Elections 2010 Ushauri kwa chama

Mvaa Tai

JF-Expert Member
Aug 11, 2009
6,159
4,443
Mimi nikiwa ni mmoja wa watu ninaye penda sana Burdani, nimegundua chama kina uwezo wa kuvunja taratibu za kampeni bila kufokewa na Msajiri wa Vyama vya siaasa wala Tume ya Taifa ya uchaguzi, hivyo basi kutokana na uwezo walionao kama chama ninaomba chama kiongeze mda na siku zake za kampeni na ikiwezekana kipeleke hata uchaguzi mbele zaidi ili tupate fursa ya kuwaona tena na tena Za commedy, Maluu, Mpooki, Wakuvyaanga na akina Cheege, kwani hii ina manufaa yafuatayo.

1. Inawelata Watanzania pamoja, (amani na mshikamano)

2. Kwa sisi tusio na uwezo wa kuwatoa wapenzi wetu out wala kwenda kumbi za starehe hii ni fursa pekee kufanya hivyo bila ghalama zozote. (maisha bora kwa kila mtanzania)
3. Kwa wafanya biashara ndogondogo kama pipi, karanga na sigara tunapata soko la mda mfupi lakini mauzo makubwa. (Kuwawezesha wajasiriamali)

4. Wasanii hupata maslahi kwani chama kina walipa vizuri. (Ajira)

Ombi

*Mwenyekiti wa Chama asihangaike kutuhutubia, akifika sanasana labda atufungulie muziki tuanze ku-enjoy, sisi ni waelewa sana na hatuna makuu, vinginevyo tungeweza kumfukuza kwa kutuahidi maisha bora kwa kila mtu na hamna dalili mpaka sasa ni miaka mitano imepita, tumekwisha muelewa anataka nini atuache tumfikirie hiyo October 31.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom