Mangwea1900
JF-Expert Member
- May 29, 2025
- 2,485
- 3,224
Siku ulipoanza kusimama katika majukwaa ya kisiasa ndipo nilipopata shida moyoni kuhusu mahusiano yako na Mungu. Siasa na imani za dini ni sawa na mafuta na maji. Dini lengo lake kuu ni kuwaelekeza watu kufika mwisho mwema baada ya maisha ya hapa duniani.
Unachokifanya kwa sasa unaendelea kujiharibia kwa wenye kujua neno.
1. Mtumishi hatakiwi kuwa mwanaharakati.
2. Mtumishi wa Mungu hapaswi kuwa mwanasiasa.
3. Mtumishi wa Mungu vita vyake ni vya kiroho sio mwilini.
4. Mtumishi wa Mungu huongozwa na roho wa Mungu peke yake katika kila anachokifanya.
Katika video zako YouTube Askofu Gwajima inaonekana unajipendekeza au kujificha kwa kujidai unatetea maslahi yao ili hali wapo waajiriwa wa kada za chini wana changamoto kuliko ukianzia kwa vibarua katika viwanda na makampuni binafsi ukiachilia mbali walimu wauza visheti.
Hotuba zako unaongea kiswaenglish huku kwetu uswazi tunaona unajidai na unalenga daraja fulani la wananchi.
Askofu Gwajima, tubu dhambi zako kwa kumsikiliza roho wa Mungu na urudi kufanya kazi madhabahuni umeingia mtegoni ;"Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika."— Mathayo 26:31/Zekaria 13:7
Yoeli 2:12-13
“Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuomboleza; rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa yeye ni mwenye neema na rehema, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa fadhili, naye hughairi mabaya.”
Aliye na masikio na asikie
Unachokifanya kwa sasa unaendelea kujiharibia kwa wenye kujua neno.
1. Mtumishi hatakiwi kuwa mwanaharakati.
2. Mtumishi wa Mungu hapaswi kuwa mwanasiasa.
3. Mtumishi wa Mungu vita vyake ni vya kiroho sio mwilini.
4. Mtumishi wa Mungu huongozwa na roho wa Mungu peke yake katika kila anachokifanya.
Katika video zako YouTube Askofu Gwajima inaonekana unajipendekeza au kujificha kwa kujidai unatetea maslahi yao ili hali wapo waajiriwa wa kada za chini wana changamoto kuliko ukianzia kwa vibarua katika viwanda na makampuni binafsi ukiachilia mbali walimu wauza visheti.
Hotuba zako unaongea kiswaenglish huku kwetu uswazi tunaona unajidai na unalenga daraja fulani la wananchi.
Askofu Gwajima, tubu dhambi zako kwa kumsikiliza roho wa Mungu na urudi kufanya kazi madhabahuni umeingia mtegoni ;"Nitampiga mchungaji, na kondoo wa kundi watatawanyika."— Mathayo 26:31/Zekaria 13:7
Yoeli 2:12-13
“Lakini hata sasa, asema Bwana, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuomboleza; rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie Bwana, Mungu wenu; kwa kuwa yeye ni mwenye neema na rehema, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa fadhili, naye hughairi mabaya.”
Aliye na masikio na asikie