Ushauri nimuache au nifanyeje?

Ushauri nimuache au nifanyeje?

Huyu member mwenzetu Avemaria ndiyo muhusika uliyeahidi utamtaja jina?
Ok! Hamna uhusiano wa SCD na kusema uongo.

Vijitu viongo viongo hata kwa mambo madogo madogo huwa havifai kamwe , hutakaa uwe na furaha.
Kuhusu kujiua hiyo haipo.

Avemaria huyu ajui chaka hili la jf siyo mfuasi ata kidogo.
 
Last edited by a moderator:
Jamani mwenzenu niko njia panda,yapata Mwaka sasa niko kwenye mahusiano na mdada fulani jina nitasema badae, jamani nampenda sana nae pia kiukweli ananipenda mno si kidogo, ila sasa amekuwa na tabia fulani ya kusema uongo wa vitu vidogo vidogo mfano amaweza kuwa yuko nyumbani akadanganya yuko kwenye Daladala huku unasikia mazingira yanaonesha siyo kwenye Gari ila yapo matukio mengi anakuwa anadanya ila ukimbana kidogo anakueleza ukweli na kuomba msamaha.

Shida imeanza leo baada ya kuwa amedanganya kaenda mahali afu akawa amerudi Nyumbani nilipompigia Simu kaanza uongo wake mara nipo kwenye Daladala sasa shisa ni kwamba mazingira ya kwao nayaelewa sana, nikaa nambishia baada ya kama dakika tatu za mabishano akaadimit na kukubali yupo home na kumuuliza anafanya hivyo akadai hana jibu.

Kwakweli nilichukia nikaamua kumtolea uvivu nilimpa masharti kadhaa na ili ayalidhi moja ilikuwa aniambie sababu ya kuwa muongo kwa vitu vya kijinga. Baada ya kuona yamekuwa makubwa akaamua kufunguka na sababu zake ni hizi:

1) Kwanza ili mchukua muda ila mwisho kasema kwa huzuni sana kuwa yeye ni mgonjwa( Sickle cell), unamfanya apende kudanganya ili kwasababu watu wa namna hii wanatabia ya kuogopa kutokubaliwa au kutojiamini muda wote.

2) Sababu ya pili kasema huwa ajui anachosema kama kitanikwaza sana, kwahiyo yeye anavyona hakuna tatizo, mimi nachukia.

Sasa waungwana wanajamvi embu nielezeni kuna uhusiano kati ya kuongopa na Sickle cell? Pili hii habari imenichanganya sana, nawaza nimwache maana huu ugonjwa ni mkubwa na si wakiza kimoja na pia nimesoma kwenye mtandao matunzo ya mtu wa sickle cell ni ghali sana! lakini hata muda wake wa kuishi ni akibahatika kuvuka 18 ni limit 50yrs.

Hapa nilipo nimechanganyikiwa sijui ata nifanyeje yeye kwasasa yupo 21, kama kuna mtu uelewa nisaidieni ameniambia hii siri baada yakuwa amelia sana. Na amevunja agano la mama yake alimwambia asije mweleza mtu ambaye ajui hili tatizo naona hofu ya mama yake ni kwamba mwanae atakosa mwanaume wa kumuoa na kanitishia nikimwacha anakunywa sumu. Nimeanza naye mapenzi alikuwa bado ajajua mwanaume nampenda Avemaria nifanyaje.

Hofu yako kubwa ni kwamba huyo bibie atafariki mapema wala sio suala la uongo.Kuhusu suala la ukimuacha atakunywa sumu, na wewe mwambie AKIKUDANGANYA utakunywa sumu.
 
Hofu yako kubwa ni kwamba huyo bibie atafariki mapema wala sio suala la uongo.Kuhusu suala la ukimuacha atakunywa sumu, na wewe mwambie AKIKUDANGANYA utakunywa sumu.

Mwanagu bonge la dailema.
 
Mmmh..niliwahi kufanya kazi na mtu mwenye sickle cell..mweh! Yataka moyo. Alikuwa akiumwa mara kwa mara, hospital kila wiki na akiumwa atalazwa kabisa. Alikuwa mtoto mdogo tu 20yrs. Sijui kale kadada ka kihindi kanaendeleaje siku hizi...!
Hata hivyo sickle cell haina uhusiano na uongo wa mtu..!
 
Mbona mwisho umemtaja Avemaria tena jamani..!!
 
Last edited by a moderator:
Hahahah umenichekesha kweli wewe dah!!!
Kwahiyo ningekuwa ndo mimi jamaa angekuwa kakosea njia? LOL

Hahaha sikua na maana hiyo bibie Avemaria.....maana yangu ilikuwa kuhusu hiyo kudisclose mambo ya chumbani na kuweka ID humu km baadhi ya waliowahi kufanya hivyo humu jamvini.
 
