KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 36,516
- 89,013
Tukianzia awamu iliyopita wamejitahidi kwa kiwango chao ktk swala zima la ujenzi wa shule mbalimbali hapa nchini,hii nikutokana na kwa wkt huo kuwa na uhaba wa shule kwa wkt huo lkn kwa sasa jambo hilo limepungua kwa kiasi chake..
Hivyo ningependelea awamu hii ijikite ktk kuhamasisha utoaji wa elimu bora.. bila hivyo kutakuwa hakuna maana nzima ya majengo yaliyojengwa na yale yote yanayofanyika kuhusu elimu yetu!
tatizo sio kuwa na shule nyingi tu hapana bali kuwa na watu waliokuwa na elimu bora maana hiki ndio msingi mzima wa neno elimu means kuelimika..
hata kama ni kukazia kuwa na shule lkn kwasasa sidhani kama hili linatakiwa kushikwa tena kwa kasi sana ila kinachotakiwa sasa ni kutolewa kwa elimu bora hili ndilo lengo haswa.
nibora kuwa na siraha moja ambayo itakulinda kwa uhakika kuliko kuwa na siraha elfu moja ambazo haziwezi kumdhuru adui! hata sifa ya kuitwa siraha zitakuwa zimepoteza.