Ushauri wa Bure kwa Director Modestus Francis Kipilimba

Ushauri wa Bure kwa Director Modestus Francis Kipilimba

Freddie Matuja

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2018
Posts
1,484
Reaction score
2,890
Kwanza kabisa nakupongeza kwa majukumu mazito ya kuwa sehemu ya Uongozi wa taasisi ambayo kwa sasa wewe ndiyo mtendaji mkuu.

Nataka kuamini unashaurika kupitia wanaokufahamu, pia hata na watu usiowafahamu maadamu msingi wa ushauri wao umelenga kwenye uzalendo na ujenzi wa taifa letu Tanzania.

Bila shaka kunaweza kuwa na namna nyingi za kukufkishia ujumbe, na bila shaka kuna nyakati ujumbe unaweza usikufikie. Na kuna uwezekano ujumbe ukikufikia, huenda ukawa umechujwa na “context” ya mtuma ujumbe isifikishwe sawia ili kutimiza malengo ya mtuma ujumbe.

Msingi wa kuandika hapa kwako na wasaidizi wako, ni kwa lengo la kuwafanya mtambue na kuwa kila Mtanzania ana uwezo wa kuwa sehemu ya mafanikio ya kuifikia nchi ya “maziwa na asali”. Bill Hybels mmoja wa walimu nguli wa Uongozi anasema, “Everyone has influence. You have influence” Pia Dr. Myles Monroe mara kadhaa amewahi kusema, makaburini ndiko kuna utajiri ambao haukuwahi kutumika. Mimi nataka kuamini, wewe kwa nafasi yako unaweza ku-harness utajiri katika akili za Watanzania ambao bila shaka haujatumika au uko-underutilized.

Nimesikia kutoka vyanzo vinavyoaminika ya kuwa wewe pia ni Mchungaji, na bila shaka biblia ni moja ya kitabu ambayo unakisoma. Kwa muktadha huo, naomba kukufikirisha hadithi kadhaa kutoka katika biblia.

Naomba nikukumbushe hadithi tatu kutoka katika biblia na baada ya hapo ntakurejesha kwenye hoja.

Yusufu mwana wa Yakobo alikuwa mfungwa gerezani. Japo alifungwa kwa kusingiziwa, tunakumbuka, ni “mfungwa huyu” alikuja na suluhisho la kiuchumi kwa Misri ambalo lilikuwa Taifa kubwa kiuchumi na kijeshi nyakati hizo.

Njaa ilikuwa ni kitu halisi kule Misri, na tafsiri ya ndoto hali kadhalika ilikuwa tafsiri halisi. Kuwa kufanya detailed analysis; miaka 7 ilikuwa muhimu kweli kukusanya chakula cha ziada, kujenga maghala ya kuhifadhi chakula, kuweka mifumo ya kudhibiti wadudu wasiharibu chakula. Kuwa na magari yak u-support logistics, kuweka ulinzi ili chakula kisiibwe. Kuwa na mifumo ya kudhibiti moto usitokee ili hifadhi ya chakula isipotee. Bila shaka kukusanya zaida kwa ajili ya ongezeko la watoto Misri na mataifa jirani na Misri ambayo kama yakipata njaa yanaweza kwenda kununua chakula.

Hadithi ya pili ni ya Daudi mwana wa Yese ambae alikuwa mchunga mifugo. Wakati nabii Samuel anafanya mchakato wa kutafuta kiongozi kuchukua nafasi ya Mfalme Sauli, baba yake mzazi hakuona “potential” kama mwanae Daud kama anafaa kuwa kiongozi. Baba alidhania kaka zake ndiyo kumbe hawakuwa watu sahihi kwa kazi ya kuongoza taifa.

Miaka kadhaa baada ya kupakwa mafuta, Daudi amekwenda kwenye “battle ground” kupeleka chakula kwa maelekezo ya baba yake. Alipofika bonde la Soko, kaka yake na Daudi aitwae Eliab alimwona Daudi kwa jicho la mtu mvivu alietoroka mifugo ya mzee Yese kwa lengo la kujionea/kushuhudia “sinema ya bure” ya mpambano kati ya Israeli na Wafilisti.


