Nakupa pongezi sana kwa kupata wazo la kuanza kujitegemea,hii ni hatua moja katika kujitambua,nakupongeza maana
::
Yeyote anaedhani kuwa bila baba,mama kaka au dada maisha hayawezekani,kila kitu kitaisha,labda atakufa kesho yake n.k Basi mtu huyo hajafikia ukomavu wa kiakili.
::
Kujitegemea unakotaka hakuna maana,utafute uhuru wa kufanya unayotaka mema kwa mabaya,la! Kuna maana uzingatie misingi ya maadili uliyofunzwa,linda maisha yako usisahau Kila mchuma janga hula na wa kwao.
::
Mambo ya msingi yatakayo kupa kibali cha kujitegemea au kuishi mbali na wazazi wako ni pamoja na KAZI HALALI inayojulikana,USALAMA wa maisha yako na MAWASILIANO ya uhakika kwa familia yako.Nadhani ukiwahakikishia kwa vitendo wazazi wako mambo hayo watakuwa radhi kukubalia.
::
Mwisho,usiogope maisha,wapo vijana wengi ambao unawazidi umri na maisha yao yana dira nzuri,wengine hawakupata bahati ya kuchungwa au kulelewa na wazazi wao(ni yatima) lakini wana maisha mazuri.Usiogope shida,,shida huleta maarifa..wakati ndio sasa,AMUA NI MAISHA YAKO.
=