viatu vyako. Nakuona ukiwa na ndoto, pengine uliianza hapo kabla (maana najua ulishawahi kuwa kiongozi wa soka) na unatamani kuimalizia au kuboresha zaidi.
Pengine una kitu ambacho umekiona na ukatamani sana sana kukitimiza kupitia nafasi yako kama kiongozi. Na kama mtu yeyote anayetaka jambo lake lifanikiwe haliishii katika ndoto hivyo umejaribu kuliweka katika vitendo.
Lakini bahati mbaya umekutana na 'rejection' ama kukataliwa. Najaribu kuwaza jinsi unavyojisikia kwa hao wanao kukataa ama kukuwekea mizengwe. Nina uhakika kwa hulka za kibinadam hakuna mtu ambaye atajisikia vizuri anapo kataliwa ama kupata changamoto za kufanya kile anachotamani.
1. Nina amini kuwa unayo dhamira ya dhati toka moyoni mwako kufanya mabadiliko ama kutimiza ndoto zako hizo. Ila kabla hujafanya jambo lolote unapaswa kufanya 'SWOC' ninajua wewe kama msomi unalijua hili.
Angalia (Kile unachoweza) strength zako, weakness zako (Udhaifu), Fursa zilizopo ( Opportunity) na Changamoto zilizopo (Challenge) ili ufanye maamuzi sahihi kabisa.
a. Strength zako: Nina imani hichi unachokiamini unaweza ndicho kinacho kusukuma kupambana miaka yote hii kutafuta uongozi katika vyama vya soka, yawezekana ni uzoefu wako a uongozi wa soka, yawezekana una network na wadau wa soka nje, yawezekana ni kutokupenda rushwa na kutenda haki katika mambo ya soka etc.
Cha kufanya: Endelea kujiimarisha katika mambo hayo na tafuta vitu bora zaidi ili uwe bora zaidi.
b.Wewe kama binadamu yawezekana una madhaifu yako ambayo hayo wenzanko au wanao kufahamu wamewekeza katika hayo kuhakikisha unashindwa kutimiza ndoto zako.
Cha kufanya: Anza sasa kujitathmini uone ni wapi kuna shida hivyo jipange upya kwa namna nyingine yoyote kutimiza ndoto yako.
c.Fursa: Nikitazama katika mambo ya michezo japo mimi sio mtaalam naona zipo fursa nyingi sana. Naona yapo maeneo makubwa nchi hii na ukanda huu wa pwani vinaweza kujengwa viwanja vikubwa vya michezo, naona vijana wengi wenye vipaji ambao wanaweza kutengeneza timu nzuri kwa mtu yeyote kumiliki tena bila gharama kubwa, naona maduka ya vifaa vya michezo na fursa nyingine nyingi katika sanaa, naona fursa ya kutengeneza shule za michezo ukauza wachezaji etc.
Cha kufanya: Achana na changamoto za simba na yannga zisikupotezee muda, ni wakati muafaka sasa uanzishe timu yako. Haitakuchukua miaka 10 - 20 utafurahia matunda ya timu yako na wewe mwenyewe ukiwa ni kiongozi mwenye kutimiza ndoto uliyo nayo kupitia watu wengine, angalia mfano wa Azam. Wapo vijana wengi sana wenye mapenzi na michezo watakachohitaji toka kwako ni uhakika wa chakula tu na mahitaji madogo madogo, nina uhakika timu yako itakuwa miongoni mwa timu nzuri Tanzania mnamo 2020.
Yawezekana unalo duka la vifaa vya michezo au gym ni muda muafaka wa kuendelea kuwekeza katika hayo.
Anzisha shule ya michezo, najua kwa network uliyo nayo na resource zako utafanikiwa sana katika hili.
Tafuta maeneo yapo mengi nunua na utafute mwekezaji mjenge kiwanja kizuri, simba na yanga hakika wana weza kuwa wateja wako, hope utawahudumia bila kinyongo.
d. Changamoto (Challenge) Angalia ni changamoto zipi zinaweza kufanya usifanikiwe. Ukiendelea kuwepo huko nadhani nafasi ya kufanikiwa ni ndogo kwa kuwa soka letu limetawaliwa na fitina, uzandiki na namna zote mbaya.
Zipo changamoto nyingi za ndani na nje unaweza kupitia ikiwemo kukosa fedha, kupata wa kukusapoti wenye ndoto kama zako, vifaa vya michezo, taratibu za kisheria, kutumia muda wako mwingi kufatilia mambo haya.
Cha kufanya: Tengeneza mkakati mzuri kukabiliana na changamoto zote hizi, tafuta best people wanaoweza kuelewa una maana gani kurisk muda wako, fedha zako, mali zako na akili yako simply because unataka kutimiza ndoto zako.Jiunge na wafadhiri wapenda michezo wenye mitaji yao waambie kama ilivyo Afrika magharibi, Afrika mashariki wapo vijana wengi wazuri wacheza soka wana oweza kuuzika katika soko la kimataifa.
Ili mwanadamu yoyote afanikiwe anahitaji mambo matatu:
1. Apende sana na kuwa na nia ya kitu anachokifanya (interest kubwa sana)
2. Awe na ujuzi ( technical know how) ya hicho anacho kifanya
3. Awe angalau na uzoefu wa hicho anachokifanya.
Ukiwa na vitu hivi hata kama huna mtaji fedha ni lazima ufanikiwe.
Mwisho nikukumbushe wapo watu walishindwa mara nyingi kuliko hata wewe, wengine ni katika siasa lakini kwa sababu walikuwa focused na ndoto zao mwisho walifanikiwa. Usikubali watu wa kukatishe tamaa, as long as you want to achieve your dream.
Kwa leo niishie hapo.