Wengi tunakumbuka Daudi alimuua Goliath kwa kombeo baada ya watu wengine kupeleka ujumbe kwa Mfalme Sauli kuwa kuna kijana mwenye ujasiri na ari ya kumpiga na kumuua Goliath kama atapata ridhaa ya Amri Jeshi Mkuu. Inafahamika Daudi hakuwa military trained na hakuwa enlisted jeshini kama Eliab (kaka wa Daudi)


Hao waliokuwa na uzoefu wa kijeshi na vita kwa muda mrefu ikiwemo Sauli ambae alikuwa Amri jeshi mkuu, wote walikuwa waoga maana hawakuwa na option (weather ni strategy, methodology au tactic) yoyote ya kumkabili Goliath ambae alikuwa tishio la Usalama wa Taifa la Israel, tishio kwa Ufalme wote na bila shaka tishio kwa kizazi cha Israel baada ya vita. Tishio kubwa halikuwa uwezekano wa kuuwawa kwa atakaejitokeza kumkabili Goliath, bila shaka tishio lilikuwa utumwa ambao Taifa la Israel lingeupata baada ya yeyote ambae angemkabili Goliath kuuwawa na Jenerali huyu nguli na mzoefu wa vita.

Hadithi ya mwisho inamuhusu Jenerali wa Jeshi la Syria kwa jina la Naaman. Naaman alipata habari (taarifa) kutoka kwa mkewe kuwa katika nchi ya Israel, kuna nabii yuko Samaria anaweza kumponya ukoma. Actually, aliemjuza mke wa Naaman, ni “house girl” aliekuwa katika nyumba ya Naaman.

Jenerali Naaman, aliamini na kuchukua hatua ya kwenda kwa nabii Elisha. Alipopata taarifa kupitia msaidizi wa Elisha ya kuwa anatakiwa kujichovya/kujitumbukiza mara saba katika mto Jordan, Naaman alivunjika moyo na hakutaka kufanya hivyo. Ndipo wasaidizi wake wakamsihi kwa nia njema bosi wao, kuwa, what’s a big deal. Kama angeambiwa jambo kubwa si angefanya. Jenerali Naaman baada ya kukubaliana na ushauri wa “aides” wake, alijichovya mara saba na ukoma ukatakasika.

Ushawishi wa kwanza ulitoka kwa “house girl” kwenda kwa mke wa Jenerali Naaman. Ushawishi wa pili ulitoka kwa “Mrs Naaman” kwenda kwa Jenerali Naaman. Hata Jenerali Naaman alipopata maelekezo ambayo hakuyapenda; aides wake waliokoa jahazi kwa kumshawishi bosi wao. Jenerali Naaman, alipo-buy in, alitakasika.

Naomba kumshauri Director Kipilimba kama layman katika mambo machache ya kukuza uchumi wa Tanzania kimkakati, hususan katika miaka hii ya Mhe. JPM ambae amejipambaua kuwafanya Watanzania kuwa “middle class” wa kati kwa kutumia viwanda kama nguzo ya kusisimua/kukuza uchumi.

Ikumbukwe, Daudi wala hakuwa enlisted jeshini, yet mkakati wake wa kumuua Goliath alileta matokeo.

Yusuf pamoja na kukaa kwa Captain Potifa kama mkuu wa wafanyakazi, hakuwahi kushika wadhifa na majukumu ya uongozi mkubwa katika Taifa la Misri. Yusuf alitoa tafsiri ya ndoto, ila mkakati wa hifadhi ya chakula kwa miaka 7 ulikuwa ni matokeao ya creativity, strategic planning na juhudi za Farao aliekuwa mtawala wa Misri kuona umuhumu wa kumjumuisha “mtu wa kuja” kwa kuwa alikuwa na akili ya kutatua matatizo ambayo insiders katika serikali ya Farao walishindwa kuja na majibu ya tafsiri ya ndoto na mkakati wa muda mrefu ya Taifa la Misr kuhifadhi chakula wakati wa neema ya chakula cha ziaada.

Hata yule house girl wa kwa Jenerali Naaman, japo alikuwa utumwani, yet alikuwa na ushawishi wa nia njema kwa bosi wake aweze kupona. Nami niko hapa kama mzalendo kwa nia njema kushauri.

