Ushauri: Nahisi nina matatizo ya kupenda sana

Ushauri: Nahisi nina matatizo ya kupenda sana

nyaggad

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
1,160
Reaction score
694
Habari wana jamii forums

Wandugu sio siri nahisi na matatizo ya kisaikolojia naombeni ushauri wenu,mimi huwa nikimpenda msichana mpaka huwa nahisi kuchanganyikiwa maana huwa napenda sana kupita mfano,sasa hivi kuna binti mmoja ndo nipo nae kwenye relation yani nampenda mpaka watu wananishangaa.

Nikiwa natembea mda wote yupo kichwani mwangu,nikiwa nafanya kazi mda mwingi yupo kwenye akili zangu,nikiona kitu kizuri kinauzwa kinachomfaa lazima nimnunulie,pesa huwa namtumia mara kwa mara bila yeye kuniomba,nampigia simu kwa siku kama si chini ya mara kumi,nikilala usiku mara nyingi huwa namuota.

Mwenzenu nimechizika kwa penzi la huyu dada,yani tunapokutana wawili huwa najihisi nimekaa na kiumbe kizuri ajabu mapigo yangu ya moyo huenda kwa kasi ajabu utafikiri nilikuwa nakimbizwa na mnyama mkali,nimemuomba mautamu ameniambia atanipa mpaka tufunge ndoa,hapa nilipo nafanya mahesabu nimuoe mapema kabla hajabadilisha nia.Hivi jamani huu ni upendo wa kawaida au na matatizo ya kisaikolojia.


Napenda kuwasilisha
 
Mkuu, unashauriwa kupenda ila sio kupita kiasi hiki, ni sawa na kucheka tunacheka kwa afya zetu kwa sababu ni dawa ila ukicheka bila sababu unahitaji dawa,, usipende kumuonesha mpenzio unampenda mno atakufanya anavyotaka utajikuta muda mwingi umeupoteza kwa mtu mmoja mpende ila sio sana kiasi hiki jamani.
 
kwa mtizamo wangu
1) wewe ni domo zege ndio maana unajiuliza akikuacha huyo uliye naye utampata wapi mwingine kwa kutumia style gani

2)Pochi yako ina matatizo

3) reception kama yangu
 
Tofautisha kupenda na wivu, pia tofautisha kupenda na mhemko. Unajua maana ya kupenda?, kama ndivyo hebu eleza maana twaweza kusema unapenda kumbe ni homontu zimekujaa
 
Huyo atakuwa mwanamke wako wa kwanza na nadhani haujawahi kugegeda...
 
Watu wasiojua kupenda utawajua tu kutokana na michango yao
 
Hivi ni nani alikuwa anafanya utafiti wa LIMBWATA humu??
 
Wasikudanganye ni kupenda, huo ni mhemko mkuu.

Jitathimini ni usikurupuke kuoa kisa kakwambia atakupa papuchi ukimuoa. Nyie ndo mbaochepuka mkishaoa.

Slow down
 
Back
Top Bottom