Ushauri kwa mabinti ambao hawajaolewa bado

Ushauri kwa mabinti ambao hawajaolewa bado

nashukuru my cousin natamani sana nije huko mkoani kukusalimia ila mume wangu ananikatakaza nisiende kwa ndugu zangu anasema eti utaachana na nduguzo na mama, baba utaambatana na mumeo nanyi mtakuwa mwili mmoja hivyo sipaswi kwenda kwani nilishaachana nanyi naomba umsaidie aelewe maandiko vizuri

huyo shem haache kukubania bwana, kama vipi ngoja nijipange nije mimi cousin wangu
 
asante sana Bujibuji kwa somo hili ila pamenigusa hapa nimeona nicopy na kupaste: 4. Tulia mbele za Mungu Filipi 4:6 Msifadhaike juu ya jambo lo lote; lakini katika kila jambo mjulisheni Mungu haja zenu, kwa kusali na kuomba pamoja na kushukuru Mungu analifahamu hitaji lako na muhimu zaidi anakujua na kukupenda, hajakusahau maana hawezi kukusahau na anakuwazia yaliyo mema. Ebrania 13:5b kwa kuwa yeye mwenyewe amesema, “Sita kupungukia kamwe wala sitakuacha” Yeremia 29:11 Kwa maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu,’’ asema BWANA. “Ni mipango ya kuwafanikisha na wala si ya kuwadhuru,ni mipango ya kuwapa tumaini katika siku zijazo”. Usikate tamaa, mume wako yupo na atakuja kwa wakati wa Bwana.

Dada nimefurahi sana unavojua kuchambua vifungu vya kutia moyo katika safari yetu tuliyonayo, kwa kuongezea tu na mimi natupia hivi hapa
Mithali 16:3 Mkabidhi Bwana kazi zako na mawazo yako yatathibitika
Mithali 3:5-6 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako
Yohana 14:14 Mkiniomba cho chote kwa jina langu nitawafanyia.
Yeremia 33:3 Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua
 
Da! bujibuji naomba unielekeze kanisa unalosali please.
 
ubarikiwe pia
Dada nimefurahi sana unavojua kuchambua vifungu vya kutia moyo katika safari yetu tuliyonayo, kwa kuongezea tu na mimi natupia hivi hapa
Mithali 16:3 Mkabidhi Bwana kazi zako na mawazo yako yatathibitika
Mithali 3:5-6 Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako
Yohana 14:14 Mkiniomba cho chote kwa jina langu nitawafanyia.
Yeremia 33:3 Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua
 
ubarikiwe na topic nzuri sana, nimepata mafunzo ya kutosha, kuomba, kujianda, kusubiri (kutarajia)...sio kutafuta. Nilipotea hapo nyuma.
 
Back
Top Bottom