Ni mahusiano ya miaka saba, na mtoto wa miaka 5, hawajaoana
Mwanzoni wa mahusiano ndugu za mwanaume hawakumtaka mwanamke kwa kuwa ana imani tofauti, lakini mwanaume aling'ang'ana
wamejenga nyumba mbili pamoja moja ipo Dar moja Kijijini kwa mwanaume. mwanaume anaishi kwenye nyumba ya Dar, mwanamke anaishi kwa wazazi wake.
Tangu 2010 mahusiano yamekuwa ni machungu kwa mwanamke mana alikuwa akipaa lugha za kejeli, matusi, vipigo na kutojaliwa. wameacha zaidi ya mara tano na kurudiana.
Kuna kipindi mwanamke aliambiwa hakupendwa, aliumia akalia lakini bado alimsamehe. wakaendelea.
katika siku saba za wiki watafurahi kwa siku moja au nusu siku the rest ni maumivu kwa mwanamke.
sometime mwanamke alikuwa akimuambia kuwa atachoka,lakini kidume atasema "utaenda wapi wewe", "mie siachwi".na maneno kedekede ya kejeli. akiombwa waongee anasema "wimbo wa taifa"
sasa mwanamke kachoka amemuacha huyu kijana tangu mwaka jana May lakini kidume kilijua ndo yaleyale atarudi tu.mpaka navyoandika hapa mwanamke kashikilia msimamo wake.
kuna usemi unasemwa 'what goes around come around'. ndo yanayomkumba mwanaume sasa.kapita kwa ndugu wote, rafiki wote,anamfwata nyumbani na kazini, bi dada hamtaki.kafikia hatua ya kulia kama mtoto aliyepigwa,bi dada wapii.sasa kafikia hatua mbaya ya kusema atajiua. je anaweza kujiua kweli au mkwala, je amtafutie watu wa kuongea nae au nini afanye?ni maswali anajiuliza bi dada hapati jibu. ndo nimeamua kuleta jamvini, mana Hapo bi dada kaogopa, hajui afanyeje,mana hataki kurudi mana anasema aliteseka sana, na amepata anayemthamini na kumpenda kwa dhati.
Anahitaji ushauri wenu wa busara wajameni.