Ushauri wa bure Kwa kafulila!!

Ushauri wa bure Kwa kafulila!!

David Kafulila a.k.a "Tumbiri" amejipa jukumu la kuwa msemaji wa watawala kuonesha kuwa uchumi wa Tanzania upo Imara na himilivu kuliko hata wale wenye jukumu Hilo.

Kafulila anaongea sana kuhusu Hali ya uchumi wa Tanzania kuliko hata Waziri wa fedha au Gavana wa Benki Kuu ambao ndiyo wenye wajibu huo.

Ushauri wangu kwake ni kwamba siyo kweli kuwa watanzania wanalalamika uchumi wao mbaya kwa sababu hawajui nadharia za uchumi.

Mtanzania anayeshindwa kulipa ada ya shule kwa mtoto wake, anaposhindwa kulipa bili za matibabu yake, anapokosa uwezo wa kununua chakula na kadhalika, huo kwake ni uhalisia wala siyo hisia anazojenga kwa kuwa hajui nadharia za kiuchumi.


Kafulila ajue tu kuwa nadharia zote za kiuchumi ni tafsiri tu ya binadamu kuhusu maisha na zenyewe siyo zinazojenga maisha.

Nadharia za kiuchumi zimewekwa angalau kujaribu kupunguza minyukano ya binadamu kwenye kujipatia mahitaji yao dhidi ya rasirimali zilizopo.

Kwa ivo watanzania wanaposema uchumi wao ni mbaya hawazushi bali ndiyo uhalisia wa maisha yao.

Labda yeye hana utofauti na yule malkia aliyesema "kama hawana mikate si wale keki?".
Ni moja kati ya watu wa hovyo waliopo
 
Anapambana sana kutunza nafasi yake kwa kumplease mama, kumbuka alipewa uRC baada ya kuachwa na mke, alipopoteza uRC probably alijiwekea nadhiri akikumbukwa tena atamwaga mashairi deile ili aendelee kuwa relevant, so tangu kapewa ile PPP ni kuchonga kwenda mbele na hapa JF analipa chawa wa kutosha ujue! Wanasema kbs ni mlipaji mzuri sana, hakopi
Yani alipe watu wanaotumia huu mtandao ili iweje?

Mtandao mtaani kwangu kote huenda naujua mimi tu ndo alipe ma anonymous ili wa waambie nini ma anonymous
🙌🏾🙌🏾🙌🏾
 
David Kafulila a.k.a "Tumbiri" amejipa jukumu la kuwa msemaji wa watawala kuonesha kuwa uchumi wa Tanzania upo Imara na himilivu kuliko hata wale wenye jukumu Hilo.

Kafulila anaongea sana kuhusu Hali ya uchumi wa Tanzania kuliko hata Waziri wa fedha au Gavana wa Benki Kuu ambao ndiyo wenye wajibu huo.

Ushauri wangu kwake ni kwamba siyo kweli kuwa watanzania wanalalamika uchumi wao mbaya kwa sababu hawajui nadharia za uchumi.

Mtanzania anayeshindwa kulipa ada ya shule kwa mtoto wake, anaposhindwa kulipa bili za matibabu yake, anapokosa uwezo wa kununua chakula na kadhalika, huo kwake ni uhalisia wala siyo hisia anazojenga kwa kuwa hajui nadharia za kiuchumi.


Kafulila ajue tu kuwa nadharia zote za kiuchumi ni tafsiri tu ya binadamu kuhusu maisha na zenyewe siyo zinazojenga maisha.

Nadharia za kiuchumi zimewekwa angalau kujaribu kupunguza minyukano ya binadamu kwenye kujipatia mahitaji yao dhidi ya rasirimali zilizopo.

Kwa ivo watanzania wanaposema uchumi wao ni mbaya hawazushi bali ndiyo uhalisia wa maisha yao.

Labda yeye hana utofauti na yule malkia aliyesema "kama hawana mikate si wale keki?".
Hoja zake ni zipi na zako wewe za kumpundua ni zipi?!!!!
Kuna kipindi chochote au nchi yoyote unayoijua ambayo wananchi wake wote Wana uwezo wa kulipa ada na kujihudumia matibabu mazuri?!!!!! Chadema bhana, mtu akishawahama tu basi hawaishi kumsakama.
 
