Ushauri juu ya Swala hili Tafadhali

Ushauri juu ya Swala hili Tafadhali

Joel360

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2013
Posts
986
Reaction score
657
Nimekuwa na uhusiano na msichana mmoja kwa muda wa mwezi mmoja na tuliahidiana mambo yakikaa sama tutaoana kwani tayari wazazi wanajua kuhusu swala hili.

Lakini kinachoniumiza ni kuwa nina rafiki yangu wa karibu ambaye anadai kuwa anasumbuliwa na huyu dada jambo ambalo kwa mara ya kwanza sikuliamini, lakini nilikuja kuamini baada ya kuona ujumbe wake simu ya rafiki yangu na pia siku hizi hana furaha yoyote anapokuwa na mimi na ninapomuuliza anakuwa mkali kidogo kwenye kunijibu. Jambo lingine linaloniumiza ni kuwa amekuwa akiwatangazia watu kuwa mimi ninamsumbua kimapenzi kitu ambacho sikufanya ila uhusiano wetu ulikuwa wa makubaliano kati yangu mimi na yeye.

Yani kwa sasa sijui nifanye kwa sababu wazazi wote wanajua wazi kwamba muda si mrefu tutafunga ndoa na mambo anayofanya ndo kama hivi, nifanyeje? Nikisema nimuache nitachora picha mbaya kwa wazazi wangu na wake kwa sababu wazazi wangu wanampenda sana dada huyu, na wazazi huwa wanamsifia mtoto wao kuwa ni mwenye tabia njema nifanyeje?
 
Wazazi na familia weka pembeni, fanya maamuzi ya kiume

Mwache huyo msichana atakusumbua mbeleni
 
hata hili linahitaji ushauri jamani, liko wazi kabisa
 
Uhusiano wa mwez mmoja wazaz wanajua? Na mnampango wa kufunga ndoa!? Aisee unashangaza kweli!!......... Ndio matatiza ya kukurupukia wanawake na kuwaahidi ndoa kabla hamjajuana
 

Mbona mnaharaka Sana kama mnaoga nje? Mwezi mmoja Tu mnatambulishana kweli?

Fanya chochote utakachojisikia kufanya kwani nani alikushauri ukamtambulishe kwenu?
 
Kama wazazi hawakushangaa mlipojitambulisha kwao na kuahidiana ndoa ndani ya mwezi mmoja tangu muanze mahusiano basi hakuna litakalowashangaza kuwahusu hata wakisika mmeachana!!
 
Unapowaza kujenga nyumba nini kinaanza? Paa au Msingi?

Inavyoonekana wewe unataka kuanzia kujenga Paa kwanza. Unaoa Mke wako na sio wa wazazi wako? unaoa mtu anayekupenda sio anayekuponda na kuwataka rafiki zako? Kwani wazazi wako kwa mfano wakikuona na kitu cha kununua wakamsifia kwa kuwa hawamjui vizuri we utaoa tu kwa kuwa wazazi wameonesha kumpenda?

Kama unaoa mke wa wazazi MUOE huyo afu utakiona baadae.
Nimekuwa na uhusiano na msichana mmoja kwa muda wa mwezi mmoja na tuliahidiana mambo yakikaa sama tutaoana kwani tayari wazazi wanajua kuhusu swala hili.

Yani kwa sasa sijui nifanye kwa sababu wazazi wote wanajua wazi kwamba muda si mrefu tutafunga ndoa na mambo anayofanya ndo kama hivi, nifanyeje? Nikisema nimuache nitachora picha mbaya kwa wazazi wangu na wake kwa sababu wazazi wangu wanampenda sana dada huyu, na wazazi huwa wanamsifia mtoto wao kuwa ni mwenye tabia njema nifanyeje?
 
Nimekuwa na uhusiano na msichana mmoja kwa muda wa mwezi mmoja na tuliahidiana mambo yakikaa sama tutaoana kwani tayari wazazi wanajua kuhusu swala hili.

Lakini kinachoniumiza ni kuwa nina rafiki yangu wa karibu ambaye anadai kuwa anasumbuliwa na huyu dada jambo ambalo kwa mara ya kwanza sikuliamini, lakini nilikuja kuamini baada ya kuona ujumbe wake simu ya rafiki yangu na pia siku hizi hana furaha yoyote anapokuwa na mimi na ninapomuuliza anakuwa mkali kidogo kwenye kunijibu. Jambo lingine linaloniumiza ni kuwa amekuwa akiwatangazia watu kuwa mimi ninamsumbua kimapenzi kitu ambacho sikufanya ila uhusiano wetu ulikuwa wa makubaliano kati yangu mimi na yeye.

