Ushauri unahitajika kunusuru roho ya mtu!

Ushauri unahitajika kunusuru roho ya mtu!

Kama hivyo ndivyo basi tena, haina haja basi, amwambie wazi kuwa haiwezekani na nakuhakikishia jamaa hawezi kujiua.

Sorry niulize, bidada kashapata pumziko lingine la moyo nini?

Hata kama anaweza jiua kwani yeye tatizo lake nini.....
 
at the end of the day “Mja asili haachi asili akiacha asili hana akili” kama kashindwa kubadilika ndani ya miaka saba its enough mwambie huyo bibie hongera zake kwanza kwa maana hana kosa
 
wajameni ya leo ndo kali zaidi. nimetoka kuongea na biadda anasema kapigiwa simu na pastor wawili wa makanisa tofauti wanataka kuongea nae jamaa kaenda kuwaomba ushauri na kuwaomba waongee na bidada.

Pastor A ametaka kusikia story ya bidada pia baada ya kuisikia amemwambia mama live your life huyo jamaa atakudhuru anahitaji psychological help na pastor kajitolea kumsaidia kama jamaa atakubali.

Pastor B kwamwomba bidada waonane ana kwa ana ili asikie kutoka kwake ndo pastor yuko njiani kwenda ofisini kwa bidada.

mwe!!!makubwa
 
Ni mahusiano ya miaka
saba, na mtoto wa miaka 5, hawajaoana

Mwanzoni wa mahusiano ndugu za mwanaume hawakumtaka mwanamke kwa kuwa
ana imani tofauti, lakini mwanaume aling'ang'ana

wamejenga nyumba mbili pamoja moja ipo Dar moja Kijijini kwa mwanaume.
mwanaume anaishi kwenye nyumba ya Dar, mwanamke anaishi kwa wazazi wake.

Tangu 2010 mahusiano yamekuwa ni machungu kwa mwanamke mana alikuwa
akipaa lugha za kejeli, matusi, vipigo na kutojaliwa. wameacha zaidi ya
mara tano na kurudiana.

Kuna kipindi mwanamke aliambiwa hakupendwa, aliumia akalia lakini bado
alimsamehe. wakaendelea.

katika siku saba za wiki watafurahi kwa siku moja au nusu siku the rest
ni maumivu kwa mwanamke.

sometime mwanamke alikuwa akimuambia kuwa atachoka,lakini kidume atasema
"utaenda wapi wewe", "mie siachwi".na maneno kedekede ya kejeli.
akiombwa waongee anasema "wimbo wa taifa"

sasa mwanamke kachoka amemuacha huyu kijana tangu mwaka jana May lakini
kidume kilijua ndo yaleyale atarudi tu.mpaka navyoandika hapa mwanamke
kashikilia msimamo wake.

kuna usemi unasemwa 'what goes around come around'. ndo yanayomkumba
mwanaume sasa.kapita kwa ndugu wote, rafiki wote,anamfwata nyumbani na
kazini, bi dada hamtaki.kafikia hatua ya kulia kama mtoto aliyepigwa,bi
dada wapii.sasa kafikia hatua mbaya ya kusema atajiua. je anaweza
kujiua kweli au mkwala, je amtafutie watu wa kuongea nae au nini
afanye?ni maswali anajiuliza bi dada hapati jibu. ndo nimeamua kuleta
jamvini, mana Hapo bi dada kaogopa, hajui afanyeje,mana hataki kurudi
mana anasema aliteseka sana, na amepata anayemthamini na kumpenda kwa
dhati.

Anahitaji ushauri wenu wa busara wajameni.

kujiua hawezi anamtisha tu huyo dada. Dada naye ashikilie msimamo wake kwani akirudi yatakuwa yaleyale kamwe asikubali mtu amuumize makusudi
 
jamani nawapa update ya story hapo juu.

jamaa kachanganyikiwa sasa hivi yeye anaenda from one church to another kuomba pastors wamsaidie kuongea na bidada. bidada kashikilia msimamo wake.mawifi wanamwambia kaka yao akifa ajue yeye ndo kamuua kwanini asimsamehe na ajifunze kumpenda tena kama mapenzi hakuna kabisa. bidada kagoma bwana kawaambia ataenda polisi kureport ili hata akifa awe alishatoa polisi.

nahisi kama movie vile.mh|!
 
Pumbaaaf! Mwambie ashikilie msimambo wake huyo anatishia nyau. Km atajiua ajiue 2. Shenz zake malipo hapahapa dunian machungu alokua anayapata bidada yanamrud. Cnaga huruma na wanaume wa dizain hiyo ningekua mim ningemnunulia sumu, kamba na kisu achague mwenye pumbaf zake.
 
Wadau ningependa kuwapa feedback ya hili songombingo la bidada shosti.

Wiki kama mbili zilizopita jamaa kaanza tena kumsumbua bidada kwa style tofauti sasa sio kujiua tena, alikuwa anaenda kazini kwa bidada anakaa nje akimwona analiiiia na kupiga magoti asamehewe claiming that he loves her,bi dada akaitwa na baba mkubwa wa jamaa akamsikiliza yule baba akamwambia kuwa anaheshimu maamuzi yake mana at the end of the day she knows him well kuliko mtu yeyote.

mkaka akaamua kumtishia bidada kuwa akimuona na mtu yoyote damu itamwagika. bidada akaogopa akaenda polisi, ikafunguliwa file pale akaitwa na mpelelezi kueleza na yule jamaa akaitwa, heee!kushangaa yule polisi akamuita bidada kesho yake anaanza kumbembelezea jamaa eti amrudie maana wana mtoto na blabla kibao.yule bidada amekaza uzi na kumwambia sasa hivi ana mtu ambaye yuko nae serious, hee!polisi kumwambia bidada basi usiolewe mimi naenda kwenye course ya miezi mitatu nikirudi nitakutafuta tuongee vizuri..hahaha polisi nae anataka kujiopolea badala ya kudeal na case, ovyo kabisa.

sasa bidada anasema yuko kwenye wakati mgumu sana hajui afanyeje mana jamaa ndo hivyo hataki kuelewa na mtu aliyenae sasa hivi yuko serious kiukweli na hapendi kuona jinsi mdada anatumiwa mamsg na kupigiwa simu na jamaa kila saaa ingawaje bi shoti hapokei ila anasema je itaendelea hivyo hata wakioana ina mana ya kwamba ndo yao haitakuwa na amani? kachanganyikiwa shostito.
 
Hakuna mwanzo usio na mwisho itafika tuuu wala mwambie asi panic kihiivyooo
E023.png
 
  • Thanks
Reactions: Hun
Back
Top Bottom