Nadhani sote tutakubaliana pia, ajali ya MV. Nyerere, kisiwani Ukara majuma machache yaliyopita, wavuvi wa ukara (laymen), waliweza kuchukua jukumu la kwanza kuokoa waliokuwa hai na kuwaokoa miili ya watu waliopoteza maisha kabla ya vikosi ya uokoaji kutoka majeshi yetu havijafika visiwani Ukara. Hivyo, kwa lugha yangu ya “U-layman”, bila shaka kuna jambo Director Kipilimba na wasaidizi wako mtaokota.

Toka 1997 wakati dira ya Taifa inazinduliwa na toka JPM atangaze namna ya kukuza uchumi kupitia sekta ya viwanda, sisi kama Taifa je kuna mkakati wa pamoja wa kiuchumi (strategic economic inclusion)?

Je tuna model ya kiuchumi/model za kiuchumi ili kutimiza malengo ya kupata output kubwa katika kufikia uchumi wa kati kupitia viwanda?

Moja ya chanzo nilichosoma kutoka maandiko mbalimbali ya model ya kiintelijensia ya kukuza uchumi inasema… If intelligence is the capability of understanding and interacting with the environment in order to act to obtain competitive advantages.

Kuna maeneo kadhaa sisi Tanania tuna “competitive advantage”. Competitive advantage inaweza kuwa realized kwa haraka kama yafuatayo yatafanyiwa kazi

  • To define the strategy, including approach and the task of each countrymen through diverse organizations they are in;
  • To have the capability for abstract reasoning and understanding of the multiple interactions existing in complex environments, including a capability of judgment and knowledge development.
  • To have the capability to detect substitute products or disruptive technology and to understand cultural or demographic changes.
  • To develop the capability to be ahead of changes in regulatory or economic conditions of market dealers in order to launch offensive or defensive actions.
Intelligence must be firstly strategic and then economic. Then, it will be competitive or solely reduced to the analysis previous to knowledge acquisition through the appropriate techniques and technologies.

Ili kufikia malengo ya kukuza uchumi wa pamoja ambao nataka kuamini kuna outsiders ambao wanaweza kuwasaidia akina Dr. Mpango (Waziri wa Fedha) Waziri VIwanda Mwijage na Waziri wa Kilimo Tizeba, Waziri wa Mifugo Mpina na Waziri wa Ajira Mhagama na Director wa TIC Godfrey Mwambe.

Akina Mark Zuckeberg wa Facebook, Jeff Bezos wa Amazon, Jack Ma wa Alibaba ni “outsiders” katika elimu ya biashara na uchumi. Ila uwezo wa kuwa “creative and Innovative” walianza mdogo mdogo, eventually leo hii wamekuwa sehemu ya kukuza uchumi wa nchi zao.


Director Kipilimba, you can adopt a system of human intelligence that obtains information through persons through economic intelligence, business intelligence and competitive intelligence to ensure Tanzania is thriving economically by use of technology and know-how. Part can be locally harnessed and part can be outsourced.

In your course of governing the entity of which you’re entrusted with God and second, you’re entrusted with the President, you can quickly get results by accepting counsels and adopting the economic models to eliminate poverty and unemployment in this country.

If it happened the outsiders like David, Joseph, the house-girl the list goes on made a difference, you can experience the same by opening-avenue for such people. Some are not far away from the battle ground, you just need to head-pick them; some are “imprisoned through false accusation”

Policies and procedure are man made to ensure desired goals are realized. Decisions made on bad policies and standard operating procedures can delay on hinder true patriots who can make a remarkable economic change in motherland Tanzania.

As you stand in position to analyze a lot of human intel from various sectors/dept. under you. There is a potential of relying to a challenge which face Moses which he was receiving a feedback report from spies who visited the “Promise land”. Up-to this moment some people in junior, middle or senior positions who are serving the current regime are coward like the 10 spies. Either they have bad perception or non believers on how we can arrive into middle income earning country.

Sir, you have a real challenge to listen to a few who are bold like Joshua and Caleb. Very fortunate the boss you serve who is Commander in Chief is a true visionary, very bold, courageous leader who is decisive with audacity to see we Tanzania are navigating towards the promise land.


