Ushauri please!!

Hance Mbuya

Member
Joined
Apr 11, 2012
Posts
45
Reaction score
12
Ilikuwa tar 24/01/2012 ndipo nilipoanzisha uhusiano wa kimapenzi na kadadaa(sio jina halisi)ana 23yrs.Kilichonifanya nianzishe uhusiano nae ni muonekano wake jinsi alivyo,usafi,pia tabia.Kadadaa alikuwa ni mkimya sana si mtu wa story kama walivyo wanawake wengine hii ilinipa shida sana kujua kama ananipenda au napoteza muda wangu kumfuatilia,ilichukua kama miezi miwili baadae akaja kunikubalia,sikuamini moyoni kama ni kweli au anatania lakini mwisho wa siku ilikuwa kweli.Mara kwa mara huwa anapenda kukaa peke yake peke yake.Sikumfahamu kiundani mwanzo ila kadri muda ulivyozidi niliweza kugundua kitu.Kadadaa na vyote alivyokuwa navyo vizuri lakini anashindwa kutoa ushauri,kuamua jambo peke yake,Wakati mwingine anaweza akawa anaangalia muvi.Badae ukampigia na kumuuliza vip ile muvi uliipenda,anakujibu yah niliipenda sana tena sana ilikuwa nzuri we acha tu,Kazi inakuja pale utakapomwambia aielezee kidogo jinsi ilivyokuwa au sehemu aliyoipenda,hapa anaweza kukata simu au akakaa kimya mpaka ubadili story.Nafahamu kila binadamu ana mapungufu yake,lakini mapungufu aliyo nayo sijui ni yanaitwaje.Kabla nilijua anafanya kusudi kumbe ndivyo alivyo.Hapa vip elimu inaweza ikachangia au maisha aliyoishi hapo awali?Naombeni ushauri kwani love inashuka siku hadi siku kama ni asilimia zimebaki 10% tu.
 
Mimi wanawake wakimya huwa siwapendi, tafuta muongeaji ili muongee mambo yanayo wahusu.


Huyo mkimya wawachie mabubu na viziwi, we unataka kupenda wale ambao wameletwa spesho kwa ajili ya mabubu na viziwi...Dhambi mshikaji.
 
Washauri mbona kazi mnayo!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kama hamfanani tabia itakua tabu bora muachie mwenyewe apumzishe nafsi yake.
 
Hayo si maumbile ya mtu tu,sasa cha kushauri nini hapo jamani
 
Kama unampenda kweli utamsaidia lakini kama una mpango wa kumchezea we chapa lapa. Inawezekana huyo binti maisha ya nyuma alipitia maisha magumu sana inawezekana wazaz au walezi wake walikuwa wakali sana kwahiyo akajikuta anaishi maisha ya kutojiamini,embu jitahid kujua background yake,ukikuta kuna tatizo anza kumchangamsha na kumsaidia kukutana na watu mbalimbali ukimjengea tabia ya kujiamini,pendelea kuzungumzia zile stori anazopenda unamshirikisha kwa upendo,unampa macare ya kufa mtu penda kujua kila wakat anafanya nini,viutan vizur vya kimapenz huku ukimthamini mbona ataanza kufunguka mwenyewe halafu atakuja kuwa talkative kuliko ww,pia inawezekana ikawa shule lakini nayo si kigezo tumia ndondoo hizo hizo hapo juu,zaid msaidie kumjengea tabia ya kujiamini kwmb mawazo yake ni mazur na unayathamin hata kama kaongea kisicho ww unapotezea unamrekebisha kiaina kwa upendo.
 

Ebana shukran kwa advise ulioutoa big up.Ni hivi nampenda sana natamani awe mke wangu.Ana kila sifa ya kuwa mke bora.Ila tatizo ndo hilo.Shukran kwa ushauri nitaufanyia kazi.
 
kwani hajasoma kabisa au? infact wanawake wenye hawaongei wanaboa saana,
pia kama mnatofautiana sana kielimu anaweza akajiona mawazo yake infirior fulani hivi
ni psychologia tu ila mambo flani kwa 6/6 nini freshi,,
\ukiona wasi sasa fanya maamuzi ya mwaka
gud luck
 
Ebana shukran kwa advise ulioutoa big up.Ni hivi nampenda sana natamani awe mke wangu.Ana kila sifa ya kuwa mke bora.Ila tatizo ndo hilo.Shukran kwa ushauri nitaufanyia kazi.
Tuko pamoja nilishakumbana nalo hilo kwa ndugu yangu na baada ya kufanya hivyo yaan mkewe amekuwa the best woman,pia jitahidi usiwe mkali sana na mwenye hasira kupitiliza,mfanye kuwa rafiki zaidi nakwambia atafunguka na ataueleza yanayomsifu,make her to feel like woman. Jembe hilo baba siku hizi kupata mwanamke mwenye sifa za mke ni adimu sana.
 
sasa wewe unataka kusimuliwa hadi movie si uangalie mwenyewe , ushajua binti ni mkimya hujiulizi labda maswali yako yanam-bore? au labda interest zenu tofauti ndo maana mnashindwa kupiga stori?
 

Kuhusu elimu ni ya primary strd 7 me 4m4,pia hatujatofautiana kivile kielimu ambayo labda ingesababisha hayo.Pamoja!
 
sasa wewe unataka kusimuliwa hadi movie si uangalie mwenyewe , ushajua binti ni mkimya hujiulizi labda maswali yako yanam-bore? au labda interest zenu tofauti ndo maana mnashindwa kupiga stori?

Hapana sio kwamba nataka anihadithie muvi alioangalia,ila hii nimeitoa kama mfano tu.Kwani unaweza kumpa hata kitu kidogo akushauri na akawa hana cha kukuambia.Sasa kama humjui unaweza sema anafanya kusudi/dharau lakini sivyo...
 
wife material huyo komaa mpaka umfunge paka kengele.
 
wengine wanapenda micharuko wengine wanapenda mabubu, ukisema wa nini achana nae subiri watakaosema watampata lini.
 
Bado sijajua nini kinatakiwa tutoe ushauri maana kazi ya kuelezea muvi mi najua anaifanya Lufufu au nawewe unamoango wakuanzisha kampuni yako kama Lufufu?
 

Huyo dada atakuwa very smart na mwangalifu sana .Hana haraka na relationship na she is happy to be left a lone .Extremely independent na anakujibu kiajabu to stop treating her like a kid .Respect her privacy ( wanaume wakibongo hamjui kurespect privacy ya mtu)unamwuliza maswali ya movie kwani wewe ni interrogator?.Love a person for who they are .Unakumbuka movie coming to America .People tend to test mtu .I used to be like her ( nilikuwa naringa dharau na ole wako uniulize vijiswali vya lijinga you are out ,some men are psychopath and needy women need to watch and be very careful especially african men ) wewe mtu hujamuoa ni girlfriend tu unamuuliza maswali kama mzazi .Wewe kaka ni stalker and very controlling .Wewe ndio tatizo sio huyo dada .stop being soo creepy and stop stalking her
 
wife material huyo komaa mpaka umfunge paka kengele.

I agree with you .wanaume wanataka wanawake waliutulia bila umbea na vurugu Za hapa na pale .sasa huyu kaka anataka drama queen kelele kutwa du kweli wanaume wakiafrica kazi mnayo.sasa hapo unataka mwanamke kutwaaa kujuchubua ngomani asubuhi mpaka jioni .
 
sasa wewe unataka kusimuliwa hadi movie si uangalie mwenyewe , ushajua binti ni mkimya hujiulizi labda maswali yako yanam-bore? au labda interest zenu tofauti ndo maana mnashindwa kupiga stori?

Trust me huyu kaka ni problem .Nina aunt yangu uwii mume wake alikuwa anaongea mpaka tunajiuliza aunt Anaishi Vipi na huyu .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…