Ngamanya Kitangalala
JF-Expert Member
- Sep 24, 2012
- 501
- 1,214
Napenda kuchukua fursa hii kumpongeza kwa dhati ndugu Dr Bashiru Ally Kakurwa kwa kuteuliwa na kuwa katibu mkuu wa chama cha mapinduzi taifa
Kwa uteuzi huu ni dhahiri pasipo shaka mh mwenyekiti taifa, amedhamiria kwa dhati kukifanya chama cha mapinduzi kiweze kujiendesha chenyewe kiuchumi, pasipo kutegemea ruzuku ama michango kutoka kwa wafanyabiashara kama ilivyokuwa siku za nyuma
Binafsi naamini jina la Dr Bashiru Ally kuwa katibu mkuu,lilikuwepo kwenye mawazo ya mwenyekiti taifa kwa muda kidogo, kwani lilikuwa likitajwa mara nyingi kama mrithi sahihi wa Comrade Kinana, hata kuteuliwa kwake kuwa mwenyekiti wa kamati ya kuhakiki mali za CCM ulifanywa kwa makusudi kabisa, ili aweze kupata fursa ya kufahamu ni kwa namna gani mali za chama zimekuwa zikitumika isivyo na kuwanufahisha baadhi ya watu wachache na si chama kama yalivyo makusudi yake
Hivyo basi kwa kuteuliwa kwake kuwa katibu mkuu CCM, itampa fursa nzuri zaidi ya kuhakikisha mali hizo zinarudi mikononi mwa chama na kukinufaisha chama, ni hatua nzuri sana ya kizalendo na ya kupongezwa iliyochukuliwa na mwenyekiti CCM taifa
Lakini binafsi kama ningekuwa kwenye nafasi ya kumshauri mh mwenyekiti au katibu mkuu mpya, ningewashauri hatua hii ya kurudisha mali za CCM, tuanzie hapa tulipo sasa, kwa maana ya kuwaomba wale wote waliojitwalia mali za chama kuzirudisha pasipo kwenda hatua zaidi za kuwataja hadharani ama kuwachukulia hatua za kisheria
Kwa nini nasema hivyo, lazima tukumbuke wale wote wanaodaiwa kuchukua mali za chama wengi ni wale wanaojiona ni CCM asilia( CCM maslahi), kundi hili ni kundi kubwa na lenye watu wengi wenye uzoefu katika siasa za nchi hii, wenye kujua fitna za siasa,
Kundi hili kama litapelekwa kwenye mikono ya sheria, litazidi kujenga chuki kubwa dhidi ya CCM mpya, kwani wengi wao katika kundi hili wanajiona wametengwa na CCM mpya
Kundi hili la CCM maslahi( CCM asilia) si la kupuuza hata kidogo, kwani ni dhahiri kwa kutumia izoefu wao katika siasa za nchi hii, wanaweza kuleta shida sana katika uchaguzi wa ndani wa CCM 2022, kwa vyevyote vile watakuwa wanajipanga kuandaa mgombea wao 2025 kama ilivyo kawaiida yao, pia ni lazima tukumbuke baada ya uchaguzi 2020, kundi hili hawatakuwa na nidhamu ya uoga tena kwa mwenyekiti kama waliyonayo sasa
Kundi hili linahitaji uangalifu wa hali ya juu katika kuwashughulikia
Kwa uteuzi huu ni dhahiri pasipo shaka mh mwenyekiti taifa, amedhamiria kwa dhati kukifanya chama cha mapinduzi kiweze kujiendesha chenyewe kiuchumi, pasipo kutegemea ruzuku ama michango kutoka kwa wafanyabiashara kama ilivyokuwa siku za nyuma
Binafsi naamini jina la Dr Bashiru Ally kuwa katibu mkuu,lilikuwepo kwenye mawazo ya mwenyekiti taifa kwa muda kidogo, kwani lilikuwa likitajwa mara nyingi kama mrithi sahihi wa Comrade Kinana, hata kuteuliwa kwake kuwa mwenyekiti wa kamati ya kuhakiki mali za CCM ulifanywa kwa makusudi kabisa, ili aweze kupata fursa ya kufahamu ni kwa namna gani mali za chama zimekuwa zikitumika isivyo na kuwanufahisha baadhi ya watu wachache na si chama kama yalivyo makusudi yake
Hivyo basi kwa kuteuliwa kwake kuwa katibu mkuu CCM, itampa fursa nzuri zaidi ya kuhakikisha mali hizo zinarudi mikononi mwa chama na kukinufaisha chama, ni hatua nzuri sana ya kizalendo na ya kupongezwa iliyochukuliwa na mwenyekiti CCM taifa
Lakini binafsi kama ningekuwa kwenye nafasi ya kumshauri mh mwenyekiti au katibu mkuu mpya, ningewashauri hatua hii ya kurudisha mali za CCM, tuanzie hapa tulipo sasa, kwa maana ya kuwaomba wale wote waliojitwalia mali za chama kuzirudisha pasipo kwenda hatua zaidi za kuwataja hadharani ama kuwachukulia hatua za kisheria
Kwa nini nasema hivyo, lazima tukumbuke wale wote wanaodaiwa kuchukua mali za chama wengi ni wale wanaojiona ni CCM asilia( CCM maslahi), kundi hili ni kundi kubwa na lenye watu wengi wenye uzoefu katika siasa za nchi hii, wenye kujua fitna za siasa,
Kundi hili kama litapelekwa kwenye mikono ya sheria, litazidi kujenga chuki kubwa dhidi ya CCM mpya, kwani wengi wao katika kundi hili wanajiona wametengwa na CCM mpya
Kundi hili la CCM maslahi( CCM asilia) si la kupuuza hata kidogo, kwani ni dhahiri kwa kutumia izoefu wao katika siasa za nchi hii, wanaweza kuleta shida sana katika uchaguzi wa ndani wa CCM 2022, kwa vyevyote vile watakuwa wanajipanga kuandaa mgombea wao 2025 kama ilivyo kawaiida yao, pia ni lazima tukumbuke baada ya uchaguzi 2020, kundi hili hawatakuwa na nidhamu ya uoga tena kwa mwenyekiti kama waliyonayo sasa
Kundi hili linahitaji uangalifu wa hali ya juu katika kuwashughulikia