Useful pointers to CHADEMA: Civil disobedience and passive resistance

Nyani Ngabu

Platinum Member
May 15, 2006
92,252
113,647
CHADEMA,

Kwa vile sasa mmeshakiri rasmi kwamba CCM wamewacheza [played you], hamna budi kujaribu mbinu nyinginezo katika harakati zenu za kuleta mabadiliko ya kisiasa.

Civil disobedience na passive resistance.

Hamasisheni watu waanze kugomea matendo ya serikali ya CCM.

Mifano:

1. Msishiriki kabisa chaguzi zozote zile zilizopangwa kufanyika chini ya mazingira yaliyopo hivi sasa. Wahamasisheni na watu waache kushiriki. Wahamasisheni waache kujiandikisha kupiga kura. Pia, vishawishini na vyama vingine vya upinzani visishiriki kabisa katika chaguzi zozote zile.

2. Washawishini wananchi waache kujitokeza kwenye sherehe zozote zile zilizoandaliwa na serikali.

3. Washawishini wananchi waache kujitokeza kwa wingi sehemu ambazo viongozi wa CCM wanakuwepo. Mfano, kama Rais ana ratiba ya kwenda kufungua mradi sehemu, wananchi wasiende. Wamwache rais na maCCM wenzake washiriki peke yao.

4. Natamani sana waajiriwa wote wa serikali kufanya migomo inayolenga kuipa shinikizo serikali ya CCM ili yapatikane mabadiliko ya kweli ya kisiasa.

Mbinu zingine mtachangia na wengine. Ila ni lazima ziwepo kwenye wigo wa civil disobedience na passive resistance.

Natambua kwamba kuyatimiza yote hayo si kazi rahisi, hususan kwenye hii jamii yetu ambayo imejaa uoga wa kupitiliza.

İli yote hayo yatimie, ni lazima wengi wetu tuwe on-code. Bila ya kuwa codified, hakuna kitakachotimia.

Kwa wale waliopo Marekani, nawatakia siku njema ya mapumziko ya sikukuu ya MLK Jr. hapo kesho Jumatatu tarehe 16.

Binafsi ninamkubali sana MLK Jr. He was super brilliant.

MLK day ndo imenipa hamasa ya kufungua mjadala huu kwa sababu Dr. King na wenzake walitumia hizo mbinu za civil disobedience na passive resistance katika kuishinikiza serikali ya Marekani kuufuta ubaguzi wa rangi wa kitaasisi [institutional racism].

Mwamko huo wa kuipa shinikizo serikali ya Marekani ulichochewa na mwanamama Rosa Parks ambaye siku moja anatoka kazini akiwa amechoka, alikataa kuachia siti yake kwenye basi ili kumpisha mzungu akae kama ambavyo sheria ilivyokuwa inasema.

Kukataa kwake huko ndo kukazaa Montgomery Bus Boycott iliyodumu kwa mwaka mzima. Mgomo huo pia ndo uliomweka Dr. King kwenye chati za uanaharakati na mengineyo yaliyobaki yakawa ni historia.

Mgomo huo pia ulipelekea mahakama ya upeo ya Marekani [US Supreme Court] kutoa uamuzi kuwa sheria za jimbo la Alabama na za mji wa Montgomery zilikuwa zinaenda kinyume na katiba ya nchi.

Pata picha endapo watu wanagoma kupanda ndege za ATCL. Wanagoma kupanda mwendokasi, n.k., mwisho wa siku serikali haitakuwa na jinsi zaidi ya kuwasikiliza watu kwa umaanani.

Najua kuandika tu na kutoa mawazo huku umekaa nyumbani kwenye kiti chako ni rahisi zaidi kuliko kutenda.

Lakini pia, hakuna tendo la kibinadamu linalotokea tu bila kuanza kama fikra kichwani.

Katika jitihada za kuleta mabadiliko nchini, ni lazima kujaribu mbinu mbalimbali.

Civil disobedience na passive resistance ni mbinu ambazo zimeleta mabadiliko sehemu nyingi tu hapa duniani.

Na kama huko kwingine mafanikio yalipatikana, basi naamini hata hapa Tanzania inawezekana pia.

CHADEMA, NCCR, and others, add this arrow in your quiver. It works.
 
