Jana rafiki yangu kanipigia simu kuniomba ushauri kuhusu kutokuelewana na mkewe wa ndoa kuhusu simu ya mkononi,jamaa ni mfanyakazi mwajiriwa na mama nimfanya biashara na biashara yenyewe ni jamaa mwenyewe katoa mtaji,sasa anasema usiku wa jumamosi kuamkia jana jumapili mkewe aliingia bafuni yeye akawa yupo kitandani, akachukua simu ya mkewe na kuanza kusoma sms,mama alipo toka bafuni akakuta mzee anasoma sms,mkewe akamuuliza mbona unapenda sana kupekua simu yangu?jamaa naye akamuuliza kwani niipekua kuna shida gani?asema mkewe alikuja juu na kumuonya siku akikuta ameshika simu yake tena na anaipekua ataivunja hiyo simu,sasa jamaa ndo kaja kwangu kuniomba ushauri yeye anasema kweli mke wake ni mwaminifu tena kama mwanzo?hakuna lililojificha ndani hapo?hivyo kabla sijampa ushauri nikaona ni vema na mimi niwashirikishe,hiki kisa ni cha kweli kabisa hivyo ushauri uwe wa kweli ni watu wapo ndani ya ndoa kwa miaka kumi sasa,asanteni