Kuna kipindi chochote au nchi yoyote unayoijua ambayo wananchi wake wote Wana uwezo wa kulipa ada na kujihudumia matibabu mazuri?!!!
Kuna mahali nimeandika wananchi wote? Sina huo uwendawazimu wa kudhani watanzania wote wana huo uwezo lakini angalau 90% ya watanzania wanatakiwa wawe na hakika ya maisha bora.
 
Unaruhusiwa na wala huvunji sheria kuamini unachoamini na hulazimishwi kuchukua kila unachosoma humu! Ndio uhuru wenyewe
Chief hata kama nina ufahamu mdogo ila hili haliniingii akilini yani watu wa humu walipwe kueneza propaganda kwa ajili ya audience kama mimi au? 😂😂

Over my dead body Kafulila atunze tu hizo pesa tukalewee, humu kama anailipa taasisi yenyewe ni sawa maana Ina wafuasi wengi nje hata ya hapa.

Anyway ni maoni ya msukuma tu kutoka Ikulwa,Geita
 
Matendo yake ni kama vile mtu umechomwa na mwiba halafu mtu mwingine ndiye ajipe haki ya kutafsiri kiwango cha maumivu unayopitia.

Watu kila siku umaskini wao unawaongezekea yeye yupo bize kusema maisha ni mazuri kuliko miaka iliyopita.
Unamkumbuka Kafulila wa miaka 10 iliyopita???
Yule ndo alikuwa mtu timamu wa kumsikiliza.
Huyu wa saizi ukimsikiliza ni "at your own expense "
 
David Kafulila a.k.a "Tumbiri" amejipa jukumu la kuwa msemaji wa watawala kuonesha kuwa uchumi wa Tanzania upo Imara na himilivu kuliko hata wale wenye jukumu Hilo.

Kafulila anaongea sana kuhusu Hali ya uchumi wa Tanzania kuliko hata Waziri wa fedha au Gavana wa Benki Kuu ambao ndiyo wenye wajibu huo.

Ushauri wangu kwake ni kwamba siyo kweli kuwa watanzania wanalalamika uchumi wao mbaya kwa sababu hawajui nadharia za uchumi.

Mtanzania anayeshindwa kulipa ada ya shule kwa mtoto wake, anaposhindwa kulipa bili za matibabu yake, anapokosa uwezo wa kununua chakula na kadhalika, huo kwake ni uhalisia wala siyo hisia anazojenga kwa kuwa hajui nadharia za kiuchumi.


Kafulila ajue tu kuwa nadharia zote za kiuchumi ni tafsiri tu ya binadamu kuhusu maisha na zenyewe siyo zinazojenga maisha.

Nadharia za kiuchumi zimewekwa angalau kujaribu kupunguza minyukano ya binadamu kwenye kujipatia mahitaji yao dhidi ya rasirimali zilizopo.

Kwa ivo watanzania wanaposema uchumi wao ni mbaya hawazushi bali ndiyo uhalisia wa maisha yao.

Labda yeye hana utofauti na yule malkia aliyesema "kama hawana mikate si wale keki?".
Bora angekuwa anajibu wananchi sababu ya kushindwa kuwa na viwanda nchini vya chuma wakati madini hayo tunanayo na nishati ya makaa ya Mawe pia tunayo.yeye amekazana kusema uchumi himilivu kwenye karatasi
 
Bora angekuwa anajibu wananchi sababu ya kushindwa kuwa na viwanda nchini vya chuma wakati madini hayo tunanayo na nishati ya makaa ya Mawe pia tunayo.yeye amekazana kusema uchumi himilivu kwenye karatasi
Uchumi himilivu Kwa daraja/kiwango kipi?

Maana labda ni himilivu kwenye kukopesheka kwenye taasisi za kimataifa. Lakini huku mtaani uchumi wetu una uwezo wa kuhimili kuendesha maisha yetu ya Kila siku?
 
Back
Top Bottom