Bandiko hili na liwe wosia kwa muhusika na wengine wengi wenye mitazamo na akili za aina yake.
Tukidhamiria kulipa tafsiri pana suala husika,hatutaacha kuelekeza lawama zetu kwa wale wote wanaochukuliwa kama watawala ndani ya taasisi ya kisiasa,CCM.
Kwa vigezo vyote,hii si CCM iliyokuwa ikihimiza dhana za,heshima na usawa wa kibinadamu,chini ya imani kuwa ''Binadamu wote ni ndugu zangu'' wala si ile iliyopata kuamini ''fitina kwangu mwiko''.
Ya sasa ni CCM isiyoona umuhimu wa kuheshimiana wala kuishi kindugu na kwa hakika haioni uwezekano wa kufanya siasa pasipo kuwekeza katika fitina,uzushi, uongo na upuuzi.
Nikiisha kuekeza lawama zangu dhidi CCM kama taasisi ya kisiasa,muhusika anawajibika,kulingana na maneno na matendo yake,kubeba lawama.Ajiulize:kwa nini,iwe ni yeye na mwenzake mmoja-ambaye naye inaonyesha amebobea katika upuuzi usiomithilika-wamekasimiwa jukumu la kutamtaka maneno yasiyo na staha dhidi ya watu wanoheshimika katika jamii badala ya kueneza sera,itikadi falsafa za chama chao?Ni imani yangu kwamba wahusika wamekabidhiwa kazi hiyo baada ya kukidhi kipimo cha siasa za sasa CCM,zinazojiegemeza katika umahiri katika kubuni na kusambaza matusi badala ya hoja.
Kimantiki,kwa hulka,mtu mpuuzi hutenda upuuzi.Hatari moja ni kuwa ni kazi inayochosha mno kumsihi mpuuzi aachane na upuuzi.Bila kutenda upuuzi muhusika mara moja anapoteza sifa ya kuitwa mpuuzi.Kwa mienendo ya baadhi yetu,upuuzi ni sifa adhimu inayokumbatiwa ,kung'ang'aniwa na kutamaniwa.Kinachoogopesha zaidi ni kuwa,kwa sasa ,upuuzi ni ajira inayolipa na walipaji hawako tayari kukatisha ajira za wapuuzi maana,kwanza jamii ya wapuuzi haiishi na pili uwekezaji katika upuuzi unawahakikishia matokeo fulani hata kama ni ya kipuuzi.