Annina
JF-Expert Member
- Nov 15, 2009
- 437
- 57
Hapo kuna mengi ya kutafakari, hawa wazee wakati mwingine wanapotoka. Kuna mzee mmoja amekataa kumuozesha binti yake kwa visingizio kibao, mara tunda la kuvundika si sawa na la kuivia mtini akimaanisha hata kijana akikubali kubadili dhehebu bado asingefaa maana kijana ni mkatoliki na binti ni msabato. Sasa binti ana watoto 3 bado yupo kwa baba ake... watu wanajiuliza ni kweli dhehebu linaweza kusababisha yote haya au mzee ana agenda ya siri na binti yake?
Annina
Annina