Ushauri kwa Serikali zote mbili - Uchimbaji Mafuta

Ushauri kwa Serikali zote mbili - Uchimbaji Mafuta

MrFroasty

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2009
Posts
1,195
Reaction score
596
Najua kuna harakati au mchakato wa kuchimba mafuta. Dunia inaelekea kwenye chanzo cha umeme hususani nchi nyingi zishatoa matamko ya kupiga marufuku magari ya mafuta. Hii ina maana madini haya mafuta hayana future na bei yake itapungua kwa kasi miaka ijayo.

Nchi zilotoa misimamo ya kusimamisha kutengeneza magari ya mafuta (ICE - Internal combusion Engines zinasita production) kuanzia miaka ya 2025 - 2030 ni kama CHINA, Marekani, Canada, EU n.k. Nashauri rasilimali hii isipewe kipaumbele hususan linapokuja suala la uharibifu wa mazingira na kuhatarisha utalii ambao una future zaidi kuliko mafuta miaka ijayo hapo mbeleni.

Wasalaam
 
Hapo unaposema isipewe kipaumbele unamaanisha nini hasa? Iachwe isichimbwe au?
 
Hapo unaposema isipewe kipaumbele unamaanisha nini hasa? Iachwe isichimbwe au?
Kama kuchimba mafuta kutapelekea kuharibu eneo la bahari ambalo linatumika kwa utalii, basi yasichimbwe. Kwasababu bahari na utalii ni muhimu kwa pato la taifa na kizazi kijacho kuliko mafuta.

Nasema hivyo kwasababu najua mikakati ilioko kwa wenzetu ambao ndio wateja wa mafuta washatoa matamko ya kupiga marufuku magari ya mafuta. China ana mkakati wa kufunga viwanda vya magari ya mafuta by 2025 na 25% ya magari yawe tayari yanatumia umeme. Wakati sie ndio kwanza tunataka kuanza.
 
We could be late in the game I am afraid
 
Back
Top Bottom