Ushauri tafadhali: Wanangu wanakoelekea siko

Ushauri tafadhali: Wanangu wanakoelekea siko

mito

JF-Expert Member
Joined
Jun 20, 2011
Posts
10,811
Reaction score
11,028
Wakuu nina vijana wangu wawili, wa kike na wa kiume. Wote wako high school sasa. Kimasomo naona kama wanaenda vizuri ila kimaadili napata shaka kidogo hadi nimeamua kuomba muongozo kwa wadau wenzangu hapa.Wako shule tofauti na huwa nawasiliana nao kwa simu, call na texts.

Sasa mimi baba yao nilikuwa nyuma kidogo na hii technology ya whatsApp, simu yangu ilikuwa haisupport hii huduma halafu pia nilikuwa sina munkari nayo kivile. Sasa majuzi hapa nimenunua simu ya kisasa kuliko niliyokuwa nayo mwanzo ni hizi smartphone.

Sasa na mimi ndo sasa nikaamua kujiunga na haya ma-whatsApp. Katika kupekenyua huku na kule si nikaingia kwenye profile zao, daah. Vilivyoko huko sikutegemea kabisa, hayo maneno sasa ya malavidavi kwenye status zao, na yanavyobadilishwa kila siku, khaa nimechoka mwili na roho na hizo picha hivyo vivazi sasa ndo mimeishiwa nguvu kabisa, hata sijawahi waona wakivivaa nyumbani na hata sijui wanavipata wapi.

Kama mzazi najitahidi sana kuongea na wanangu, hadi huwa najipa imani kuwa wananielewa ila haya mambo yao ya kwenye mitandao ndo yamenipa mashaka sasa. Sijawauliza chochote hao watoto na wala hata wife sijamshirikisha. Nimeona nije kwanza kupata ushauri wenu kwa kunijibu mambo yafuatayo.

Je na wewe kama mzazi ulishawahi ona mambo kama hayo kwa vijana wako we uliyachukuliaje.Je haya ni mambo ya kawaida tu katika ulimwengu wa sasa hivyo niyapuuze,je nifanyeje mimi kama mzazi.

NB: Team kuponda tafadhali piteni tu huko pembeni, nitawashukuruni sana.
 
weka hapa picha hizo ndipo tutoe ushauri.
 
Wana umri gani? Huenda puberty inawasumbua lakini angalia isiwachukue moja kwa moja... Cha zaidi wakabidhi mikononi mwa Mungu awaepushe na ya dunia...
 
Wana umri gani? Huenda puberty inawasumbua lakini angalia isiwachukue moja kwa moja... Cha zaidi wakabidhi mikononi mwa Mungu awaepushe na ya dunia...

Mkuu average age ya watoto wa high school hujui.Ila asante kwa ushauri, nitazidi kuwaombea mkuu
 
Kaunga leo nimekuona hapa jukwaani, i want to hear something from you. Of course from others as well
 
Last edited by a moderator:
aisee wakirudi likizo kaa nao chini waeleze hilo mitandao inaharibu sana hasa kama unatumia ndivyo sivyo
 
Jifunze kuwaelewa, usitake wafuate 100% unayoyataka/kuyapenda kwa sababu dunia yako inazeeka kama ulivyo mzee, hawawezi kuvaa bugaloo ulilovaa enzi zako kwa madai ni maadili mema, usiwatenge wanao kutoka dunia yao, shukuru hawavai mbele yako (ina maana wanakuelewa na kukuheshimu) huko kwenye mawasapu umewafuata mwenyewe uwe mpole.
Sio kwamba nawaunga mkono la hasha, nimesimulia kaukweli kanakotukabili, nyinyi mmezoea kuziita changamoto.
 
Mie kwa maoni yangu mshirikishe mkeo kuhusu hili na mkae chini kuongea kwa kina. Watoto wenu watakaporudi likizo mkae kama familia mkae tena kuongea kwa kina na kuonyesha kutoridhika kwenu na mambo mliyoyaona na kuomba wayaache mara moja. Kama ni wasikivu basi haitakuwa shida kwao kuachana na yale msiyoyaafiki ila ufuatiliaji wa kila mara ni muhimu sana. Kulea watoto hasa wa rika hilo katika hii dunia ya leo na huu utandawazi ni mtihani mkubwa. Kila la heri.
 
nimejaribu kusoma maandishi yako matamko yako hayaendani na ulicho kipost, nikama unachezea watu akili

Mkuu si unaona mzazi mwenyewe ni wa dotcom? huyu mzazi walah hafananii kujiita mshamba wa dotcom. Watoto kwa umri huo haya mambo ni lazima!
 
Sasa vivazi vya huyo wa kiume vikoje?
 
Halafu peleleza kupiti mama yao ujue wanao wanakuita jina gani.

1. Mshua
2. Mdingi/dingi

Ikiwa wanakuita kwa namba moja basi ujue wanakukubali jinsi unavyoitikia maombi yao.

Na ikiwa wanakuita kwa jina la namba mbili ujue wanachukia baadhi ya taratibu zako ambazo wanaziita za kikoloni.
 
Jifunze kuwaelewa, usitake wafuate 100% unayoyataka/kuyapenda kwa sababu dunia yako inazeeka kama ulivyo mzee, hawawezi kuvaa bugaloo ulilovaa enzi zako kwa madai ni maadili mema, usiwatenge wanao kutoka dunia yao, shukuru hawavai mbele yako (ina maana wanakuelewa na kukuheshimu) huko kwenye mawasapu umewafuata mwenyewe uwe mpole.
Sio kwamba nawaunga mkono la hasha, nimesimulia kaukweli kanakotukabili, nyinyi mmezoea kuziita changamoto.

asante sana mkuu nimekuelewa
 
Halafu peleleza kupiti mama yao ujue wanao wanakuita jina gani.

1. Mshua
2. Mdingi/dingi

Ikiwa wanakuita kwa namba moja basi ujue wanakukubali jinsi unavyoitikia maombi yao.

Na ikiwa wanakuita kwa jina la namba mbili ujue wanachukia baadhi ya taratibu zako ambazo wanaziita za kikoloni.

Daah, hili nalo neno! Ukweli sikuwahi kufikiria kuhusu hili
 
Mie kwa maoni yangu mshirikishe mkeo kuhusu hili na mkae chini kuongea kwa kina. Watoto wenu watakaporudi likizo mkae kama familia mkae tena kuongea kwa kina na kuonyesha kutoridhika kwenu na mambo mliyoyaona na kuomba wayaache mara moja. Kama ni wasikivu basi haitakuwa shida kwao kuachana na yale msiyoyaafiki ila ufuatiliaji wa kila mara ni muhimu sana. Kulea watoto hasa wa rika hilo katika hii dunia ya leo na huu utandawazi ni mtihani mkubwa. Kila la heri.

Asante sana mkuu BAK ila umeninyima kamwimbo ka kusindikizia!!
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom