Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Chadema wametangulia akili sana, ungejiuliza ni kwa nini mikutano imewekwa mwezi mmoja mmoja mbele?

Kuna mabingwa wa mikakati wanazijuwa akili zenu ndogo mtalipuka mapovu yote kabla hata tarehe waliotangaza Chadema haijafika Dunia nzima itakuwa inajuwa kwamba kuna tatizo Magogoni.

Mimi ningelikuwa Rais ningewaambia wapinzani anaetaka kuandamana hata kila siku ruksa tu na aandamane.

Hii ndio best medicine aliitumia Nyerere kwa Mrema, aliwaambia Polisi wamwache Mrema tena tu si kwa wanaosukuma gari lake bali wambembe kabisa.

Bado sielewi kama ccm mpaka leo kama wanakumbuka sawasawa misingi ya mwalimu ilikuwa ni ipi!

Ili kuweka kumbukumbu sawa, nchi hii mtu wa kwanza kushtakiwa kwa kosa la uchochezi ni Baba wa Taifa.

Sawa. Maneno mengi ya nini? Tunasubiri tuone mkwara wenu hapo September 1.
 
Kuna watu humu wamebaki yatima wa kisiasa, Rais ni mkristo tena mkatoliki basi hawajui hata wafanyeje maana walijifanyaga ni mashabiki wa ccm kwa sababu kulikuwa na Rais ndugu yao katika imaani sasa Mkatoliki yupo kwenye ufalme wamebaki yatima wa kisiasa maana chuki yao ilikuwa kwa padre Slaa, sasa tumeweka mfuasi wa Vatican kabisa ikulu.
Tehe tehe tehe umeamka na faida leo
 
Unajua kwa tanzania elimu ya siasa na uraia kuna mapungufu sana........
Kiukweli wapinzani pamoja na serikali wote wanamaeneo wanakosea pia wanapatia.........
Nikianza na wapinzani........hawa mlengo wa hoja zao zimekaa kukosoa serikali sio kwa lengo la kuijenga bali kuiharibia ili nao wapate ridhaa ya wananchi katika kuliongoza taifa.....hili si jambo zuri hata kidogo.......huu ni usanii kabisa....

Nitawapa mfano wa inshu ya sukari.........wabunge wengi wa upinzani walichachamaa sana kwa kuwaambia wananchi kuwa serikali haiwatakii mema kwa kuzia uagizaji wa sukari usio fuata taratibu za kisheria za biashara katika manunuzi........nakumbuka walituhadaa wananchi kuwa sukari haitokuja kushuka maana serikali inakosea......leo hapa mimi nipo kilimanjaro nimetoka kununua sukari kilo 1800. Tokea ilipokuwa 3000. Sasa najiuliza huwa wapinzani wakiongea wanatumia taarifa za wapi.......maana ni kama wanapotosha uma.........mimi naona ni kama wanaweka jitihada nyingi kubeza jitihada zinazofanywa na kupotosha uma wa watanzania.......na asilimia kubwa ya watanzania si wafuatiliahi huwa wanajiridhisha na story za kusadikika ama za mtaani au post za facebook ambazo huwa wanaozipost hawajulikani ni akina nani plus wanamalengo gani.......

Swala la elimu......wanabeza sana maamuzi ya kuweka vigezo ambavyo vitarejesha thamani ya elimu sio kama sasa kila mtu anadegree uchwara halafu uwezo zero kazi kupiga domo tu.....wapinzani wanakazana kuropoka tu ili wapate hii popularity kama ya akina wema na diamond kwa kuropoka.......

Me nasema mh.raisi yupo sahihi kukataza hizi kelele zisizo na tija yeyote ........hawa wapinzani si muda wote.wapo sahihi......wanayohaki ya kuikanya......kuirekebisha na kuikosoa serikali.......ila sio kwa staili hii wanavyofanya ya kuibeza na kuikejeli badala ya kuishauri.............wapinzani hawaongei jipya kazi yao ni kubeza .Unapomkosoa mtu......toa suggestion ......au wazo mbadala ila sio unangojea mwenzako akosee ndipo povu likutoke........tena unatoa kauli za kuhatarisha amani na usalama wa raia........

serikali ni kweli inakosea kuwazuia wapinzani kuongea na uma lakini ni kwasababu wamegundua mnaitumia fursa hiyo kuongea vijembe.....na kukejeli serikali ndio maana wanawabana kwa kila namna .......hata ningekuwa mimi nisingeruhusu mtu ambaye hauna ridhaa ya kuendesha nchi uongee maneno ya uchochezi badala ya kutoa ushauri.......hii kitu alishaifanyaga mbatia mara moja tu......aliishauri serikali kuhusu kuhamisha maofisi yao maeneo ya posta na kuyasambaza maeneo mengine ili kupunguza msongamano wa foleni za magari asubuhi watu wanapokwenda makazini maana msongamano huu unaitia serikali hasara kila siku ya mabilioni......na ndio maana kikwete akamkubali sana akampa nafasi ubunge viti maalumu.........mrema huyo hapo amepewa nafasi anashirikiana na serikali......huo ndio upinzani wa ukweli unatakiwa kuwa sio hawa wakina zitto wanakwenda kusoma vitabu na notes za shule wanakuja kutuletea theory za utabiri hapa.....wanaboa sana......
Umeongea vizuri sana wote tungekuwa tunafikiria hivyo tungefika mbali.
 
Mkuu Pasco, kufa ni mara moja tu.
Ni kweli kufa ni mara moja tuu, ila sio mtu umeona moto halafu unakwenda kucheza na moto, ukiungua usilie! . Wafuasi wa Chadema sio watoto wa kuambiwa wacheze na wembe! , ushujaa ni kufa katika kupigania haki na kifo kikakukuta katika mapambano kama vitani lakini sio unakiona kifo kile kisha unakifuata mwenyewe kama walivyokufa Wafuasi wa Kibwetere au wale wa David Koresh wa Camp Davidians! .
Pasco
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!

Nitasimama na kuitetea nchi yangu,siwezi kuona mtu mmoja akiangamiza nchi.
 
Pasco huyo mtu wako ni PAPER TIGER na ni mharibifu toka eneo la waharibifu Dikteta Uchwara
Mkuu Magelemwa, uchwara ni isiyo halisi yaani yule anayejifanyisha tuu kama walivyo the barking dogs seldom bite! , mbwa koko hubwekwa sana ila ukimkaribia kimya na kuufyata mkia! .

Magufuli sio dikiteta uchwala ni dikiteta halisi kwa maneno na matendo ,ila tofautI na madikiteta wengine huyu ni dikiteta mzalendo anayefanya udikiteta kwa nia njema na dhamira safi ya kulikomboa taifa hili kwa sababu demokrasia, uhuru uliopitiliza, haki na utawala wa sharia ndio vimetufikisha hapa. Anachofanya ni kutumia udikiteta kidogo kwa kuiweka kando kidogo katiba na kuinyoosha kwanza nchi, maana kiukweli nchi ilikuwa imepinda sana, serikali ilikuwa imewekwa mifukoni na mafisadi, nchi ikiisha nyooka na kukaa kwenye mstari sasa ndipo tutazungumzia demokrasia na haki za binaadamu.

Pasco
 
Mbowe aliwakataza Bavicha wasiende dodoma watatumia njia za kimahakama kudai haki zao. Sasa nini kimebadili msimamo wao na Lowasa aliyewashauri kuwa maandamano hayasaidii? Hivi hawa ndugu zetu wanajua wanasimamia nini?
Mkuu Mtazamo, kama hata baada ya yote yanayozungumzwa na bado kuna wafuasi watajitokeza, nitaamini kweli hawa jamaa ni nyumbu! .

Naunga mkono haki ya kuandamana na haki ya kukusanyika ila mkiisha katazwa na mamlaka husika, hakuna sababu za kutunishiana misuli na mwenye nguvu, mwenye nguvu mpishe!.

Pasco
 
mwananchi.co.tz
MAONI YA MHARIRI: Jaji Mutungi simamia pia kanuni za haki,
Kwa ufupi

Mikakati hiyo ya Chadema, licha ya kuwaibua CCM ambao ni mahasimu wao wa kisiasa, pia imemuibua Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi aliyejitoa taarifa akisema tamko la Chadema limejaa lugha za uchochezi, kashfa na kuhamasisha uvunjifu wa amani.
Advertisement

Kumeibuka sintofahamu ya kisiasa baada ya chama cha Chadema kutangaza mikakati mitatu ya kupinga suala inaloliona kuwa ni ukandamizaji wa haki na demokrasia, ikiwa ndani ya operesheni iliyopewa jina la Umoja wa Kupambana na Udikteta Tanzania (Ukuta) na kufanya maandamano na mikutano nchi nzima kuanzia Septemba Mosi.