Last edited by a moderator:
Uongo siyo mzuri. Mtu muongo ni wa kumuogopa sana, inaonekana na bado kuna vingi sana anakudanganya. Ana mambo yake tu huyo, siku ukija kumfumania atkuambie alikuwa anakudanganya tu.
 
kwi kwi kwi kwi kwi kwi

Hayo ndo yanaitwa mahaba ntie ngwala ning'oe meno ya barazani

Acha uoga kijana wanawake wako wengi kama vumbi la dhahabu geita

Mwambie unaachana naye halafu sikilizia baada ya wiki na nusu then call her uone kama hujaisikia sauti yake

Anayetaka kujiua hasemi ugali mtamu jamani!



mmmh labda nakushauri ukasikilize ule wimbo wa ambwene mwasongwe kwanza wa upendo then ndio urudi.Mungu anauwezo wakufanya pale ambapo hata sisi hatufikirii kama inawezekana.mwasongwe aliimba yule kijana alimpenda yule dada akiwa kichaa na Mungu alimponya yule dada ili yule kaka asiaibike na upendo wake.sasa unafikir mungu hawez mponya mtu mwenye siko cel?????pale kwenye mapungufu upendo ndio hupimwa.
 
Uongo siyo mzuri. Mtu muongo ni wa kumuogopa sana, inaonekana na bado kuna vingi sana anakudanganya. Ana mambo yake tu huyo, siku ukija kumfumania atkuambie alikuwa anakudanganya tu.

Asante kwa ushauri!
 
Kwanza, .sickle cell haingiiliani na uongo wake. Kuna dada nafanya nae kazi hapa ni good performer at work ana cheo cha umeneja wa kuaminika, Postgraduate na ni mama wa watoto 3 ila siku ikimbana ndo utamwonea huruma ni ICU kwenda mbele. Sasa angekuwa anatumia huo ugonjwa wake kama ni excuse sidhani kama angefika that far...ugonjwa ni mindset yake tu.

Pili, nahisi matatizo yanaweza kuwa kwako, wewe waonyesha kutokumwamini. Maana unapenda kumuuliza uko wapi kila mara, labda anakujua tabia yako na mazingira aliyopo unaweza ukakasika ndio anaishia kukudanganya. Acha kumuuliza uko wapi everyone now and then...labda you're controling freak!

Tatu, mtu mwenye Sickle cell anaweza kuolewa na kuzaa watoto salama, nendeni mkapime genetic zenu. Huyo dada nilioleza hapo juu mumewe sio sickler na ameweza kuwa na family ambayo haina maradhi. Shughuli jitaarishe na kuuguza when needed, na kama unampango wa family kubwa sidhani kama litawezekana kwa hawa watu.

umeongea point sana
 
mmmh labda nakushauri ukasikilize ule wimbo wa ambwene mwasongwe kwanza wa upendo then ndio urudi.Mungu anauwezo wakufanya pale ambapo hata sisi hatufikirii kama inawezekana.mwasongwe aliimba yule kijana alimpenda yule dada akiwa kichaa na Mungu alimponya yule dada ili yule kaka asiaibike na upendo wake.sasa unafikir mungu hawez mponya mtu mwenye siko cel?????pale kwenye mapungufu upendo ndio hupimwa.

Big point...! Hapa sasa imani itatosha make kwa Mungu tiba ya kwanza ni imani ya mwombaji na muombewa kiukweli nimechanganyikiwa sijui nini nifanye mwenzenu..!
 
Mimi nafikiri unatumia vibaya neno "Nakupenda", kama kweli una maanisha basi huo ugonjwa wake wala isingekuwa tatizo.

Wasiwasi wangu ni kwamba huenda hata hilo swala la yeye kuumwa sickle cell kakudanganya.

Kwa kweli niliposoma hiyo story hata mimi nimeshangaa, kati ya magonjwa ambayo mtu hawezi kuyaficha kwa mtu unayeonana naye mara kwa mara ni Sickle Cell...lazima ungejua kuwa ni mgonjwa! Labda kama ana Sickle Cell trait, ambayo mbebaji wa trait si lazima awe na dalili. Sickle Cell kama ugonjwa haisababishi kuogopa..lakini muathirika wa huo ugonjwa kuna uwezekano mkubwa wa kuapata athari za kisaikolojia akawa muoga na kutumia uongo kujilinda. Japo sioni link kati ya uongo wake na ugonjwa huo...Wagonjwa wa Sickle Cell huudhuria clinic maalum kila mwezi, muombe uende naye siku yake ya clinic utaujua ukweli.
 
Love doesnt ask why
maradhi sio tatizo ktk mapenzi ila ww HUMPENDI na ndo mana unawaza kumuacha
 
Bila shaka avemaria mwingine...!
Ningekushauri hapo ulipotaja jina Avemaria ungeweka angalizo kwamba sio huyu wa jamvini.Licha ya kuwa umefafanua kwenye comment ila kuna wataoishia kusoma maada tu na kuconclude kuwa ni mimi au pengine anaweza asipaone hapo ulipokanusha maana si wote husoma kila comment.
 
Ningekushauri hapo ulipotaja jina Avemaria ungeweka angalizo kwamba sio huyu wa jamvini.Licha ya kuwa umefafanua kwenye comment ila kuna wataoishia kusoma maada tu na kuconclude kuwa ni mimi au pengine anaweza asipaone hapo ulipokanusha maana si wote husoma kila comment.

Pole kwa masaibu yanakupata kwasababu ya hii thread nifanya hivyo. kama jamaa kajidai kutimua nitaziba pengo maana avemaria atakuwa yupo baada ya kuondoka jokes but possible usijali
 
Back
Top Bottom