Ushauri: RITA imekosa umakini, ivunjwe

Ushauri: RITA imekosa umakini, ivunjwe

mandokwa

JF-Expert Member
Joined
Jun 5, 2013
Posts
620
Reaction score
865
Nawasalim wakuu,

Nimekuwa mara zote nikipata shida sana kuhusu utendaji kazi wa RITA. ni kwamba, kila anayepeleka hoja ya kupata cheti cha kuzaliwa hupata bila kufanyika utaratibu wa kutafiti kama kweli ni raia au la.

Madhara yake ni kwamba hatuwezi kuwa na hakika kwamba kila anayejinadi kuwa ni mtanzania ni kweli anahaki yakuwa mtanzania.

Ukienda RITA leo ukaongea na jamaa unaweza kupata cheti hata kesho bila kupeleka evidence yoyote authentic. kismsingi cheti cha kuzaliwa ni record nyeti sana. Inakupa haki zote za tanzania kuanzia pasport na kitambulisho cha taifa. Pia kinakuruhusu kufaidika na kila service ya serikali ikiwemo kushika nyadhifa yoyote ile...

Kwakua ni jipu la mda mrefu, nashauri ifanyike reform katika hili. tuangalie jinsi bora ya kudhibiti upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa.

Tuwabadili wasimamizi lakini pia kuwe na audit sio ya kifedha bali operation audit... ni bora NIDA waongezewe madaraka au waunganishwe na uhamiaji so dhat kusiwe na gaps zinazowezesha records zetu kutokuwa consistent....

Nawasilisha,

Nangu Mandokwa
 
Mleta UZI pamoja na Archduke wote nawaunga MKONO...!!

Wageni/Wakimbizi wote, halali na haramu, kwa pamoja wanasifia MIFUMO yetu MIBOVU jinsi inavyo wawezesha kupata NYARAKA/HATI/VYETI mbalimbali pasipo uhakiki wa KINA. mfano Leseni za Udereva, Kadi ya kupigia Kura, Kitambulisho cha Uraia na Vyeti vingine mbalimbali, mambo/taratibu za upatikanaji wa vitu hivi ziko HOLELA kwelikweli....!

Ni BORA Mifumo ikabadirishwa ama kuunganishwa na idara ya UHAMIAJI (kama alivyopendekeza mchangiaji hapo juu)

Kidogo inaweza kuleta UFANISI...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwakuwa wewe ushapata ndiyo umeona watumbuliwe

ngoja wengine tupate kwanza, halafu sio kweli kwamba ukienda leo kesho unapata nakataa kwa nguvu zote
===
Jaribu kuongeanao kikubwa uone kama hupati kesho yake...
 
Mimi nilizaliwa tarehe 15 mwezi wa 7 mwaka 1990.pale muhimbili.cha ajabu nilimtajia yule mzee jina langu Na la baba..
Nilipokwenda kuchukua cheti.nikakuta kuna jina mpaka la mama.nilishangaa.kumbe kulikuwa na rekodi zangu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nawasalim wakuu,
Nimekuwa mara zote nikipata shida sana kuhusu utendaji kazi wa RITA. ni kwamba, kila anayepeleka hoja ya kupata cheti cha kuzaliwa hupata bila kufanyika utaratibu wa kutafiti kama kweli ni raia au la.
Madhara yake ni kwamba hatuwezi kuwa na hakika kwamba kila anayejinadi kuwa ni mtanzania ni kweli anahaki yakuwa mtanzania. Ukienda RITA leo ukaongea na jamaa unaweza kupata cheti hata kesho bila kupeleka evidence yoyote authentic. kismsingi cheti cha kuzaliwa ni record nyeti sana. Inakupa haki zote za tanzania kuanzia pasport na kitambulisho cha taifa. Pia kinakuruhusu kufaidika na kila service ya serikali ikiwemo kushika nyadhifa yoyote ile...

Kwakua ni jipu la mda mrefu, nashauri ifanyike reform katika hili. tuangalie jinsi bora ya kudhibiti upatikanaji wa vyeti vya kuzaliwa. Tuwabadili wasimamizi lakini pia kuwe na audit sio ya kifedha bali operation audit... ni bora NIDA waongezewe madaraka au waunganishwe na uhamiaji so dhat kusiwe na gaps zinazowezesha records zetu kutokuwa consistent....

Nawasilisha,

Nangu Mandokwa

Kaka kuna kitu unakosea, Cheti cha Kuzaliwa sio hati ya uraia, yoyote anayezaliwa Tanzania ana haki ya kupata cheti cha kuzaliwa, awe Mtanzania, Mkenya, Msomali nk,

Mgodo visa ,
 
Nenda ujerumani uone kama utapata hicho cheti. Hata kama umezaliwa humo lkn hujafuata masharti yao wanayoyahitaji , utaishia patupu. Tunazichezea sana nyaraka za taifa.
 
Mleta UZI pamoja na Archduke wote nawaunga MKONO...!!

Wageni/Wakimbizi wote, halali na haramu, kwa pamoja wanasifia MIFUMO yetu MIBOVU jinsi inavyo wawezesha kupata NYARAKA/HATI/VYETI mbalimbali pasipo uhakiki wa KINA. mfano Leseni za Udereva, Kadi ya kupigia Kura, Kitambulisho cha Uraia na Vyeti vingine mbalimbali, mambo/taratibu za upatikanaji wa vitu hivi ziko HOLELA kwelikweli....!

Ni BORA Mifumo ikabadirishwa ama kuunganishwa na idara ya UHAMIAJI (kama alivyopendekeza mchangiaji hapo juu)

Kidogo inaweza kuleta UFANISI...

Sent using Jamii Forums mobile app
Uhamiaji ndipo kuna Shida wamegawa passport za Tanzania kwa wageni wanaijeria waghana na Nchi za huko Africa magharibi matokeo yake wengi wakikamatwa na Unga china jina la Tanzania linachafuka zaidi matokeo yake watanzania hawaaminiki popote Duniani kumbe passport zao zinatumiwa na wageni
 
Nenda ujerumani uone kama utapata hicho cheti. Hata kama umezaliwa humo lkn hujafuata masharti yao wanayoyahitaji , utaishia patupu. Tunazichezea sana nyaraka za taifa.

Hakuna nchi yoyote inayomnyima mtu aliyezaliwa kwenye nchi hiyo cheti cha kuzaliwa, cheti cha kuzaliwa na kifo ni haki ya kila mtu anayeishi kwenye nchi yoyote,
Fomu zote za kuomba visa duniani haya maswali mawili lazima yawepo, Nchi uliyozaliwa na Uraia wako, na swali hilo lipo kwa sababu kuzaliwa kwenye nchi fulani nà uraia ni vitu viwili tofauti
 
Pia kinakuruhusu kufaidika na kila service ya serikali ikiwemo kushika nyadhifa yoyote ile...


Mkuu hapa naona umeingia chaka, kuna service gani tunazonufaika nazo, zaidi ya ile ya kula, kulala bure na kichapo juu! labda kwa miaka ila ya zamani, sidhani kwa sasa kama zipo
 
Kaka kuna kitu unakosea, Cheti cha Kuzaliwa sio hati ya uraia, yoyote anayezaliwa Tanzania ana haki ya kupata cheti cha kuzaliwa, awe Mtanzania, Mkenya, Msomali nk,

Mgodo visa ,
====
Rudia kusoma utaelewa cheti cha kuzaliwa kinalink vipi na nyaraka zingine...
 
Back
Top Bottom