Mungu Ibariki Tanzania.
 
Ushauri mzuri. Ukweli ni kwamba kila mwanadamu hakuja duniani kwa bahati mbaya isipokuwa ni kwa mpango wa Mungu. Na hivyo kila mwanadamu ana mchango katika kuleta maendeleo duniani na hasa katika eneo anamoishi. Together We Can
 
" Very fortunate the boss you serve who is commander in chief is a TRUE VISIONARY , VERY BOLD COURAGEOUS LEADER WHO IS DECISIVE WITH AUDACITY to see we Tanzanian are navigating towards the promise land " , Kama hutajali unaweza kufafanua hapa ulimaanisha nini ? na kama haya uliyoyaandika hapa yanatoka moyoni kabisa na ni kweli unayamaanisha , kwa vigezo vipi ?

Tambua kwamba hapa JF kuhojiwa ni jambo la kawaida , kwahiyo usihofu .
 
Mleta mada umejaza porojo nyingi hueleweki.

Pili ukimwandikia mtu mkubwa andika kifupi na direct kwenye point.

Hili jarida uliloandika hakuna mtu mkubwa anaweza pata muda wa kusoma jarida refu kama hilo.

Ungeandika point zako walau kwa paragraff mbili tu au tatu. Umeandika kama mtu ambaye alikuwa yuko kwenye kuota anaandika kwa kutiririka anachoota zaidi.

Hebu andika kwa kifupi kwa paragrah tatu ambazo kila paragraph isizidi sentensi saba nini ulichokuwa ukimaanisha au kushauri
 
Duuu nimekuelewa kote ila hapo mwishoni kwamba ni visionary Leader nimepatwa na kigugumiz labda kama unamaanisha Blurred Visionary

Kuwa na Tamaa ya Tanzania kuwa middle class ni jambo moja lakini kuwa na mikakati ya kufikia tamaa hiyo ni jambo lingine kabisa .Tafakari katikati ya haya mawili utapata jibu lako ,na kaa nalo .

Anyway muda utaamua yote
 
Kwanza kabisa nakupongeza kwa majukumu mazito ya kuwa sehemu ya Uongozi wa taasisi ambayo kwa sasa wewe ndiyo mtendaji mkuu.

Nataka kuamini unashaurika kupitia wanaokufahamu, pia hata na watu usiowafahamu maadamu msingi wa ushauri wao umelenga kwenye uzalendo na ujenzi wa taifa letu Tanzania.

Mungu Ibariki Tanzania.
Mkuu Fredm asante kwa hii kitu, umemwaga nondo za kufa mtu, la nyuzi za hivi, huwa hazichangiwi sana, ila ukiweka thread ya Daimond Platnum, michango tele!.

Kiukweli Tanzania tuna matatizo from top to bottom, left, right and center!.
P.
 
I like ur topic ume elaborate vzuri nchi yetu inahtaji economic intelligence, business intelligence ili tupige hatua rather than investing in dirty politics, nchi zilizoendelea zilijikita zaidi kwenye economic intelligence, ndo mana zimepiga hatua sie tukiona wachina wamezagaa dunia wale wamejikita kwenye intelligencia ya kunusa fursa, without economic intelligence no development hasa kwenye era hii ya globalization, we are weak wenzetu wanatusoma udhaifu wetu na kutumia loophole kutupiga mfano issue za madini na makinikia.
 
Mleta mada umejaza porojo nyingi hueleweki.

Pili ukimwandikia mtu mkubwa andika kifupi na direct kwenye point.

Hili jarida uliloandika hakuna mtu mkubwa anaweza pata muda wa kusoma jarida refu kama hilo.

Ungeandika point zako walau kwa paragraff mbili tu au tatu. Umeandika kama mtu ambaye alikuwa yuko kwenye kuota anaandika kwa kutiririka anachoota zaidi.

Hebu andika kwa kifupi kwa paragrah tatu ambazo kila paragraph isizidi sentensi saba nini ulichokuwa ukimaanisha au kushauri
Acha uvivu wa kusoma yani uvivu wa Watanzania kusoma ndo maana maarifa yako kushoto loh.
 
