Ni mahusiano ya miaka
saba, na mtoto wa miaka 5, hawajaoana
Mwanzoni wa mahusiano ndugu za mwanaume hawakumtaka mwanamke kwa kuwa
ana imani tofauti, lakini mwanaume aling'ang'ana
wamejenga nyumba mbili pamoja moja ipo Dar moja Kijijini kwa mwanaume.
mwanaume anaishi kwenye nyumba ya Dar, mwanamke anaishi kwa wazazi wake.
Tangu 2010 mahusiano yamekuwa ni machungu kwa mwanamke mana alikuwa
akipaa lugha za kejeli, matusi, vipigo na kutojaliwa. wameacha zaidi ya
mara tano na kurudiana.
Kuna kipindi mwanamke aliambiwa hakupendwa, aliumia akalia lakini bado
alimsamehe. wakaendelea.
katika siku saba za wiki watafurahi kwa siku moja au nusu siku the rest
ni maumivu kwa mwanamke.
sometime mwanamke alikuwa akimuambia kuwa atachoka,lakini kidume atasema
"utaenda wapi wewe", "mie siachwi".na maneno kedekede ya kejeli.
akiombwa waongee anasema "wimbo wa taifa"
sasa mwanamke kachoka amemuacha huyu kijana tangu mwaka jana May lakini
kidume kilijua ndo yaleyale atarudi tu.mpaka navyoandika hapa mwanamke
kashikilia msimamo wake.
kuna usemi unasemwa 'what goes around come around'. ndo yanayomkumba
mwanaume sasa.kapita kwa ndugu wote, rafiki wote,anamfwata nyumbani na
kazini, bi dada hamtaki.kafikia hatua ya kulia kama mtoto aliyepigwa,bi
dada wapii.sasa kafikia hatua mbaya ya kusema atajiua. je anaweza
kujiua kweli au mkwala, je amtafutie watu wa kuongea nae au nini
afanye?ni maswali anajiuliza bi dada hapati jibu. ndo nimeamua kuleta
jamvini, mana Hapo bi dada kaogopa, hajui afanyeje,mana hataki kurudi
mana anasema aliteseka sana, na amepata anayemthamini na kumpenda kwa
dhati.
Anahitaji ushauri wenu wa busara wajameni.