Yani kwa sasa sijui nifanye kwa sababu wazazi wote wanajua wazi kwamba muda si mrefu tutafunga ndoa na mambo anayofanya ndo kama hivi, nifanyeje? Nikisema nimuache nitachora picha mbaya kwa wazazi wangu na wake kwa sababu wazazi wangu wanampenda sana dada huyu, na wazazi huwa wanamsifia mtoto wao kuwa ni mwenye tabia njema nifanyeje?

Haaaa mwezi moja mpaka wazazi wanajua duuh zaidi ya marathon... anyway huna chako hapo... swali lakizushi mshamgegedana??
 
UUUUUUUPSIIIIIIII

RELATION one month WAZAZI WANAJUA????BE SERIOUS NA NDOA UNAPLAN????

OMG dont rush i lov jaman mbio za nini???
mapenz yalikuwepo,ypo na yataendelea real gentman hasumbuliwi hasa ishu kama hii ambayo inagusa maisha yake.

mada za leo vijana mlalia lia duuu
 
Uhusiano wa mwez mmoja wazaz wanajua? Na mnampango wa kufunga ndoa!? Aisee unashangaza kweli!!......... Ndio matatiza ya kukurupukia wanawake na kuwaahidi ndoa kabla hamjajuana
Inawezekana ni mgeni katika sekta hiyo
 
Haaaa mwezi moja mpaka wazazi wanajua duuh zaidi ya marathon... anyway huna chako hapo... swali lakizushi mshamgegedana??

umeua hapo kwenye Marathon
sina cha kuongeza, labda nisubiri jibu la swali ulilomuuliza!!
 
ukitaka ujutie maamuzi yako maisha yako yote oa huyo dada.Halafu wenzako hatuendagi kasi hivyo mapenzi yanahitaji kupeana muda wa kufahamiana vizuri ndipo taratibu nyingine zinafata.....
Mwezi mmoja huez ukasema umemfaham mtu vizuri na huez sema unampenda kweli kweli hata maji hayapiti kwenye koo,kwani mapenz ya mwanzo ni sweeter than kuku...WATCH OUT
 
umeua hapo kwenye Marathon
sina cha kuongeza, labda nisubiri jibu la swali ulilomuuliza!!
Mwanachama mwenzangu karibu sana

Umeingia muda muafaka mambo moto moto hakuna kusinzia tangu nilipoingia
 
inaonekana mtoa mada kazama kwa huyu binti...ila binti yuko kimaslahi zaid
shtuka broh!
 
uhusiano una mwezi mmoja na wazazi wote wanajua?....mna speed
ndani ya mwezi mmoja anamsumbua rafiki yako na wewe unaona ,halafu hujui cha kufanya,kweli?
pole sana

Na Mimi icho cha mwezi mmoja kmenistua.
 
umeua hapo kwenye Marathon
sina cha kuongeza, labda nisubiri jibu la swali ulilomuuliza!!

ha ha ha kwa hzi spidi hawa tayari washagegedana labda tuulize kama ana mimba
 
Nimekuwa na uhusiano na msichana mmoja kwa muda wa mwezi mmoja na tuliahidiana mambo yakikaa sama tutaoana kwani tayari wazazi wanajua kuhusu swala hili.

Lakini kinachoniumiza ni kuwa nina rafiki yangu wa karibu ambaye anadai kuwa anasumbuliwa na huyu dada jambo ambalo kwa mara ya kwanza sikuliamini, lakini nilikuja kuamini baada ya kuona ujumbe wake simu ya rafiki yangu na pia siku hizi hana furaha yoyote anapokuwa na mimi na ninapomuuliza anakuwa mkali kidogo kwenye kunijibu. Jambo lingine linaloniumiza ni kuwa amekuwa akiwatangazia watu kuwa mimi ninamsumbua kimapenzi kitu ambacho sikufanya ila uhusiano wetu ulikuwa wa makubaliano kati yangu mimi na yeye.

Yani kwa sasa sijui nifanye kwa sababu wazazi wote wanajua wazi kwamba muda si mrefu tutafunga ndoa na mambo anayofanya ndo kama hivi, nifanyeje? Nikisema nimuache nitachora picha mbaya kwa wazazi wangu na wake kwa sababu wazazi wangu wanampenda sana dada huyu, na wazazi huwa wanamsifia mtoto wao kuwa ni mwenye tabia njema nifanyeje?
Achana na habari ya wazazi wewe ndie unayemjua kindakindaki ,halafu ndugu yangu uchumba wa mwezi mmoja si uchumba umekuwa na haraka mno ya kutambulisha u need at least one year agano la ndoa ni la milele sasa unakimbilia nini ?
Kwa vyovyote vile lazima abehave mbele ya wazazi wako ili kuficha makucha yake marefu kama meno ya ngiri
 
Back
Top Bottom