Ushauri: Serikali msumari wa Mwisho pigeni hapa

Ushauri: Serikali msumari wa Mwisho pigeni hapa

Wauza unga wananguvu ndio ila mm namini ukiamua inawezekana hawa jamaa kuwapangua
 
Hayo mambo kusema Haiwezekani yamepitwa na Muda.. Zama zimebadilika kaka
Nayaona ndomana nakwambia haiwezekani nenda bandarini rafu zinachezwa mpaka muda huu japo rais alikuwa huko ukija kwenye utakatishaji wa pesa ni kama kumsukuma mlevi
 
Hivi unawazungumzia GSM au hawa huwazungumzii kisa kwa sasa wanafadhilini au nawe umekuja kututoa kwenye direction Bashite wa koromije weka vyeti acheni bla bla
 
Biashara hii inatokana na uwezo wa ku laundry money!... Tanzania mchezo umeiva Sana wasanii, wanasiasa, wanaojifanya watu wa MUNGU, wafanyabiashara wakubwa yaani watu wanaingia na tones of money na kuondoka nazo bila kuulizwa.

Benki zetu zinabadilisha fedha kama vile ni mchezo wa kawaida kwa hiyo Mafia wote wa Europe wamekita Bongo wakinunua Unga na kuusambaza duniani.

Pamoja na kwamba bei yetu ni kubwa, sasa hivi Unga utatumika kuzalisha crack na aina nyinginezo ambazo zinauzwa sana na vijana wadogo ktk ma club ulaya na North America, Japan na kadhalika.

This is big business kwa hiyo kuivunja hii biashara magufuli huna budi kuanza na kuvunja money laundry nchini, sheria kali katika benki zetu na kuondoa kabisa uwezo wa mtu kuingia na kutoka nchini na kiasi chochote cha fedha za kigeni bila kibali maalum toka benki ya ndani ama nje.

Pia Bank to Bank transfer ziwe zinachunguzwa zaidi na kibali hakitoki kwa mtu mmoja tu.

Nakupongeza Sana Kwa kuanza kuvunja Mafia mob yenyewe ambayo inahitaji nguvu ya dola!.... problem kubwa ni kwamba kweli watu wanawafahamu watu wengi wanaohusika lakini wamejifanya kuwasahau.

Mnataka mkatapeli wapi tena? Hayo magari m,fedha na nyumba amjaridhika tu?
 
Mafia Mob? Unaifahamu au unaishia kuisoma kwenye mitandao? Magufuli maisha yake yote hataweza ivunja zaidizaidi anaungana nao taratibu ni vile tu kachagua nae upande wake ambao upo tofauti na wengine na money laundry ni kama maji lazima uyanywe au kuyaoga ili usinuke shombo.
Ni sawa na bandari hawawezi acha kupiga madili hata ikawaje utawatoa wengine watakao ingia wataendeleza ni cheni ambayo inarithi
Pale bandarini dili hazifi nyerere mwenyew alichemka mamaeee
 
Magufuli yape dozi baba yanasambaza hela watu wazungumzie vyeti na kuvamiwa kwa clouds studio
 
Unaanzisha uzi wewe na unajijibu wewe mwenyewe mwaka huu kazi ipo kila mtu kavurugika tulieni dawa iwaingie
 
Hakuna cha nani wala nani lazima Taifa linyooshwe kwani huyo Nape alivyo kuwa anashadadia swala la makonda nakuundabtume haraka huku akishirikiana na wapinzani ilikuweje
 
Mwaka 2013 alipofariki Alibert Mangwea kulizuka tafrani kubwa miongoni mwa wasanii wakituhumu wamiliki wa Clouds Media kuwa ndio chanzo cha kifo chake!
Nakumbuka P Funk Majani alivyokuwa akilia kama mtoto huku akisema hata yeye azikwe ila kazi ama nyimbo za wasanii zilizotengenezewa Bongo Records zisipigwe kabisa kwenye Media zote za Clouds.

Labda niweke kumbukumbu sawa, mnamo tarehe 27/5/2013 usiku nchini Afrika Kusini alifariki msanii Albert Mangwea (Ngwea ) ambapo kwa taarifa zilizothibitishwa na madaktari waliomfanyia upasuaji ni kuwa jamaa alikuwa amebeba dawa za kulevya tumboni mwake na kwa bahati mbaya zilichelewa kutoka na zikapasukia tumboni na kupelekea kuzidiwa na alipofikishwa hospitali akawa amekata roho

P Funky akiwa ndiye mtu wa karibu sana wa Ngwea akasema biashara waliyokuwa wanamfanyiza akina Ruge Mutahaba aliwawi kumkataza asiifanye lakini akawa anajificha na kupeleka mzigo kama kawaida na matokeo yake akaja kufa na mzigo tumboni!

Hili nimeona niweke kwanza kumbukumbu sawa kisha tuangalie sasa hilo linaloendelea.
Binafsi sipendi niingilie story katikati kabla taswira ya picha kamili kuanza kujichora!
Sasa rangi zimeanza kuonekana.

Siku za hivi karibuni RC wa Dar es Salaam Paul Makonda alivamia ofisi za Clouds media akiwa na vijana toka special unit baada ya kupewa taarifa za biashara iloyokuwa ikifanyika kule ndani nyakati za usiku.

Baada ya lile tukio uongozi wa clouds media ulikaa kimya, ili kutaka kujisafisha wakatengeneza clip fake ambayo kwa kuanza inamuonesha kweli Paul Makonda alivyoingia kule ndani kwa masada wa CCTV camera. Wakaenda wakamtafuta mwanamke mwenye mtoto eti anajifanya mpenzi wa Josephat Gwajima, na baadae vile vipande wakaviunganisha ili vitengeneze habari!
Kweli wakafanikiwa kuwateka wasio na uwezo wa kuchambua mambo.
Juzi Ruge Mutahaba akiwa anaonekana kabisa kudanganya kwenye kipindi cha 360 akasema walivamiwa na Makonda akitaka ile clip irushwe alihali yeye alikataa. Akaendelea kusema vijana wa SHILAWADU waliogopa wakawa wameshikwa na presha.
Ni Logic tu ndogo, mtu ambaye unashinda naye nyumbani kwako akiwa na polisi wenye bunduki siku akija kwako usiku tena wa saa nne utaogopa mpaka udondoke kwa presha?

Ile siku ambayo anatoa maelezo Ruge kwa kujichanganya tu eti kati ya watu walokuwa wakimhoji ni Masoud Kipanya ambaye wakati nikiwa mitaa fulani Dar vijana wakanitonya jamaa naye ni pusha mzuli tu. Nikawauliza, mnamsema Masoud mwingine au huyu Kipanya? Wakanambia brother wewe si wa mkoani tu, unajua nini kuhusu Dar?
Nikanyamaza, story ikakata.

Leo Gwajima kawatembelea Clouds eti kuwapa pole kwa kilichowakuta, kapokelewa kama mungu wa pili pale clouds. Mwenye akili kwa kichwa atajua kuunganisha hili fumbo!

NAPE NNAUYE
Huyu tatizo hawakumwamini tangu mapema na kumshirikisha katika mambo haya. Kila kilichofanyika hakuwa sehemu yake mpaka alivyojulishwa juzi usiku tena kwa kuitwa ikulu.
Nape hakujua hata wale vijana ni wapi walioenda na Makonda.
Labda kwa wasiojua Wale wanaitwa Cobra CC9-H. Hawa ni kikosi maalumu ambacho ndani yake kuna Black Agents, Eagle, ISS-011 HP-Spiers. Hawa wana mafunzo ya hali ya juu kuliko kawaida, na Command yao iko kwa Rais na TISS Director General tu.

Sasa Nape kwakuwa yeye ameishi maisha yake yote kwenye usemaji tu akataka aendeleze fani yake.

Tume aliyounda kuchunguza ilipigiwa simu usiku ule ule. Na sasa kaelewa kinachoendelea.

Rai yangu kwa vijana wenzangu, tusifanywe mavuvuzela ya wauza madawa ya kulevya hasa sisi tunaojiita learned (elites ) bali sisi tuwe ndio mstari wa mbele kupigania taifa letu.
Kwenye siasa tujadili tu, tusemane, tukosoane n.k ila kwenye masuala ya kitaifa tuungane kutetea maslahi ya kitaifa. Tuungane kukemea uovu, tuungane kutetea uhai wa vijana wenzetu!

Leo ni wao, kesho ni watoto wetu na wadogo zetu!

Mungu ibariki Tanzania, Mungu tubariki vijana!

By Maroah Kissiry
 
Okoa Tanzania, pambana dhidi ya #UPUNGUFU_WA_AKILI_KICHWANI(UWAKI)
 
Back
Top Bottom