Azoge Ze Blind Baga
JF-Expert Member
- Mar 8, 2019
- 366
- 1,375
Salaam wanajamvi
Nina Mke na watoto wawili na mmoja ni kijacho
Nimekuwa kwenye mahusiano na mwanamke huyu kwa miaka 9 na mwaka Jana tukafunga ndoa ya bomani maana kila mmoja Ana imani yake na hakuna Kati yetu alietaka kubadili na kimfuata mwenzake.
Miaka ya nyuma mapenzi yalikuwa safi Mawasiliano yalikuwa imara Sana,yeye na Mimi tunaishi mikoa jirani Kama Km 220 hivi
Yeye ni muajiriwa na Mimi ni muajiriwa sekta binafsi ambayo salary yake ni ndogo so Mke kanizidi parefu Sana.
Sasa tangu mwaka Jana mwezi wa 6 Mawasiliano Kati yetu yamekuwa finyu mnoo na tuna migogoro ya mara kwa mara na chanzo Cha migogoro hii ni kunituhumu Mimi nachepuka baada ya kupata story toka kwa majirani.
Nimejaribu kuzungumza nae Sana ,mwenzangu haelewi na sasa ndo kaacha kabisa Mawasiliano na Mimi.
Nisipopiga Mimi hata siku 5 ndio imetoka hiyo,mwanamke hajui kupiga simu hajui kutuma msg,inshort Mawasiliano ya maana Kati yake na yangu hamna.
Ninajitahidi kupiga simu mara kadhaa ili niwajulie hali watoto ila nahisi kukata tamaa.
Mwenzangu anaonekana bado Ana kinyongo na Mimi ,lakini pia hali hii ya Mawasiliano kuwa finyu aliianzisha miaka kadhaa nyuma ila kwa sasa hali imekuwa mbaya Sana.
Ushauri wenu tafadhali jinsi ya kumdhibiti huyu mwanamke ili atambue umuhimu wa Mawasiliano hasa kwa wapenzi ambao wanaishi mbalimbali.
Nimechoka kila wakati nianze kumtafuta Mimi.
Nina Mke na watoto wawili na mmoja ni kijacho
Nimekuwa kwenye mahusiano na mwanamke huyu kwa miaka 9 na mwaka Jana tukafunga ndoa ya bomani maana kila mmoja Ana imani yake na hakuna Kati yetu alietaka kubadili na kimfuata mwenzake.
Miaka ya nyuma mapenzi yalikuwa safi Mawasiliano yalikuwa imara Sana,yeye na Mimi tunaishi mikoa jirani Kama Km 220 hivi
Yeye ni muajiriwa na Mimi ni muajiriwa sekta binafsi ambayo salary yake ni ndogo so Mke kanizidi parefu Sana.
Sasa tangu mwaka Jana mwezi wa 6 Mawasiliano Kati yetu yamekuwa finyu mnoo na tuna migogoro ya mara kwa mara na chanzo Cha migogoro hii ni kunituhumu Mimi nachepuka baada ya kupata story toka kwa majirani.
Nimejaribu kuzungumza nae Sana ,mwenzangu haelewi na sasa ndo kaacha kabisa Mawasiliano na Mimi.
Nisipopiga Mimi hata siku 5 ndio imetoka hiyo,mwanamke hajui kupiga simu hajui kutuma msg,inshort Mawasiliano ya maana Kati yake na yangu hamna.
Ninajitahidi kupiga simu mara kadhaa ili niwajulie hali watoto ila nahisi kukata tamaa.
Mwenzangu anaonekana bado Ana kinyongo na Mimi ,lakini pia hali hii ya Mawasiliano kuwa finyu aliianzisha miaka kadhaa nyuma ila kwa sasa hali imekuwa mbaya Sana.
Ushauri wenu tafadhali jinsi ya kumdhibiti huyu mwanamke ili atambue umuhimu wa Mawasiliano hasa kwa wapenzi ambao wanaishi mbalimbali.
Nimechoka kila wakati nianze kumtafuta Mimi.