Ushauri: Nimemuacha anatishia kujidhuru

Ushauri: Nimemuacha anatishia kujidhuru

Hakuna mzima kati yenu. Nyote ni matatizo matupu.
 
Hodi wanajamvi,

Kwa zaidi ya miaka nimekua mfuatiliaji wa thread mbalimbali jukwa hili na nimejifunza mengi kwenu, naamini kwa busara zenu mtanishauri nini cha kufanya katika hili linalonisibu.

Mwanzoni mwa mwaka huu nilikutana na binti mmoja anasoma chuo uuguzi, nilimpenda na tukaanzisha mahusiano, mimi na huyu mpenzi wangu tulikua tunaishi wilaya moja ila maeneo tofauti hivyo tulikua tunaona wikendi moja kila wiki mbili.Nilimjali na kumthamini kwa kila hali na tukawa na mipango ya kutambulishana nyumbani mara tu atakapohitimu masomo yake.

Ilipofika mwezi wa tano nikaanza kuona mabadiliko, tunapokua naye wikend usiku anapigiwa simu ambazo sizielewi nikimuuliza anasema ni kaka yake. Ilipofika mwezi wa sita nikapata safari ya kikazi kwenda mkoa mwingine kwa kipindi cha miezi miwili, mpenzi wangu alikuja kuniaga nilimuomba simu yake nicheze game nikainstall spy application kwenye simu yake nikaenda zangu safari, kuanzia siku hiyo nikawa napata taarifa za mawasiliano yake.

Kupitia hiyo application niliweza kugundua ana mahusiano na watu wawili mmoja akiwa ni ndugu yake, nilijizuia kumuuliza chochote kwa kipindi cha mwezi mzima ili nikusanye ushahidi vizuri.

Juzi uzalendo ukanishinda nikamuuliza kakataa, nikamtumia baadhi ya sms walizokua wanachat akagoma sio zake, eti rafiki yake alikuwa anatumia simu yake. Nikawabana wote wawili rafiki yake kakubali kua sms sio zake (sms ni za mpenzi wangu), basi nikaamua kuachana nae.

Tatizo ni kuanzia jana ananisumbua turudiane nimegoma anatuma sms za kutishia kujidhuru nifanyejee?

1. Niendelee kukaa kimya nisijibu sms wala simu yake.

2. Nikatoe taarifa polisi.

3. .......

NB: Nimeshaamua SITARUDIANA NAE.
Wewe kijana mbaya sana, why spying on your fellow to that extent in the first place ?
Huoni kwamba kwa kufanya ulichokifanya unahitaji kuhukumiwa?
 
acheni kutuchunguza jamani khaaa
ngoja niache kutumia smartphone maana tunachunguzwa mno
khaaa
 
he better take precaution,..Kitu gani kimekuaminisha na kuku''guarantee'' hawezi jiua?..Mbona kuna kesi nyingi tu za watu kutishia kujiua,na wakajimaliza kweli.?..Ni bora huyu mtu achukue all neccessary measures.Asijekuwa namba one suspect baada ya suicide kutokea.Hivi vitu vina usumbufu wake sana polisi.
ni kweli basi namshauri aende polisi aseme ukwelli ili ikitokea la kutokea asihusishwe na lolote lile mkuu niaminivyo n kuwa mwenye kufanya ubaya hua hatamki wazi wazi
 
Pole sana kaka. Mpe nafwasi ya kutafuta replacement. Alikufanya atm yake sasa unagoma kwa kupoteza password. Usikate haraka supply kihivyo. Atakula nini tena ka ndo umeamua kumkaushia?
Mpe notice kuwa mwisho ni mwezi wa 10 angalao arekebishe mpango kwa hao mafala waliobaki.
 
Hodi wanajamvi,

Kwa zaidi ya miaka nimekua mfuatiliaji wa thread mbalimbali jukwa hili na nimejifunza mengi kwenu, naamini kwa busara zenu mtanishauri nini cha kufanya katika hili linalonisibu.

Mwanzoni mwa mwaka huu nilikutana na binti mmoja anasoma chuo uuguzi, nilimpenda na tukaanzisha mahusiano, mimi na huyu mpenzi wangu tulikua tunaishi wilaya moja ila maeneo tofauti hivyo tulikua tunaona wikendi moja kila wiki mbili.Nilimjali na kumthamini kwa kila hali na tukawa na mipango ya kutambulishana nyumbani mara tu atakapohitimu masomo yake.

Ilipofika mwezi wa tano nikaanza kuona mabadiliko, tunapokua naye wikend usiku anapigiwa simu ambazo sizielewi nikimuuliza anasema ni kaka yake. Ilipofika mwezi wa sita nikapata safari ya kikazi kwenda mkoa mwingine kwa kipindi cha miezi miwili, mpenzi wangu alikuja kuniaga nilimuomba simu yake nicheze game nikainstall spy application kwenye simu yake nikaenda zangu safari, kuanzia siku hiyo nikawa napata taarifa za mawasiliano yake.

Kupitia hiyo application niliweza kugundua ana mahusiano na watu wawili mmoja akiwa ni ndugu yake, nilijizuia kumuuliza chochote kwa kipindi cha mwezi mzima ili nikusanye ushahidi vizuri.

Juzi uzalendo ukanishinda nikamuuliza kakataa, nikamtumia baadhi ya sms walizokua wanachat akagoma sio zake, eti rafiki yake alikuwa anatumia simu yake. Nikawabana wote wawili rafiki yake kakubali kua sms sio zake (sms ni za mpenzi wangu), basi nikaamua kuachana nae.

Tatizo ni kuanzia jana ananisumbua turudiane nimegoma anatuma sms za kutishia kujidhuru nifanyejee?

1. Niendelee kukaa kimya nisijibu sms wala simu yake.

2. Nikatoe taarifa polisi.

3. .......

NB: Nimeshaamua SITARUDIANA NAE.
Anyetaka kujidhuru hatoi taarifa, ni utekelezaji tu, sasa naona anakuchimba mkwara,pili vipi unampenda bado? Kama humpendi muache kistaarabu haina haja ya vijembe au kumtishia unamuacha, tatu hebu nitumie jina ya hiyo application uliyokuwa unamchunguzia kwenye simu yake..
 
Mwambie apitie nyumbani kwako achukue dawa umemnunulia ambazo atakufa haraka. .
 
Anakujaribu anaetaka kufa Wala hasemi ajiua tu hema usende polisi Wala wapi endelea Na Maisha yako tena kua kimya akipiga usipokeee akituma SMS usijibu kingine usirudie kumchunguza bata hutamla.

Asante kwa ushauri wako
 
ukiona hivyo ujue huko alikokuwa kakosa mapenz km uliyompa ndio maana kakung'ang'ania.
Watu huwa hawaelewagi, wanaona ni jambo la kawaida tu ktk maisha kuchepuka.
Kiukweli usaliti wa mapenz ni mbaya sana, haijalishi umemfanyia vitu vingap vizuri ila likija suala la usaliti upendo hupungua na imani hutoweka kbsa.
Ni sawa unakula chakula kizuri na kitamu halaf ktk chakula hicho ukakumbana na kinyesi cha binadamu kibichi. Je, utaendelea kula chakula hicho?
Tena kwa sisi wanaume huwa ni vigumu sana kusamehe pind tukigundua umenisaliti.
Mkuu huyo achana naye, mpotezeee kbs

Nimekusoma Mkuu
 
Anyetaka kujidhuru hatoi taarifa, ni utekelezaji tu, sasa naona anakuchimba mkwara,pili vipi unampenda bado? Kama humpendi muache kistaarabu haina haja ya vijembe au kumtishia unamuacha, tatu hebu nitumie jina ya hiyo application uliyokuwa unamchunguzia kwenye simu yake..

Moja, Nashukuru kwa ushauri. Mbili, nimeshamtoa moyoni na nimemuacha kwa amani tu ila yeye ndo anatishia kujidhuru. Tatu nitakujibu PM
 
acheni kutuchunguza jamani khaaa
ngoja niache kutumia smartphone maana tunachunguzwa mno
khaaa

Ukiwa na njia za panya lazima uogope kweli, ila kama muaminifu huna sababu ya kuogopa
 
Pole sana kaka. Mpe nafwasi ya kutafuta replacement. Alikufanya atm yake sasa unagoma kwa kupoteza password. Usikate haraka supply kihivyo. Atakula nini tena ka ndo umeamua kumkaushia?
Mpe notice kuwa mwisho ni mwezi wa 10 angalao arekebishe mpango kwa hao mafala waliobaki.

ha ha ha ha
mkuu umenifanya nicheke hadi majirani wananishangaa
 
Msamehe kwani imeandikwa tusameheane saba mara sabini.
 
Weeeeeee maneno tu na hawez thubutu watu wa vitendo huwa hawatangazi bali ww utaxkia kwa watu kuwa kafanya kitu fulani ,lala mbele
 
Back
Top Bottom