Ushauri: Kuendana na utawala huu, jitahidi kufanya haya

mwambadog

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
1,736
1,447
habarini wadau

kila utawala huwa na mambo yake mzuri na mabaya. nijukum lako wewe kama mwananchi, kiongozi na wakuu wa taasisi mbali mbali za dini kuweza kuendana na tawala hio, ili kufikia malengo yako, uwaongozao au taasisi unayowakilisha.

MWANANCHI
mwananchi wa kawaida kuwa mbinafsi wa kuakikisha maisha yako yanakuwa bora vile upendavyo baada ya kujiridhisha na mafanikio yako kumbuka kuwasaidia wahitaji wanaokuzunguka. kamwe usitegemee hii serikali kukupa mazingira bora ya kubadili maisha yako maana utaumia. kuna maamuzi mabaya yamefanywa na hii serikali na mengine mengi tu itaharibu, lakini ili uendane na zama hizi usiruhusu maamuzi hayo yakuguse wewe, kilasiku umiza kichwa kupata mkate.

VIONGOZI WA SERIKALI
hakikisha hujipendekezi kwa ubunifu usiokuwa na hakika nao. vizuri kila jambo ufanyalo upate baraka za kiongozi wako wa juu, tena si kwa maneno pendelea baraka hizo ziwe katka maandishi. pia hata ukiona kitu au jambo ambalo unaamini ni baya kabla hujakosoa angalia nani kalitoa......

VIONGOZI WA DINI NA TAASISI ZA DINI
ni bora kuwa na uwezo mzuri wa kubalance mambo. najua mnawapenda waumini wenu pia mwapenda support za hawa wanasiasa. nivizuri kama waamini wenu hawatapoteza imani na hiizi taasisi. hata kama unamawazo tofauti usitoe mpaka ujiridhishe na mitazamo ya waamini wenu, itapunguza misuguano na mwisho wa siku tutakuwa na nchi salama.

wote twataka kuishi sehemu iliyo salama na tulivu
 
Back
Top Bottom