Mikakati hiyo ya Chadema, licha ya kuwaibua CCM ambao ni mahasimu wao wa kisiasa, pia imemuibua Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi aliyejitoa taarifa akisema tamko la Chadema limejaa lugha za uchochezi, kashfa na kuhamasisha uvunjifu wa amani.

Jaji Mutungi alinukuu vipengele kadhaa vya Sheria ya Vyama vya Siasa, Sura ya 258 kwenye kanuni na maadili ya vyama vya siasa za mwaka 2007.

Ni jambo jema kwamba Jaji Mutungi amefanya jitihada za kuvikumbusha vyama vya siasa umuhimu wa kufuata sheria na kanuni.

Tunakubaliana naye kwa kuwa alirejea Sehemu ya Tatu ya sheria hiyo inayozungumzia wajibu wa chama cha siasa wa kutunza maadili kwa kunukuu kanuni ya 5 (1) (d) inayovikataza vyama kutoa maneno ya uongo au maandishi ya uongo kuhusu mtu yeyote au chama chochote cha siasa.

Tunaamini kuwa kwa dhamira hiyohiyo Jaji Mutungi ataendelea kufanya hivyo kwa kugisa maeneo mengine mengi ya sheria hiyo. Mfano kanuni ya “c” inazuia matumizi ya vyombo vya dola kukandamiza na kutoa vitisho kwa chama chochote cha siasa.

Pia, kanuni “e” inaruhusu kufanya mkutano wa kisiasa na maandamano bila kufanya vurugu kwa mujibu wa sheria za nchi. Pia kifungu “f” kinavitaka vyama vya siasa kulaani na kupinga vitendo vyenye kuashiria ukandamizaji, matumizi ya lugha ya matusi, vitendo vya kibabe na vurugu, matumizi ya nguvu ili kujipatia umaarufu wa chama au sababu yoyote ile.

Pia kifungu “i” kinavitaka vyama vya siasa kuepuka kutumia mamlaka, rasilimali za Serikali, vyombo vya dola au wadhifa wa kiserikali, kisiasa au ufadhili wa nje ama wa ndani kwa namna yoyote ile ili kukandamiza chama kingine.

Tunatumaini kuwa weledi aliouonyesha Jaji Mutungi, ambaye pia ni katibu wa Baraza la Vyama vya Siasa, atauendeleza katika kusimamia haki za vyama vya siasa kama ilivyoelezwa Sehemu ya Pili ya kanuni ya 4(1) (b) kwamba chama kina haki ya kutoa maoni ya kisiasa kadri kitakavyoona inafaa ili kutekeleza sera zake kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Katiba ya Zanzibar.

Hatuna shaka kwamba Jaji Mutungi atasimamia kanuni “c” ya haki ya chama ili vipate fursa ya kujadili na kushindanisha sera zake na zile za chama kingine cha siasa kwa lengo la kutaka kukubalika kwa wananchi.

Kwa weledi ule ule tunaamini atahakikisha kanuni ya “d” ya haki ya chama inatoa fursa kama ilivyotamkwa kwamba viwe na uhuru wa kutafuta wanachama na kama ni wakati wa kampeni, basi kuwe na uhuru wa kutafuta kuungwa mkono na wapiga kura. Pia, tuna hakika atasimamia kanuni “e” inayotoa fursa kwa kila chama cha siasa kuwa na haki ya kufanya mikutano ya kisiasa na maandamano kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Siasa.

Ni vizuri Jaji Mutungi akasimamia sheria hiyo ya vyama vya siasa inayovipa haki za kufanya mikutano ya hadhara, kuandamana, kutafuta wanachama na kukemea jambo vinaloona ni la ukandamizaji ili kuondoa matatizo yanayoonekana kunyatia amani yetu.
Sheria iko wazi, kimsingi washauri wa raisi kama si kuwa wanamwogopa kuna jambo mkuu wetu haliko sawa. Kudhihilisha hilo hata msajili wa vyama vya siasa amekwepa vifungu vya sheria vinavyotoa haki za kidemokrasia kwa vyama vya siasa imelalia kipengele cha zuio bila kuweka bayana vipengele vyote vinavyotoa haki ya hayo maandamano na mikutano. Hii tafakari ya mhariri wa gazeti la mwananchi inatosha kutoa rejea kwa wanaopinga tamko la CHADEMA bila kuleta rejea za kisheria. Ukifuatilia michango ya wadau wa upande wa pili, hawana hoja ya msingi bali wanasimamia maneno ya raisi anayoendelea kutoa bila kuakisi ni wapi amekosea. #Kuna watu wanamwabudu rais hata kwenye makosa.
 
Pasco bana! UKUTA na wengine wote wanaomlalamikia Rais Magufuli wajaribu kukumbuka hali ya nchi ilivyokuwa. Kwa kweli inahitaji kuwa na kiongozi kama Magufuli kuweza kuirejesha nchi katika mstari. Magufuli ni msomi anayejua fika umuhimu wa Katiba. Je tunategemea aendelee kufuata mtindo wa uongozi ulioifikisha nchi hapo ilipokuwa kabla ya yeye kuingia madarakani? Ana miaka 5, mwacheni msaidieni!
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kutoa ushauri wa bure, huu ni ushauri wa bure kwa Chadema, japo kuandamana na mikutano ya kisiasa ni haki iliyotolewa kihalali ndani ya katiba, nawashauri kwa dhati kabisa, tafadhalini sana msiandamane, na kusitisha hiyo Operesheni UKUTA, ili kuutumia ule msemo wa Kiswahili "Mwenye nguvu mpishe", hata kama una haki, usitake kujipima nguvu kwa kutunishiana misuli na mtu mwenye nguvu zaidi yako, na sio tuu ana nguvu zaidi yako, na tayari, umeishajua ni dikiteta, bali ndio mwenye nguvu ya dola mikononi mwake!.

Misingi ya Katiba na The Rule of Law
Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya katiba na sheria, (the rule of law) ambapo inapaswa kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni, na sio kwa matamko ya viongozi yanayokwenda kinyume cha katiba!.

The Separation of Powers & Check and Balance .
Nchi yetu ina mihimili mikuu mitatu, Serikali, (the executive), Bunge (The Legislature) na Mahakama (The Judiciary). Mihimili hii mitatu, ilipaswa kufanya kazi kwa kujitegemea bila mhimili mmoja kuingilia mhimili mwingine (independence), huki kila mhimili uki act as a watchdog wa muhimili mwingine usivuke mipaka ya madaraka au mamlaka yake yaani (The sepaation of powers check and balance).

Serikali yenye Nguvu, Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo!.
Mihimili hii, inaongozwa na viongozi ambao wana mamlaka kuu kuhusu mihimili yao. President ndio mkuu wa the executive, Spika ndio mkuu wa The Legistlatue, na Jaji Mkuu, ndie mkuu wa The Judiciary, lakini pamoja na nia njema kuwa mihimili yote inamamlaka na hakuna mhimili wowote uliokuwa unapaswa kuwa na mamlaka kuliko mhimili mwingine, lakini kiukweli, mhimili wa the executive ndio mhimili mkuu unaomiliki vyombo vya dola na kuitawala mihimili mingine yote!, hivyo mkuu wa the executive, yaani rais, ndio kila kitu!, akisema!, amesema!.

Rais Magufuli na Uvunjaji wa Katiba.
Tuambiane ukweli, tangu rais Magufuli ameingia madarakani, sio mara moja au mbili amekuwa akitoa kauli tata, zinazokwenda kinyume cha katiba, mhimili wa Bunge na Mahakama ilipaswa kuingilia kati kwa kumcheck mkuu wa the executive, lakini vyombo hivyo vimekaa kimya hivyo kumfanya rais ajisikie kuwa he is always right! kwa kanuni ya "the boss is always right!".

Udikiteta wa Magufuli.
Hoja kama Magufuli ni dikiteta au la, haina mjadala, Magufuli ni dikiteta wa ukweli ambaye hana msalie mtume, na alipoingia tuu madarakani, alianza kuonyesha udikiteta wake right away kwa kuliingilia bunge na mahakama kuziweka chini ya amri zake!. Lile katazo lake la watumishi wa umma hawaruhusiwi kusafiri safari za nje bila kibali chake kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, liliwahusu watumishi wote wa serikali, likiwemo bunge na mahakama!, just imagine Jaji Mkuu na Spika wa bunge wakapige magoti kwa rais kuomba kutimiza wajibu wao!.

