VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Tafadhalini sana someni hapa. Msiishie kuwaandaa makada/makamanda/wanachama wenu kulinda kura. Kila mmoja wenu,kwa nafasi yake, yampasa kufanya kampeni ya kutosha kuhakikisha watanzania wenye sifa stahiki wanajiandikisha kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura. Uchaguzi utanoga kukiwa na wapigakura wa kutosha.Uchaguzi utanoga na mshindi kuheshimiwa,mamilioni ya watanzania yakipiga kura kuchagua viongozi wao hapo Oktoba. Vyama visitegemee 'simple majority' itakiwayo kwenye Katiba ya sasa.
Viongozi na wanachama tuhamasishane na tuhamasishe wengine kujiandikisha. Hakika nawaambia,kujaza watu wasiopiga kura mikutanoni si kipimo sahihi ha demokrasia. Kusomba na kuswaga washangiliaji pia si kipimo sahihi. Watanzania wajae kwenye Daftari la Kudumu laWapigakura na wamiminike vituo vya kupigiakura Oktoba. Hapo,tutaiona demokrasia na kumchagua tutakaye kama Rais,Mbunge na Diwani bila mawaa. La sivyo,kumi tu watatuchagulia viongozi wetu!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Viongozi na wanachama tuhamasishane na tuhamasishe wengine kujiandikisha. Hakika nawaambia,kujaza watu wasiopiga kura mikutanoni si kipimo sahihi ha demokrasia. Kusomba na kuswaga washangiliaji pia si kipimo sahihi. Watanzania wajae kwenye Daftari la Kudumu laWapigakura na wamiminike vituo vya kupigiakura Oktoba. Hapo,tutaiona demokrasia na kumchagua tutakaye kama Rais,Mbunge na Diwani bila mawaa. La sivyo,kumi tu watatuchagulia viongozi wetu!
Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam