Hance Mbuya
Member
- Apr 11, 2012
- 45
- 12
Ilikuwa tar 24/01/2012 ndipo nilipoanzisha uhusiano wa kimapenzi na kadadaa(sio jina halisi)ana 23yrs.Kilichonifanya nianzishe uhusiano nae ni muonekano wake jinsi alivyo,usafi,pia tabia.Kadadaa alikuwa ni mkimya sana si mtu wa story kama walivyo wanawake wengine hii ilinipa shida sana kujua kama ananipenda au napoteza muda wangu kumfuatilia,ilichukua kama miezi miwili baadae akaja kunikubalia,sikuamini moyoni kama ni kweli au anatania lakini mwisho wa siku ilikuwa kweli.Mara kwa mara huwa anapenda kukaa peke yake peke yake.Sikumfahamu kiundani mwanzo ila kadri muda ulivyozidi niliweza kugundua kitu.Kadadaa na vyote alivyokuwa navyo vizuri lakini anashindwa kutoa ushauri,kuamua jambo peke yake,Wakati mwingine anaweza akawa anaangalia muvi.Badae ukampigia na kumuuliza vip ile muvi uliipenda,anakujibu yah niliipenda sana tena sana ilikuwa nzuri we acha tu,Kazi inakuja pale utakapomwambia aielezee kidogo jinsi ilivyokuwa au sehemu aliyoipenda,hapa anaweza kukata simu au akakaa kimya mpaka ubadili story.Nafahamu kila binadamu ana mapungufu yake,lakini mapungufu aliyo nayo sijui ni yanaitwaje.Kabla nilijua anafanya kusudi kumbe ndivyo alivyo.Hapa vip elimu inaweza ikachangia au maisha aliyoishi hapo awali?Naombeni ushauri kwani love inashuka siku hadi siku kama ni asilimia zimebaki 10% tu.