Ushauri kwa huyu binti

Ushauri kwa huyu binti

pakaywatek

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2014
Posts
4,710
Reaction score
6,372
Tunafanya naye kazi pamoja sasa wiki iliyopita yaani Jumatatu ya hiyo wiki, alinialika lunch kwenye hoteli ambayo ndiyo huwa tunakula lunch hapo.

Wiki nzima ananialika tukishakula nikitaka kulipa ananiambia usijali nimeshalipa, ilipofika Jumamosi wakati tumemaliza nikamwambia na mimi acha nilipe leo akagoma tukaondoka kurudi kazini.

Baada ya kazi akanambia tuonane hapo hapo kwenye compound akanieleza kwamba ana mpenzi wake ambaye huwa analipa bill kila mwisho wa mwezi hivyo nisijali na anapenda tuwe tunakula wote make ndo ana enjoy.

Nikamwambia sawa lakini mimi sitakula tena na atafute msichana mwenzake wawe wanakula pamoja sababu ni aibu mwanamme kula jasho la mwenzie.

Sasa tangu Jumatatu ya juzi binti kanuna lunch hali nikitaka kwenda kula ananiambia nikienda mwenyewe nitaona nikimwalika twende lunch ananiambia twende kule kule.Sasa hivi nashinda tu na njaa na yeye anashinda

Ushauri jinsi ya kumfanya aondokane na hili tatizo.

 
Kwanza kabisa nimependa mtazamo wako wa kuona si jambo zuri kula jasho la mwanaume mwenzio.
Labda ungemuuliza kwanini anataka aende na wewe? Na si mtu mwingine?
 
Yan ww usipokula naye hali?
Wakat chakula ananunuliwa na mpenz wake? Nadhan kuna tatizo maana au stor siyo ya kwel maana angekutaka asingelazimisha ule chakula kilichonunuliwa na mpenz wake na asingeona umuhim wa kula chakula cha huyo mpenz wake. Jaribu kumuuliza vizur

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Soma Alama Za Nyakati Huyo Dada Anakupenda Kuliko Mpenzi Aliye Naye Cha Msingi We Mtongoze Hiyo Ndo Dawa Na Suluhisho Lako

je ataweza kulipia billy ya mwenzi mzima ? huyo dada ni mchepuko wa mtu ambaye awazi kujenga maisha zaidi ana maintain aliyonayo... kijana wa watu anajijenga bado nauhakika
 
Jiandae kuletwa hapa JF ukipewa sifa ya U-Marioo
 
Achaaa hizoo utakua hushikwi na njaaa aiseee... # hayoo ni mahaba niuee
 
Hajashikwa na njaa huyo mnigiza tu chakula chenyewe chips hata sahani haijai ndio unalalama hali
 
Nahisi ananuna kwa sababu umeuruka mtego wa limbwata kabla hajaliweka kwa msosi wa ofa. Ushauri unao si umeshanielewa??????????
 
Hajashikwa na njaa huyo mnigiza tu chakula chenyewe chips hata sahani haijai ndio unalalama hali

asubuhi wamekunywa supu na chapati mbili kila mmoja huko anakotokea alafu mchana wanajifanya wanashinda njaa... eti wamefiana?
 
Kaka ni ela ya mwanaume ambaye anampenda huyo binti! Wewe utakisikiaje Kama mwanaume Atakuwa anakula hela yako kupitia mpenzi wako? Wacha kabisa hiyo ni mbaya stay away na jitahidini kuepusha visa vya wivu wa mapenzi vinavyosababisha vifo! Hawa wan awake ni Mama zetu twawapenda ila tukae nao kwa akili!

OTE=pakaywatek;11887962]Tunafanya naye kazi pamoja sasa wiki iliyopita yaani jumatatu ya hiyo wiki, alinialika lunch kwenye hoteli ambayo ndiyo huwa tunakula lunch hapo.

Wiki nzima ananialika tukishakula nikitaka kulipa ananiambia usijali nimeshalipa, ilipofika jumamosi wakati tumemaliza nikamwambia namimi acha nilipe leo akagoma tukaondoka kurudi kazini.

Baada ya kazi akanambia tuonane hapo hapo kwenye compound akanieleza kwamba ana mpenzi wake ambaye huwa analipa bill kila mwisho wa mwezi hivyo nisijali na anapenda tuwe tunakula wote make ndo ana enjoy.

Nikamwambia sawa lakini mimi sitakula tena na atafute msichana mwenzake wawe wanakula pamoja sababu ni aibu mwanamme kula jasho la mwenzie.

Sasa tangu jumatatu ya juzi binti kanuna lunch hali nikitaka kwenda kula ananiambia nikienda mwenyewe nitaona nikimwalika twende lunch ananiambia twende kule kule.Sasa hivi nashinda tu na njaa na yeye anashinda

Ushauri jinsi ya kumfanya aondokane na hili tatizo.
[/QUOTE]
 
Anaenjoy company yako kuliko huyo mpenzi hewa. Weka uhusiano weka clear, msijejichanganya.....ukajakatwa mananihii
 
Kweli umeshindwa kwenda kula sababu ya maneno hayo kwamba utaona.

Sasa ngoja akugande halafu ndio uone kweli.
 
Back
Top Bottom