BASIASI
JF-Expert Member
- Sep 20, 2010
- 9,735
- 5,003
Kwenu wahusika!
Tunakuwa na foleni zisizo na tija kabisa muda wa jioni kuanzia Kibo kwenda Kimara na muda mwingine hadi Stopover.
Mh mkuu wa kanda maalum, tunaomba njia mbadala kuondoa hizi foleni service road zitumike. Huzuni imekuwa ni sehemu ya watu kupigia faini zao.
Wanaokaa Kimara DAWASCO
Hivi sasa kuna njia imetengenezwa vizuri tu, mnaweza mkaona mtu anaekwenda Kimara DAWASCO badala ya kukaa foleni anatumia service road mpaka bucha. Anaingilia mataa ya Kibo pale anapandisha Korogwe inakwenda mpaka njia ya kuingilia DAWASCO Kimara hapo unaokoa magari mengi kukaa mainroad.
2) Wanaoishi Baruti na Bucha na Korogwe, kiuhalisia hawa watu wangeweza kusaidiwa na service road. Wakifika Kibo mataa wanaingia service road wanaokaa vinane wanaingilia pale Msikitini, wanaoenda Bucha wakifika kwa Thomas Lyimo waanaenda moja kwa moja makwao.
Wale wa Korogwe badala ya kusubiri foleni wanaambaa na service road mpaka Kanisani wanaingia makwao.
Inasikitisha hata sisi tunaowahi ibada za jioni kwa mastaha unakuta ibada ndio imeisha ama unakuta watu wamekaa pale mataa upande a service road inabidi sadaka ujigaie kwenye gari mwenyewe ama utafute nyama choma karibu
Naamini hata njia kuu itabaki na malori tu na baadhi ya magari ya Kimara Bonyokwa nk. Tunaomba msaada wenu kwa hili, hivi sasa ikifika saa kumi na moja hujapita unakaa foleni saa moja, Kibo kuiona Baruti ama Kimara
Tunakuwa na foleni zisizo na tija kabisa muda wa jioni kuanzia Kibo kwenda Kimara na muda mwingine hadi Stopover.
Mh mkuu wa kanda maalum, tunaomba njia mbadala kuondoa hizi foleni service road zitumike. Huzuni imekuwa ni sehemu ya watu kupigia faini zao.
Wanaokaa Kimara DAWASCO
Hivi sasa kuna njia imetengenezwa vizuri tu, mnaweza mkaona mtu anaekwenda Kimara DAWASCO badala ya kukaa foleni anatumia service road mpaka bucha. Anaingilia mataa ya Kibo pale anapandisha Korogwe inakwenda mpaka njia ya kuingilia DAWASCO Kimara hapo unaokoa magari mengi kukaa mainroad.
2) Wanaoishi Baruti na Bucha na Korogwe, kiuhalisia hawa watu wangeweza kusaidiwa na service road. Wakifika Kibo mataa wanaingia service road wanaokaa vinane wanaingilia pale Msikitini, wanaoenda Bucha wakifika kwa Thomas Lyimo waanaenda moja kwa moja makwao.
Wale wa Korogwe badala ya kusubiri foleni wanaambaa na service road mpaka Kanisani wanaingia makwao.
Inasikitisha hata sisi tunaowahi ibada za jioni kwa mastaha unakuta ibada ndio imeisha ama unakuta watu wamekaa pale mataa upande a service road inabidi sadaka ujigaie kwenye gari mwenyewe ama utafute nyama choma karibu
Naamini hata njia kuu itabaki na malori tu na baadhi ya magari ya Kimara Bonyokwa nk. Tunaomba msaada wenu kwa hili, hivi sasa ikifika saa kumi na moja hujapita unakaa foleni saa moja, Kibo kuiona Baruti ama Kimara