Naomba kuuliza kwa wale wataalam wetu wa mambo ya simu au yeyote mwenye ufahamu naomba anisaidie katika hili. Ninasimu yangu inatumia Micro-SD na nilikuwa naishi nje ya nchi lakini sasa nataka kurejea TZ na kwa msingi huo nitahitaji kutumia laini zetu za kawaida za Voda, Tigo, n.k. Sasa swali langu ni kwamba, vipi hizo laine za simu za hapo Tanzania naweza kupata Micro-sd nitakayoweza kutumia kwenye simu yangu??? Kwani simu yangu ina sehemu ndogo cha line kiasi kwamba hizo normal lines za Vodacom, Tigo, n.k za hapo TZ haziwezi kuingia. Au kuna utaalam wowote wa kukata hizo kadi na kuwa micro ili iweze kuingia kwenye simu isiyotumia laini zenye ukubwa wa kawaida?
Naombeni ushauri katika hilo.
Ahsanteni na Kristmas njema kwa wote mtakaosoma uzi huu.
Naombeni ushauri katika hilo.
Ahsanteni na Kristmas njema kwa wote mtakaosoma uzi huu.