Sanyambila
JF-Expert Member
- Jan 24, 2018
- 394
- 523
Habari ya majukumu ya kulijenga taifa wazalendo
Mimi kama mwananchi wa Tanzania, niliyezoea taifa lenye umoja, mshikamano na utulivu
nimepigwa na butwaa kilichotokea nchini kwetu.
Kumekuwa na kauli nyingi na nyingine zenye mkanganyiko wa makusudi tu kutetea ama kujisitiri pasipo kujua nchi hii vijana wamesoma na wana uelewa wa hali ya mambo yalivyo nchini.
Mimi Nampa pole sana Samia kwa haya yaliyotokea katika regime yake na anaonesha ana dhamira ya kurudisha nchi mahali pake Ila NJIA ANAYOOTUMIA NI NDEFU SANA
USHAURI WANGU
Ili kurejesha Amani nchini si kwa polisi pekee bali na diplomasia na NJIA za kisiasa zilipaswa kutumika
1. Rais angelitoka hadharani kutoa pole na kulaani vitendo vilivyo fanywa na askali na makundi ya usalama yaliyofanya mauaji hapa watu wangewajibishwa (kutolewa katika nafasi zao)
a) IGP nje
b) mkuu wa usalama nje
C) mkuu wa Majeshi aliingilia majukumu ua askali naye nje
d) waziri wa mambo ya ndani na waziri wa ulinzi nao pia nje
e) wakuu wa Mikoa na RPCS' ambako watu waliouwawa Dar, mbeya, Songwe, Arusha, Mwanza Tanga, na scheme za majiji wakae pembeni
2. Awasikilize wanaotoa USHAURI sisi ni wananchi wake na wapiga kura wake. Amtoe Tundu Lissu maana hii ni karata nzito itapunguza maadui
na wote walioshikiliwa kisiasa awaachie
3. Siku ya tarehe 29 Oktoba iwe siku ya maombolezo kila mwaka
Na awape pole wana familia waliopotelewa na ndugu siku hiyo ( inahitaji roho ngumu Ila Huna jinsi) ndo siasa
4. KATIBA Mpya ndo tulizo la mwisho la wa Tanzania hakuna namna muda ndo huu KATIBA Mpya na tume huru, hii wameikataa
5. Waite wadau, wawakilishi wa gen z, vyama vya siasa, asasi za kiraia na zisizo, wazee wanao aminika, viongozi wa Dini, kaa nao kwa kikao wa sikilize wao
Kisha ita kamati kuu ya chama CCM waeleweshe mliojadili na wadau
Toa maamuzi sahihi
Ikishindika sasa
Hii ni climax
Mama ajihudhuru ang'atuke hii itakuwa ni bonge LA heshima
Wa Tanzania watakuona kama kiongozi wao milele ndo siasa
Ili kutunza heshima yako mama
Nje na hapo unachelewa na unaongeza chuki Amani itakuwepo Ila tu ni kwasababu ya mtutu au polisi basi
Nimeshangaa bado ukamataji wa polisi ni uleule japo waziri wa mambo ya ndani amekataza ukamataji huo mfano ni MWAMBE . Inamaana polisi wapo juu ya waziri
Mama hawa unaowaita wasaidizi wako wanakutukanisha au kugombanisha na raia wako
Bado ni wababe, kauli zao zina uchochezi, kwa wananchi
Niishie tu kusema
Mstaafu Rais Kikwete alifumba macho wakati wa Richmond alimtoa Swaiba wake U waziri mkuu nchi ikatulia
Mama pole najua sign hili ni Zito Ila mwenyezi Mungu akupe subra na ujasiri pia maamuzi mazito yatakayo fuata
NCHI ITATULIA TU
AHSANTE SAANA
IONWE KWENYE JALADA
Mimi kama mwananchi wa Tanzania, niliyezoea taifa lenye umoja, mshikamano na utulivu
nimepigwa na butwaa kilichotokea nchini kwetu.
Kumekuwa na kauli nyingi na nyingine zenye mkanganyiko wa makusudi tu kutetea ama kujisitiri pasipo kujua nchi hii vijana wamesoma na wana uelewa wa hali ya mambo yalivyo nchini.
Mimi Nampa pole sana Samia kwa haya yaliyotokea katika regime yake na anaonesha ana dhamira ya kurudisha nchi mahali pake Ila NJIA ANAYOOTUMIA NI NDEFU SANA
USHAURI WANGU
Ili kurejesha Amani nchini si kwa polisi pekee bali na diplomasia na NJIA za kisiasa zilipaswa kutumika
1. Rais angelitoka hadharani kutoa pole na kulaani vitendo vilivyo fanywa na askali na makundi ya usalama yaliyofanya mauaji hapa watu wangewajibishwa (kutolewa katika nafasi zao)
a) IGP nje
b) mkuu wa usalama nje
C) mkuu wa Majeshi aliingilia majukumu ua askali naye nje
d) waziri wa mambo ya ndani na waziri wa ulinzi nao pia nje
e) wakuu wa Mikoa na RPCS' ambako watu waliouwawa Dar, mbeya, Songwe, Arusha, Mwanza Tanga, na scheme za majiji wakae pembeni
2. Awasikilize wanaotoa USHAURI sisi ni wananchi wake na wapiga kura wake. Amtoe Tundu Lissu maana hii ni karata nzito itapunguza maadui
na wote walioshikiliwa kisiasa awaachie
3. Siku ya tarehe 29 Oktoba iwe siku ya maombolezo kila mwaka
Na awape pole wana familia waliopotelewa na ndugu siku hiyo ( inahitaji roho ngumu Ila Huna jinsi) ndo siasa
4. KATIBA Mpya ndo tulizo la mwisho la wa Tanzania hakuna namna muda ndo huu KATIBA Mpya na tume huru, hii wameikataa
5. Waite wadau, wawakilishi wa gen z, vyama vya siasa, asasi za kiraia na zisizo, wazee wanao aminika, viongozi wa Dini, kaa nao kwa kikao wa sikilize wao
Kisha ita kamati kuu ya chama CCM waeleweshe mliojadili na wadau
Toa maamuzi sahihi
Ikishindika sasa
Hii ni climax
Mama ajihudhuru ang'atuke hii itakuwa ni bonge LA heshima
Wa Tanzania watakuona kama kiongozi wao milele ndo siasa
Ili kutunza heshima yako mama
Nje na hapo unachelewa na unaongeza chuki Amani itakuwepo Ila tu ni kwasababu ya mtutu au polisi basi
Nimeshangaa bado ukamataji wa polisi ni uleule japo waziri wa mambo ya ndani amekataza ukamataji huo mfano ni MWAMBE . Inamaana polisi wapo juu ya waziri
Mama hawa unaowaita wasaidizi wako wanakutukanisha au kugombanisha na raia wako
Bado ni wababe, kauli zao zina uchochezi, kwa wananchi
Niishie tu kusema
Mstaafu Rais Kikwete alifumba macho wakati wa Richmond alimtoa Swaiba wake U waziri mkuu nchi ikatulia
Mama pole najua sign hili ni Zito Ila mwenyezi Mungu akupe subra na ujasiri pia maamuzi mazito yatakayo fuata
NCHI ITATULIA TU
AHSANTE SAANA
IONWE KWENYE JALADA