Duuu nimekuelewa kote ila hapo mwishoni kwamba ni visionary Leader nimepatwa na kigugumiz labda kama unamaanisha Blurred Visionary

Kuwa na Tamaa ya Tanzania kuwa middle class ni jambo moja lakini kuwa na mikakati ya kufikia tamaa hiyo ni jambo lingene kabisa .Tafakari katikati ya haya mawili utapata jibu lako ,na kaa nalo .

Anyway muda utaamua yote
Kuwa na middle class ya makaratsi ni possible ila kwa nchi yetu sijaona hzo mbinu na mikakati ya kukwamua nchi yetu ifike middle economy.
 
Kuwa na middle class ya makaratsi ni possible ila kwa nchi yetu sijaona hzo mbinu na mikakati ya kukwamua nchi yetu ifike middle economy.
Hapa ndipo palipo na mtihani ,Ngoja tuendelee kununua Madiwani na Wabunge ama sijui tuwafundishe wanyama umuhimu wa Stiglers Gorge au marufuku kwa watumishi kuvaa suti mpaka siku Rais anakuja ndio mikakati tunayoiweza .
 
Umenikumbusha Secondary kwenye kuandika Ese unapamba zile point na maelezo mengi ya kujaza hata karatasi 8 halafu mwisho wa siku unapata 6 ya 20.

Sijaelewa ulichoandika.
 
Una point lakini mbwembwe zimezidi hadi unachosha kusoma. Wakati mwengine nenda kwenye point utaeleweka tuuu.
 
Hapa ndipo palipo na mtihanani ,Ngoja tuendelee kununua Madiwani na Wabunge ama sijui tuwafundishe wanyama umuhimu wa Stiglers Gorge au marufuku kwa watumishi kuvaa suti mpaka siku Rais anakuja ndio mikakati tunayoiweza .
Yani mi Raisi namkubali ila hii idea ya watu kujiuzulu na hakemei inamshushia credibility kabisa na itamfanya record yake huko mbeleni ije kuwa fedheha aisee, sioni huo umuhimu sijui rudia uchaguzi niunge mkono washauri hawampi ukweli hyo kitu imempunguzia heshima yake.
Hafu maendeleo mazuri ni ya watu pia maendeleo ya miundo mbinu. Faida ya miundo mbinu itaonekana like 10 years to come, pia asisahau uchumi sasa sio mzuri walah.

Hao wa marufuku kuvaa suti wamekosa kazi muhimu ya kufanya nchi inachagamoto nyingi kuliko wavaa suti. Huyo RC amejizalilisha au ndo alikua anatafta kiki.
 
Mkuu Fredm asante kwa hii kitu, umemwaga nondo za kufa mtu.
P.
Ujumbe wake ni mrefu sana lakini tunamshauri mkuu wa Usalama aimarishe taarifa toka kwa wasaidizi wake huko mikoani wilayani ambapo wengi sasa wanawalinda ma RC na DC na viongozi wengine huko, wamekuwa watetezi wa Maovu mfano huko Tarime mara siku Rais magufuli alipohutubia DC na OCD waliwapora Mabango wananchi kimya kimya hivyo kukosa fursa ya kuanika kero zao mbele ya Rais magufuli, pia OCD amenunuliwa na matajiri wa madini ambapo huenda kwenye migodi yao kuwapiga kuwapora madini na mali zao kisha kuwabambikia kesi ili waogope na pindi wakiwa jela matajiri wa madini hutumia mda huo kupora madini yao na mali zao, hapo ndipo wananchi wanaona idara ya usalama inawalea viongozi wanaowatesa wananchi na kuwabambikia kesi.
 
I like ur topic ume elaborate vzuri nchi yetu inahtaji economic intelligence, business intelligence ili tupige hatua rather than investing in dirty politics, nchi zilizoendelea zilijikita zaidi kwenye economic intelligence, ndo mana zimepiga hatua sie tukiona wachina wamezagaa dunia wale wamejikita kwenye intelligencia ya kunusa fursa, without economic intelligence no development hasa kwenye era hii ya globalization, we are weak wenzetu wanatusoma udhaifu wetu na kutumia loophole kutupiga mfano issue za madini na makinikia.
Well said, bro, umeandika kifupi lakini naamini umeeleweka mno...
 
Back
Top Bottom