Ushauri / Ujumbe kwa JWTZ

Mpori pori twende taratibu usikimbie nataka tuone kati yangu mimi na wewe nani shule alienda na yupi hakwenda.

Mpori pori unasema Jeshi la Wananchi(JWTZ/TPDF) ni taifa ndani ya taifa sio?kwasababu wana hospitali zao,mahakama zao(hizi ni hoja zako mpori pori)

Sawa uko sahihi.Kwahiyo na Roman Catholic ni taifa ndani ya taifa? maana wana shule zao,makanisa yao na hospitali si ndio.

Taifa ni nini mpori pori kwa uelewa wako?

Taifa ni mjumuisho wa watu wenye utamaduni wao,mipaka inayotambulika na mataifa mengine,sheria na miongozo mingine wakiwa wanaongozwa na kiongozi ambaye anaweza kuwa rais,malkia au mfalme kulingana na mfumo wa utawala wa taifa husika.

Hiyo ni tafsiri nyepesi mpori pori, haya nambie mipaka ya JWTZ hiko wapi?utamaduni wao ni upi?

Ukijibu vizuri ntakubali kwamba umenizidi
 
Jeshi halihitaji imani au kupendwa na wananchi

Ni taasisi nyingine kabisa, ina sheria zao, hospitali zao, maduka yao, mahakama zao na maisha yao

Hawahitaji imani wala kupendwa na mtu
Umekurupuka...!
 
Pakitokea vita Kati ya JWTZ na jeshi la nchi jirani, JWTZ watachakaa vibaya mno Kwa sababu raia hasa vijana tutawachoma sana jwtz Kwa kutoa ushirikiano Kwa majeshi adui.
😂😂
 
Kuna watu mmesoma shule za ajabu Emma high school ndo takataka gani?
 
Kwahiyo mlitaka jeshi liungane na vibaka kufanya mapinduzi ? Niwakumbushe tena, wale hawana Cha kuwafanyia ili muwaone ni watu safi. Jw haikuvunja mwiko wowote wa kimaadili na kisheria katika majukumu Yao siku zile. Kilichotokea ni vijana wachache kati Yao waliokuwa na mawazo ya kuungana na vibaka siku Ile.
 
Hakuna JESHI hapo.


Kuna MILITIA ya KIKWETE na MATAPELI.

Hizo mission unazoita, HAKUNA ndio maana huoni cha maana.

Juzi hapo wametoa STOO helkopta mpaka mbovu kutishia watu.

Hakuna JESHI timamu limewahi, kugeuzia SILAHA za KIVITA RAIA wake lenyewe.
 
Kilichotokea ni vijana wachache kati Yao waliokuwa na mawazo ya kuungana na vibaka siku Ile.
Soma tena ulichoandika...ulitaka kusema nini!?

Hao unaoita vibaka ni watanzania kama wewe waliotokana na utawala mbovu wa hii serikali.
Hukumu ya mtu kuwa kibaka sio kuuliwa kama ngedere.
Hii nchi ina mifumo ya kisheriia, Kama walikosa wangehukumiwa kisheria.

Jeshi lilijidhalilisha sana kwa kukubali kutumika kisiasa.
 
Rangi ya damu ya mzee🤣
 
Shule ya ajabu unajua hiko nchi gani?Haiko Tanzania acha wenge wewe
Kutokuwa Tanzania haihalalishi Kuwa umesoma shule ya ajabu, jina tu limekaa kimchongo kama open school
 
Kutokuwa Tanzania haihalalishi Kuwa umesoma shule ya ajabu, jina tu limekaa kimchongo kama open school
Uliza waliosoma Uganda au wanaojua Kampala ni sawa na mtu awe nje ya Tanzania ukimwambia kuna shule kama Tusiime, Feza , kaizirege,Waja,Marian si atasema kama wewe.Siwezi kulaumu tu sema ulizia wanaojua watakusaidia.

Never judge book by its cover(wamakonde wanasema)
 
Haya wewe una akili, Furahi sasa

Kama jeshi ni la wananchi katisha kizembe kambini kwao sababu wewe ni mwananchi uone kibano chake
Hiki ulichokisema hapa kwa hii comment ni moja ya kiashiria kuwa na jeshi la ovyo sana la watu wasiotumia akili hata kidogo, halijui kutengeneza uhusiano mzuri na wanainchi... na ndio maana wanainchi tulio wengi tunalichukia.

Kumpa adhabu raia kisa tu amekatisha kwenye kambi ya jeshi ni upumbavu wa hali ya juu, huo ujinga huwezi kuskia kwenye majeshi bora duniani.

Unasema kuwa jeshi halihitaji kupendwa na wanainchi, aisee basi una akili za kitoto sana, sidhani kama unajua hata moja ya sababu zilizofanya JWTZ wakamkimbiza Amin ilikuwa ni ushirikiano mzuri walioutoa waganda kwa wanajeshi wetu.
 
HUYO MTU NI MJINGA!
ANAANDIKA UPUMBAVU.
 
Haya wewe una akili, Furahi sasa

Kama jeshi ni la wananchi katisha kizembe kambini kwao sababu wewe ni mwananchi uone kibano chake
Kwahiyo kazi ya Jeshi na uwezo wake ni kupambana na kina JUMA KIDUKU.
 
Jeshi halihitaji imani au kupendwa na wananchi

Ni taasisi nyingine kabisa, ina sheria zao, hospitali zao, maduka yao, mahakama zao na maisha yao

Hawahitaji imani wala kupendwa na mtu
Hayo uliyosema ni kwa majeshi ya Ulaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…