Gorgeousmimi
JF-Expert Member
- Jun 21, 2010
- 9,296
- 7,688
Ni kweli kabisa uyasemyo BAK bila ushirikiano na msimamo kutoka kwa upande wa mume kuhusu hilo suala la elimu kutakuwa na utata!Ni kweli mimi49 inawezekana kabisa mke kusoma ndani ya ndoa lakini kikubwa ni kuwa na mume muelewa. Kama mume si mulewa au maamuzi yake yanayumbishwa na ndugu, jamaa na marafiki basi mke kusoma ndani ya ndoa ni ngumu mno. Wengine waliokuwemo ndani ya ndoa hupata bahati na kupata scholarship nchi za nje kwa Masters na kama watafanya vizuri basi wataunganisha na PhD. Sasa ukute ndio wana watoto wadogo mume anaweza kutumia sababu ya kuwa na watoto wadogo kumkatalia mwenzie kujiendeleza kielimu kwa kudai watoto wanahitaji "mapenzi ya mama" na kama ndugu, jamaa na marafiki wanampa maneno ya kutomruhusu mwenzie na mume ni rahisi kuyumbishwa basi ndio imetoka hiyo, lakini mke akibahatika kuwa na mume muelewa atamwambia nenda mwenzangu kwani elimu yako si kwa manufaa yako tu bali pia kwa manufaa ya familia yetu. Watoto wadogo ndio lakini mie nitajitahidi sana kuona hawakosi mapenzi yangu kama baba.
Last edited by a moderator: