Ushauri: Mke wangu toka aende kujifungua kwao, sasa mtoto ana mwaka na nusu hajarudi

abdukarim

JF-Expert Member
Mar 29, 2017
476
591
Nimeoa 2015 kwa ndoa halali kabisa kwa mapenzi ya Mungu mke akapata mimba, tukakaa baada ya miezi saba mke akasema hawezi jifungulia hapa nilipo ni lazima ajfungulie nyumbani kwao.

Mimi nikasema sawa kulingana na Mila zetu hutaenda nyumbani kwenu bali utaenda kwetu akasema sawa. Nikatafuta nauli akaenda nyumbani kwa sababu nyumbani ni mbali alisafiru peke yake kwa sababu nauli mtu mmoja Kama 85 elfu nauli peke yake.

Baada ya kufika nyumbani wazazu wangu wakampokea na kufurahi.
Baada ya wiki moja akamwambia baba yangu anataka kwenda kwao, baba akamwambia kwani mlipangaje na mume wako wakati wazazi niliwapa taarifa ya kuja huko kujifungua wakashukuru na kufurahi.

Baba akamwambia ngoja niongee na mumeo nisikie anasemaje yeye akamjibu baba mkwe kuwa sikuombi nauli bali ni taarifa nakupa. Baada ya siku moja akabeba mizigo yake akaondoka mama yangu akamzuia ili asubiri maelekezo yangu akakataa.

Baada ya miezi miwili akajifungua huko kwao taarifa nilipewa na wazazi wangu kwani wao walipata kwa mshenga. Yeye toka alivyoenda kwao simi yangu alikuwa hapokei. Baada ya kujifungua mama yangu akaenda huko kumuona na mambo yote yanayomhusu mzazi na mimi nikatuma pesa kupitia mama mkwe kwan ndio tulikuwa tunaongea kwenye simu.

Baada ya miezi miwili nikampigia simu mama mkwe kwa kumuomba nimtumie nauli arudi kwangu kwan kwa wakati huo nilikuwa bize na masomo nisingeweza kwenda huko. Mama mkwe hakutoa jibu na mke wangu jibu alilotoa alisema huko siwezi kurudi, sababu hakuniambia nikasema acha nimuongezee muda labda atabadilika.

Kibaya zaidi akakataa kumleta mwanangu kwa bibi yake na babu yake kitu ambacho wazazi wangu wamechukia kwa sababu nauli kutoka kwao mpaka kwa wazazi wangu ni sh 2000 tu. Wazazi wake wakakata mawasiliano na wazazi wangu.

Mimi nikiwapigia simu kuhusu kurudi kwa mke wangu wanasema hawajui atarudi lini, na kibaya zaidi alibadili laini ambayo mimi siijui ili nisimsumbue.

Mpaka sasa mtoto ana mwaka mmoja na nusu hajui kwao, ninapopata hela ya matumizi natuma kwa mama mkwe kwani toka mama mkwe aseme kunitumia no mpya hiyo mwaka unaenda.

Nilimuoa kwa ndoa halali na kumthamni kwani wazazi wake walitaka mahari nyingi kama milioni na nusu na wazazi wangu wakatoa na harusi kubwa ikachezwa.

Ushauri ninaomba je huyo mwanamke niachane nae nitafute mwingine au nifanyeje maana umri unasogea now nina 32years na wazazi wangu wanaonyesha moyo wakutokutaka nirudiane nae kwani wanasema wamedharauliwa na wazee wenzao.

Ushauri please, nifanyeje nakosa maamuzi.

Sent from my TECNO W5 Lite using JamiiForums mobile app
 
sihitaji kuumiza kichwa kaka,

hapa dhahiri ulifosi ndoa kwa kutumia mkwanja,

ulishawishi ndoa hatimaye binti alikubali kishingo upande,

alikubali kuolewa huenda alishatendwa so akaamua HASIRA ZA MKIZI,

ILA NA WEWE MBONA HUJAENDA KUMUONA CHALII YETU TOKA AZALIWE?

Utasingizia kazi inabana, lakini ipo likizo fupi kwa baba aliyepata mtoto,



Sent from my TECNO-W5 using JamiiForums mobile app
 
Hizi Mambo hazihitaji uhsauri wowtoe kwa Dharau aliyoifanya kwa Wazazi wako ni Sababu Tosha yakutoendelea kumhifadhi kwenye Uko wenu . Pia huyo Mtoto aliyezaliwa siyo Mtoto wako japo unaendelea kujipendekeza kuwasiliana na huyo Unayemuita Mama Mkwe. Kifupi Ndoa ipo Moyoni na siyo Kanisani au Kwenye Vyeti.. Yeye alichokifanya aliondoa Gundu ya Kuolewa ila alikuwa hahitaji Ndoa. Au wewe ulilazimisha ndoa ila yeye hakuwa anakuhitaji wewe.

Kikubwa ameepukana na Aibu kubwa tu ambaye ingekuandama siku za usoni.
 
Itabidi tuanzishe jukwaa la watu wazima maana kama mtu hana ndoa ni vigumu kumshauri mwenye ndoa.
Mada imeeleweka, vijana wengi huwa tunapotea kwa kutofata ushauri wa wazee wetu, fuata maelekezo ya wazee naamini ni vizuri na ndio utatuzi wa tatizo lako, kwani huwezi jua yeye kwenda kwao kuna kitu gani amejaribu kukuepusha au kukificha ili usijue. Fuata maelekezo ya wazee wako, umri unasonga ndugu.

sent from my Samsung smart tv using JamiiForums
 
Kwa sababu tumeskia upande mmoja ni ngumu sana kushauri mkuu maana ni ngumu sana kutokea kama ulivyoandika na kama ni kweli basi huna hata haja kuomba ushauri maana kila kitu kiko wazi. Yaani mke aamue tu kujiamulia kuondoka ukweni kwao? Kisha aamue tu kubadili line bila mume kujua? Alafu aamue tu kujibu sirudi? Na aamue tu kutompeleka mtoto kwa babu/bibi zake wengine wakati nauli sh 2000/=? Amini nakuambia kuna kitu hapa nyuma ya pazia! Eiza unakijua au hukijui.

Pole sana kwa maswahibu mkuu.
 
Hapo lazima kuna kitu tu nyuma ya panzia either unakijua au umekificha makususudically!

Yaani mtu aondoke tu hivi hivi bila sababu yoyote hile wala haiingii akilini...

Sent from my GT-N8000 using JamiiForums mobile app
Hakuna kitu kingne, tofauti na hapo hata kabla hajaondoka kwa wazaz walimuuliza kunashida na mmeo akakataa katakata ndoo maana wazaz wanakasrka, kama kulikua na tatzo kwa nn asiseme?

Sent from my TECNO W5 Lite using JamiiForums mobile app
 
Nilimpenda mwenyewe tukapendana hakuna kingne mkuu

Sent from my TECNO W5 Lite using JamiiForums mobile app
Inawezekana kuwa una power juu yake na am echo ka ku submit kwako, either familia yenu iana uwezo zaidi na umemzidi madarasa.

Angekula na j shughuli kinachomwingizia pesa huko uliko angerudi sasa kurudisha kuwahi kuosha masufuria hata yeye amechoka.
 
Hakuna kitu kingne, tofauti na hapo hata kabla hajaondoka kwa wazaz walimuuliza kunashida na mmeo akakataa katakata ndoo maana wazaz wanakasrka, kama kulikua na tatzo kwa nn asiseme?

Sent from my TECNO W5 Lite using JamiiForums mobile app
Basi kama ni hivo hakuna upendo hapo, je alikubali kuolewa kwa hiyari yake au kuna kitu kilimfosi?

Au kakimbia una dushe kubwa(mkunyenge) mkuu...

Sent from my GT-N8000 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom