Inkoskaz
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 6,372
- 2,374
Kikao hiki ni muhimu sana katika ratiba ya vikao vya bunge kila mwaka hivyo na kwa kuwa wawakilishi wetu japo sio wote lakini wengi ni wageni mjengoni sio vibaya tukishare mawazo mbalimbali humu mitandaoni kwa faida yenu nyinyi wenye mic huko bungeni
1.Mjenge utaratibu wa kusoma kwa makini vijitabu vya bajeti,kutafakari na kuweza kuibua hoja pale panapohitajika marekebisho
2.Muwe na vikao vyenu vya marejeo na majumuisho ya mliyojadili na mtakayojadili kila mwishoni mwa wiki japo na ninyi mnahitaji kupumzisha akili kule mnadani
3.Kutofautiana hoja mbalimbali isiwe sababu ya kuwabomoa,wekeni namna ya kuzijadili hoja binafsi na kukubaliana kabla hazijawakilishwa na mhusika
4.Wanachama,wapenzi na wafuasi wa CDM wapo wametapakaa kila kona na humu mitandaoni wapo,msisite kuwaomba ushauri na pia kusikiliza maoni yao kwa kila bajeti husika i.e Miundombinu-Engineers,Katiba na Sheria-Lawyers,Afya-Doctors,Elimu-Walimu,nishati na Madini-Consultants,Kilimo,ufugaji,uvuvui,watoto,kazi,mambo ya ndani kote kuna wataalam etc..etc..
5.Pingeni kwa nguvu ule utaratibu wa kupiga kura kwa kujibu ndiyo au hapana,uwepo utaratibu wa siri(kumbuka hata wabunge CCM wanaweza kuwa na support kwenu lakini kwenye kura ya kusimama na kujibu akakionea chama chake aibu akajibu kinyume na nafsi yake) refer ule muswada wa sheria za mahakama kikao kilichopita.
Technology imekuwa sana,unaweza hapo kwenye meza yako ukapress button ya yes or no na rekodi ya kura yako ikaingia na kujumlishwa bila kuchakachuliwa
6.Maswali ya Nyongeza is a must yale ndio muhimu kwani majibu ya awali huwa ni uwongo uliokwishaandaliwa,sasa mkiwa na maswali mazuri ya nyongeza tuna hakika ya kujua waziri alichojibu anakielewa au alikesha 84
7.Nidhamu ya kikao,Mahudhurio ya vikao vyote bila kukosa labda kwa udhuru maalumu na kujali muda wa kuanza vikao,waacheni hao wanaosema wana majukumu ya uwaziri nk,nyinyi pigeni mzigo matokeo mtayaona
Najua wenzangu nao wana mengi waliyonayo watawaeleza hivyo mkipata wasaa japo chungulieni humu mtapata hazina ya mawazo yao
Nawatakia kikao chema na motomoto
1.Mjenge utaratibu wa kusoma kwa makini vijitabu vya bajeti,kutafakari na kuweza kuibua hoja pale panapohitajika marekebisho
2.Muwe na vikao vyenu vya marejeo na majumuisho ya mliyojadili na mtakayojadili kila mwishoni mwa wiki japo na ninyi mnahitaji kupumzisha akili kule mnadani
3.Kutofautiana hoja mbalimbali isiwe sababu ya kuwabomoa,wekeni namna ya kuzijadili hoja binafsi na kukubaliana kabla hazijawakilishwa na mhusika
4.Wanachama,wapenzi na wafuasi wa CDM wapo wametapakaa kila kona na humu mitandaoni wapo,msisite kuwaomba ushauri na pia kusikiliza maoni yao kwa kila bajeti husika i.e Miundombinu-Engineers,Katiba na Sheria-Lawyers,Afya-Doctors,Elimu-Walimu,nishati na Madini-Consultants,Kilimo,ufugaji,uvuvui,watoto,kazi,mambo ya ndani kote kuna wataalam etc..etc..
5.Pingeni kwa nguvu ule utaratibu wa kupiga kura kwa kujibu ndiyo au hapana,uwepo utaratibu wa siri(kumbuka hata wabunge CCM wanaweza kuwa na support kwenu lakini kwenye kura ya kusimama na kujibu akakionea chama chake aibu akajibu kinyume na nafsi yake) refer ule muswada wa sheria za mahakama kikao kilichopita.
Technology imekuwa sana,unaweza hapo kwenye meza yako ukapress button ya yes or no na rekodi ya kura yako ikaingia na kujumlishwa bila kuchakachuliwa
6.Maswali ya Nyongeza is a must yale ndio muhimu kwani majibu ya awali huwa ni uwongo uliokwishaandaliwa,sasa mkiwa na maswali mazuri ya nyongeza tuna hakika ya kujua waziri alichojibu anakielewa au alikesha 84
7.Nidhamu ya kikao,Mahudhurio ya vikao vyote bila kukosa labda kwa udhuru maalumu na kujali muda wa kuanza vikao,waacheni hao wanaosema wana majukumu ya uwaziri nk,nyinyi pigeni mzigo matokeo mtayaona
Najua wenzangu nao wana mengi waliyonayo watawaeleza hivyo mkipata wasaa japo chungulieni humu mtapata hazina ya mawazo yao
Nawatakia kikao chema na motomoto