Ushauri jamani

Ushauri jamani

Duh!
20 years!!
Una mpenzi!!
Mpenzi nyumbani wanamjua!!

Mweeh! Tanzania hiihii.Kweli utandawazi umefika hadi kwa wazazi

Mdogo wangu achana na haya mambo kwa sasa,kila kitu kina wakati wake na kwa sasa ni wakati wa wewe kusoma.
 
Ungekuwa ni mdogo wangu nina uhakika kwa miaka hiyo yako 20 Mzee Malafyale angemfukuza huyo mmeo lkn nyie kwenu hadi wanamjua wazazi wako na wanamkubali?
Miaka 20 si ulitakiwa wewe uwe koleji au?
 
Pole mwaya tulia tu utapata aliye mwema kwako
 
Mimi ni msichana mwenye umri wa miaka 20 nina mpenz wangu ambaye nampenda sana, na yeye pia ananipenda sana na mpaka nyumbani wameshamjua, na ananihudumia kwa kila kitu ninachotaka. Tulipoanza mahusiano nilimuuliza kama kaoa akakataa ila akasema ana mtoto mmoja, sasa hivi juzi nimeingia fb nikakuta picha yake mkewe na watoto wao wawili, na ahadi yetu ni kufunga ndoa na kumbe dini alinidanganya yeye muislam mimi mkristo na alisema yeye mkristo nifanye nini jamani maana hapa nilipo hadi nimeumwa mwenzenu baada ya kujua ni mume wa mtu.

Pole sana. Hapo unapoteza muda wako huyo ni mine wa mtu kwako anachepuka tu.
 
Mie ndio maana napenda mwanaume akiniambia anamke tena namkubar kirahc kuliko awa rika la kati waongo sanaa.....ushaur wang tafta mume wa mtu mawazo yote yataisha na utamsahau uyo mwongo wakoo

Duuh !!!!
unamshauri atafute mume wa mtu.........
Yaani awe japo si lazima "chanzo cha kuvunjika ndoa ingine"

Ok tuseme atafute mume wa mtu na uyo mwenye mme unamfikiriaje?
 
Duuh !!!!
unamshauri atafute mume wa mtu.........
Yaani awe japo si lazima "chanzo cha kuvunjika ndoa ingine"

Ok tuseme atafute mume wa mtu na uyo mwenye mme unamfikiriaje?

Mwenye mume atajijua
 
Back
Top Bottom