Baada ya katazo lile, checks and balance zingepaswa kuanzia hapo kwa Jaji Mkuu kumweleza rais huko ni kuingilia uhuru wa mahakama (the independence of the judiciary) hivyo muhimili wa mahakama haukupaswa kujisubmit chini ya the executuve, bali mamlaka hayo ya kuzuia safari za nje, Spika alipaswa kuwa nayo kudhibiti safari za mhimili wa bunge, na Jaji Mkuu alipaswa kuwana nayo kudhibiti safari za mhimili wa mahakama, lakini mihimili hii ilikaa kimya kwa kujisubmit chini ya the executive, hivyo kumfanya rais ndio kila kitu!.

Hivyo sasa rais Magufuli ndio kila kitu, hakuna cha bunge, mahakama, wala katiba, amri ya rais ndio kila kitu na ndio sheria kuu!, hivyo nawashauri Chadema kwa dhati kabisa, wasitishe maandamano yao, wasifanye kabisa mchezo wa kumjaribu Ngosha, wataumia bure!.

Hili la udikiteta wa rais Magufuli, tumeisha lizungumza sana humu
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...
Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia ...
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...
Utumbuaji Majipu wa Rais Magufuli: Is It A Right Thing, At The ...
Je, Hizi Terorizing za Ziara za Kushtukiza, Hakutajenga Nidhamu ya ...
Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote | Page ...
Nimetishwa, Kushitushwa na Kuogopeshwa na Kauli Hii ya Rais ...
Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ...
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa ...

Ila kitu kimoja kuzuri kuhusu udikiteta wa rais wetu, ni Rais Magufuli ni dikiteta mzalendo!, mwenye uchungu na umasikini wa nchi hii, mwenye nia njema ya kusafisha uozo wote wa uzembe, rushwa na ufisadi, na kulikomboa taifa letu toka kwenye lindi la umasikini uliotopea na kuwa nchi ya maziwa na asali kupitia uchumi wa gesi na viwanda.

Mungu mbariki Magufuli!.

Mungu ibariki Tanzania.

Wasalaam.

Pasco
Rejea za shauri za bure
Ushauri wa Bure Kwa Lowassa: Kwa Vile ni Magufuli, Kubali Matokeo ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura; Kaa ...
Ushauri wa Bure kwa CCM: Hope for the best but get prepared for ...
Ushauri wa Bure kwa Mhe. Lowassa: Ili kuilinda Heshima yako ...
Ushauri wa Bure kwa ZZK!-Congratulations..But,,,!, Be Calm!, Keep ...
Ushauri wa Bure Kwa Hon Dr. Harison Mwakyembe (Mb)-Kwa Hili la ...
Ushauri wa Bure Kwa Mhe. Zitto on Escrow Report: Please Keep Quite ...
Ushauri wa Bure kwa CHADEMA: Heri Nusu Shari Kuliko Shari Kamili ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Magufuli, Futilia Mbali Utawala wa Sheria ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Kikwete, muombe msamaha Lowassa kabla ya ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Usikanyage Arumeru!, Atamponza Sioi!.
Ushauri wa Bure kwa Dr. Shein: Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ...
Ushauri wa Bure kwa Magufuli, DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es ...

THEN KWA KIFUPI PASCO HAKUNA HAJA YA VYAMA VINGI UNTIL 2020
 
Serikali yenye Nguvu, Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo!.
Mihimili hii, inaongozwa na viongozi ambao wana mamlaka kuu kuhusu mihimili yao. President ndio mkuu wa the executive, Spika ndio mkuu wa The Legistlatue, na Jaji Mkuu, ndie mkuu wa The Judiciary, lakini pamoja na nia njema kuwa mihimili yote inamamlaka na hakuna mhimili wowote uliokuwa unapaswa kuwa na mamlaka kuliko mhimili mwingine, lakini kiukweli, mhimili wa the executive ndio mhimili mkuu unaomiliki vyombo vya dola na kuitawala mihimili mingine yote!, hivyo mkuu wa the executive, yaani rais, ndio kila kitu!, akisema!, amesema!.


Mungu ibariki Tanzania.

Wasalaam.

Pasco


Siyo kweli kwamba Raisi wa JMTZ ana Mamlaka sawa Spika au Jaji Mkuu huo ni upotoshaji mkubwa, Raisi wa JMTZ ndiyo kila kitu na hii ni kulingana na madaraka makubwa aliyo nayo Raisi wa JMTZ, kwani Raisi anaweza kuvunja Bunge muda wowote ule kama wakimzingua na hii ni Kikatiba kabisa ukija kwenye Mahakama raisi ndiyo anayetuea Majaji wote mpaka Jaji Mkuu hivyo indirectly ni kwamba ana nguvu juu yao whether unataka au hautaki kwa maana anayekuteua yuko juu yako hiyo ni common sense ya kawaida kabisa na kama hiyo haitoshi Raisi wa JMTZ ndiyo Mwenyekiti wa CCM Chama ambacho ndicho kilichotoa Spika na Naibu Spika na chenye Wabunge wengi klk vyote, hivyo kwa kuwa Spika ni Mbunge wa CCM ina maana Bosi wake ni Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Raisi wa JMTZ, hivyo basi ina maana Mwenyekiti wa CCM ana uwezo wa kusitisha Uanachama wa Mwanachama yoyote ikiwa pmj na Mbunge ambaye ndiye Spika wa Bunge la JMTZ, hivyo kwa kuzingatia hayo kusema kwamba Raisi kwa mujibu wa Katiba yetu ana madaraka sawa na Jaji Mkuu au Spika siyo kweli kwani,


Raisi wa JMTZ yuko juu ya Sheria ndani ya JMTZ!
 
Idd Amin dadaa alianzaga kidogo matamko,mbwembwe za ngoma,kutukana wapinzani wake na baadae akaanza kuua,kutesa na kula nyama za waganda.Watanzania tujenge UKUTA kabla mbo hayajawa magumu na uncontrollable
 
Lile BARAZA LA WAZEE LA CHAMA KILEEEEEE,huwa linafanya kazi saa ngapi?wako macho?wanaona upepo mkali ukivuma?wanaona mwelekeo wa jahazi?kwakuwa sisi si wazoefu,tunatamani watuhakikishie safari.
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kutoa ushauri wa bure, huu ni ushauri wa bure kwa Chadema, japo kuandamana na mikutano ya kisiasa ni haki iliyotolewa kihalali ndani ya katiba, nawashauri kwa dhati kabisa, tafadhalini sana msiandamane, na kusitisha hiyo Operesheni UKUTA, ili kuutumia ule msemo wa Kiswahili "Mwenye nguvu mpishe", hata kama una haki, usitake kujipima nguvu kwa kutunishiana misuli na mtu mwenye nguvu zaidi yako, na sio tuu ana nguvu zaidi yako, na tayari, umeishajua ni dikiteta, bali ndio mwenye nguvu ya dola mikononi mwake!.

Misingi ya Katiba na The Rule of Law
Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya katiba na sheria, (the rule of law) ambapo inapaswa kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni, na sio kwa matamko ya viongozi yanayokwenda kinyume cha katiba!.

The Separation of Powers & Check and Balance .
Nchi yetu ina mihimili mikuu mitatu, Serikali, (the executive), Bunge (The Legislature) na Mahakama (The Judiciary). Mihimili hii mitatu, ilipaswa kufanya kazi kwa kujitegemea bila mhimili mmoja kuingilia mhimili mwingine (independence), huki kila mhimili uki act as a watchdog wa muhimili mwingine usivuke mipaka ya madaraka au mamlaka yake yaani (The sepaation of powers check and balance).

Serikali yenye Nguvu, Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo!.
Mihimili hii, inaongozwa na viongozi ambao wana mamlaka kuu kuhusu mihimili yao. President ndio mkuu wa the executive, Spika ndio mkuu wa The Legistlatue, na Jaji Mkuu, ndie mkuu wa The Judiciary, lakini pamoja na nia njema kuwa mihimili yote inamamlaka na hakuna mhimili wowote uliokuwa unapaswa kuwa na mamlaka kuliko mhimili mwingine, lakini kiukweli, mhimili wa the executive ndio mhimili mkuu unaomiliki vyombo vya dola na kuitawala mihimili mingine yote!, hivyo mkuu wa the executive, yaani rais, ndio kila kitu!, akisema!, amesema!.

Rais Magufuli na Uvunjaji wa Katiba.
Tuambiane ukweli, tangu rais Magufuli ameingia madarakani, sio mara moja au mbili amekuwa akitoa kauli tata, zinazokwenda kinyume cha katiba, mhimili wa Bunge na Mahakama ilipaswa kuingilia kati kwa kumcheck mkuu wa the executive, lakini vyombo hivyo vimekaa kimya hivyo kumfanya rais ajisikie kuwa he is always right! kwa kanuni ya "the boss is always right!".

Udikiteta wa Magufuli.
Hoja kama Magufuli ni dikiteta au la, haina mjadala, Magufuli ni dikiteta wa ukweli ambaye hana msalie mtume, na alipoingia tuu madarakani, alianza kuonyesha udikiteta wake right away kwa kuliingilia bunge na mahakama kuziweka chini ya amri zake!. Lile katazo lake la watumishi wa umma hawaruhusiwi kusafiri safari za nje bila kibali chake kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, liliwahusu watumishi wote wa serikali, likiwemo bunge na mahakama!, just imagine Jaji Mkuu na Spika wa bunge wakapige magoti kwa rais kuomba kutimiza wajibu wao!.

Baada ya katazo lile, checks and balance zingepaswa kuanzia hapo kwa Jaji Mkuu kumweleza rais huko ni kuingilia uhuru wa mahakama (the independence of the judiciary) hivyo muhimili wa mahakama haukupaswa kujisubmit chini ya the executuve, bali mamlaka hayo ya kuzuia safari za nje, Spika alipaswa kuwa nayo kudhibiti safari za mhimili wa bunge, na Jaji Mkuu alipaswa kuwana nayo kudhibiti safari za mhimili wa mahakama, lakini mihimili hii ilikaa kimya kwa kujisubmit chini ya the executive, hivyo kumfanya rais ndio kila kitu!.

Hivyo sasa rais Magufuli ndio kila kitu, hakuna cha bunge, mahakama, wala katiba, amri ya rais ndio kila kitu na ndio sheria kuu!, hivyo nawashauri Chadema kwa dhati kabisa, wasitishe maandamano yao, wasifanye kabisa mchezo wa kumjaribu Ngosha, wataumia bure!.

Hili la udikiteta wa rais Magufuli, tumeisha lizungumza sana humu
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...
Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia ...
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...
Utumbuaji Majipu wa Rais Magufuli: Is It A Right Thing, At The ...
Je, Hizi Terorizing za Ziara za Kushtukiza, Hakutajenga Nidhamu ya ...
Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote | Page ...
Nimetishwa, Kushitushwa na Kuogopeshwa na Kauli Hii ya Rais ...
Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ...
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa ...

Ila kitu kimoja kuzuri kuhusu udikiteta wa rais wetu, ni Rais Magufuli ni dikiteta mzalendo!, mwenye uchungu na umasikini wa nchi hii, mwenye nia njema ya kusafisha uozo wote wa uzembe, rushwa na ufisadi, na kulikomboa taifa letu toka kwenye lindi la umasikini uliotopea na kuwa nchi ya maziwa na asali kupitia uchumi wa gesi na viwanda.

Mungu mbariki Magufuli!.

Mungu ibariki Tanzania.

Wasalaam.

Pasco
Rejea za shauri za bure
Ushauri wa Bure Kwa Lowassa: Kwa Vile ni Magufuli, Kubali Matokeo ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura; Kaa ...
Ushauri wa Bure kwa CCM: Hope for the best but get prepared for ...
Ushauri wa Bure kwa Mhe. Lowassa: Ili kuilinda Heshima yako ...
Ushauri wa Bure kwa ZZK!-Congratulations..But,,,!, Be Calm!, Keep ...
Ushauri wa Bure Kwa Hon Dr. Harison Mwakyembe (Mb)-Kwa Hili la ...
Ushauri wa Bure Kwa Mhe. Zitto on Escrow Report: Please Keep Quite ...
Ushauri wa Bure kwa CHADEMA: Heri Nusu Shari Kuliko Shari Kamili ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Magufuli, Futilia Mbali Utawala wa Sheria ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Kikwete, muombe msamaha Lowassa kabla ya ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Usikanyage Arumeru!, Atamponza Sioi!.
Ushauri wa Bure kwa Dr. Shein: Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ...
Ushauri wa Bure kwa Magufuli, DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es ...

Pasco wewe tayari tumesha kustukia kuwa unatumika sasa na watawala hivyo ushauri wako peleka huko huko kwenu lumumba
 
Pasco usipotoshe. Kinachoitwa separation of powers ni katika sub-system ya utawala - ndani (siyo nje) ya Bunge na Mahakama. Rais wa nchi ndiye Mkuu wa nchi na Serikali. Serikali ndiyo yenye mamlaka ya kuanzisha, kuratibu na kusimamia utekelezaji wa sera na sheria zote za nchi. Mahaakama na Bunge hukutana na Serikali (executive) katika eneo moja dogo katika kuendesha serikali - sheria (administration of justice). Bunge hutunga sheria wakati Mahakama hutafsiri sheria ili kutoa haki, basi. Si Mahakama wala Bunge mwenye mamlaka ya kutunga na tutekelea sera zake kwa namna watakavyo. Kwa hiyo uamuzi wa Serikali/JPM kudhibiti fiscal extravagance ulitakiwa kutekelezwa na Bunge na Mahakama bila kusita. It was a genuine, rightful, timely and constitutionally mandated supreme order.
Mkuu Sophist, kwanza nimefarijika sana kwa mchango wako kwa sababu wewe ndio mtu wa kwanza kuchangia kuhusu the separation of powers tena kwa kupangua hoja kwa hoja japo you are not right but you've tried.

Lengo la the principal of the separation of powers and checks and balance ni ili kuuzuia mhimili mmoja usijiinue kupitiliza. Bunge ni mtunga sheria, mahakama mfasiri na serikali mtekelezaji, serikali inapotunga a draconian law na Bunge likaipitisha Mahakama inauwezo wa kuifutilia mbali. Serikali ikitenda kwa kukiuka, kutokutenda au kukandamiza, mahakama kupitia powers zake inatoa executive orders, au writs za prohibition, certiorary na mandamus kuiamuru serikali itake isitake! .

Kitendo cha the executive kuingilia freedom of movement kwa mhimili ya Bunge na Mahakama ni kuingilia the independence ya mihimili hii.

Haki ya vyama vya siasa kukutana na kufanya mikutano ni haki iliyomo kwenye katiba, haki hii sio territorial lakini rais ameingilia haki hii kinyume cha katiba kama ilivyo rais hana mamlaka yoyote ya kupunguza mshahara wa mtumishi yoyote.

Rais Magufuli ametoa kauli kibao za uvunjaji wa katiba Bunge na Mahakama vinaangalia tuu.

Pale kunapotokea kauli za uvunjaji wa katiba au kinyume cha haki za binaadamu kama zilivyoainishwa kwenye katiba, Mahakama ina mamlaka ya ku act kwa mtindo unaoitwa act on suo motto, ni acting on it's own volition na kutoa tafsiri ya katiba ili maandishi nini bila hata kumsubiri yoyote kufungua shauri.

Bunge linapoona rais anatenda ndiyo sivyo lina mamlaka kujadili kauli za rais na kuzitolea azimio la Bunge.

Lakini hebu tusemezane ukweli, Jaji Chande na Spika Ndungai na Naibu Dr. Tulia ni watu wa kutengemewa kumfanyia checks Magufuli huku wengine wamefanywa kubebwa na wengine ni wastaafu siku nyingi wanaendelea na kazi kwa hisani tuu ya Magufuli.

Tanzania tunafuata mfumo wa presidential ambao rais ndio kila kitu, Bunge ni Butu na Mahakama ni Kibogoyo haina meno ya kuingata serikali, ndio maana nawashauri Chadema Mkuu wa the executive akisema hiki usifanye, hata kama wewe ndio mwenye haki, usifanye kwa sababu kauli hiyo ni final na conclusive! . Japo katiba yetu inasisitiza no one's is above the law, rais wetu is over and above the law! . Yeye ndio katiba, ndio Bunge, ndio mahakama na ndiye the law kubali kataa. Mtu wa namna hii akisema hapana ni hapana.

Pasco
 
Back
Top Bottom