Kijana leo
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 2,860
- 812
Unasubiri jibu gani wakati umeshamuona anafanya kazi baa?
Mfungulieni restaurant awe anauza maana inaonekana hiyo kazi yenyewe anaiweza.
Usije ukafikiri kazi ya baa siyo kazi. Akiisimamia vizuri inalipa zaidi hata ya ajira za kuajiliwa just mfanyieni fair tu maisha yasonge.
jaribuni kumpa elimu ya ujasiriamali then mpeni mtaji afanye biashara
anasema yeye hawezi kusoma, sasa hiyo ELIMU YA UJASILIAMALI ataipataje?
afu weweeeeee!
Nieleweke ni ndugu yangu 'Damu' mtoto wa Baba Mkubwa.
Kamaliza form four mwaka 2010 kafail alipata ziro na 'D' moja tu, 2011 akareseat ndo kavurunda kabisa, 2012 nikamwambia njoo huku nchi jirani nilipo mie akaja akaanza kusoma Diploma ya HR kaharibu mbaya semister ya kwanza kachemsha na vitabia fulani sio vizuri.
Nikamrudisha home nikamwambia chagua usome nini he jibu nililopata nusu nizimie 'Dada mie kusoma siwezi' nikasema wataka nini sasa. Ngoja nifikirie mie haya he kaenda kwa Mdingi wangu ambaye ni Mdogo kwa Baba yake kawashiwa moto hatari kwa ujinga wake na ushauri wa kipumbavu wa marafiki katoroka akaenda kuishi hostel na rafiki anayesoma CBE.
Jana nimekwenda mahali kula kiti ya moto mara namuona kabeba tray anakuja kunihudumia mie mdomo wazi. Namuuliza hii ndo kazi uliyotaka kufanya ama?? Anaanza kulia eti dada nisamehe nimekosa pesa ya kula imebidi nifanye hii kazi nisaidie.
Mwenzenu mate yalinikauka, maneno yalipotea sikujibu hata neno moja kiti ya moto yenyewe ilikuja nikafunga hata apetite yote iliyeyuka.
Naomba ushauri wenu nifanyeje
jaribuni kumpa elimu ya ujasiriamali then mpeni mtaji afanye biashara
jaribuni kumpa elimu ya ujasiriamali then mpeni mtaji afanye biashara
sijajua hapa njiapanda upo wewe au yeye? na njiapanda ya kumsaidia au? kama hajakupa jibu wala usiwaze na huyo tayari akili yake imeeshajichanganya na kukomaa. mshaurini umpeleke akaanze memkwa.