Watanzania siyo wajinga kama unavyofikiria wewe kwa mawazo ya kijinga na yasiyo na mantiki wala mashiko. Ni nani na mtanzania yupi mwenye akili timamu na anayejitambua na anayefahamu na kutambua historia ya CHADEMA,matendo ya viongozi wa CHADEMA na kukosa kwao uzalendo kwa Taifa letu? Watanzania kwa mamilioni yao wanafahamu kuwa viongozi wa CHADEMA siku zote wamekuwa wakipigania maslahi yao.siki zote wamekuwa waumini wa kutafuta upenyo wa sheria au kanuni au mazingira yatakayowawezesha kupata nafasi za uongozi hasa ubunge ili wakapata pesa za kushibisha matumbo yao. Ni wapi katika muda wote umewahi kusikia viongozi wa CHADEMA wakikataa posho wakiwa bungeni au kusema wanaitisha maandamano ya kupinga posho za wabunge kipindi chote walipokuwa bungeni?

Kwanini hatujawahi kuona CHADEMA wakipinga kiinua mgongo kwa wabunge kisicho na kikokotoo kama ilivyo kwa watumishi wengine kama walimu na maaskari? CHADEMA hawajawahi kufanya haya kwa kuwa yalikuwa yanawanufaisha na kuwapa shibe ya matumbo yao na kutunisha akaunti zao kama ambavyo akina sugu wamekuwa wakijitapa kuwa na fedha nyingi kwenye akaunti zao benki.

Watanzania hawawezi kushiriki wala kuunga mkono huo ujinga uliouopendekeza kwa sababu CHADEMA hawana usafi wa kuwashawishi watanzania kufanya hayo. Watanzania wanaaelewa dhamira njema ya Rais wao na serikali yao katika kuwainua kiuchumi.wameona na kujionea namna ambavyo miradi mbalimbali imetekelezwa hapa nchini na kuwasogezea huduma karibu yao Watanzania wameona namna mabilioni ya fedha yalivyoelekezwa katika miradi mbalimbali iliyogusa maisha yao na kuleta matokeo bora na chanya.watanzania wanajionea namna Rais wao na serikali yao inavyopambana usiku na mchana kuboresha maisha yao kwa kuelekeza kila senti inayokusanywa katika shughuli zinazozalisha fursa mbalimbali za kiuchumi ikiwepo ajira kwa vijana,kuongezeka kwa mapato, kuchochea biashara na uwekezaji, kuongezeka kwa mzunguko wa pesa mitaani na mengine mengi tu.
 
Watanzania siyo wajinga kama unavyofikiria wewe kwa mawazo ya kijinga na yasiyo na mantiki wala mashiko. Ni nani na mtanzania yupi mwenye akili timamu na anayejitambua na anayefahamu na kutambua historia ya CHADEMA,matendo ya viongozi wa CHADEMA na kukosa kwao uzalendo kwa Taifa letu? Watanzania kwa mamilioni yao wanafahamu kuwa viongozi wa CHADEMA siku zote wamekuwa wakipigania maslahi yao.siki zote wamekuwa waumini wa kutafuta upenyo wa sheria au kanuni au mazingira yatakayowawezesha kupata nafasi za uongozi hasa ubunge ili wakapata pesa za kushibisha matumbo yao. Ni wapi katika muda wote umewahi kusikia viongozi wa CHADEMA wakikataa posho wakiwa bungeni au kusema wanaitisha maandamano ya kupinga posho za wabunge kipindi chote walipokuwa bungeni?

Kwanini hatujawahi kuona CHADEMA wakipinga kiinua mgongo kwa wabunge kisicho na kikokotoo kama ilivyo kwa watumishi wengine kama walimu na maaskari? CHADEMA hawajawahi kufanya haya kwa kuwa yalikuwa yanawanufaisha na kuwapa shibe ya matumbo yao na kutunisha akaunti zao kama ambavyo akina sugu wamekuwa wakijitapa kuwa na fedha nyingi kwenye akaunti zao benki.

Watanzania hawawezi kushiriki wala kuunga mkono huo ujinga uliouopendekeza kwa sababu CHADEMA hawana usafi wa kuwashawishi watanzania kufanya hayo. Watanzania wanaaelewa dhamira njema ya Rais wao na serikali yao katika kuwainua kiuchumi.wameona na kujionea namna ambavyo miradi mbalimbali imetekelezwa hapa nchini na kuwasogezea huduma karibu yao Watanzania wameona namna mabilioni ya fedha yalivyoelekezwa katika miradi mbalimbali iliyogusa maisha yao na kuleta matokeo bora na chanya.watanzania wanajionea namna Rais wao na serikali yao inavyopambana usiku na mchana kuboresha maisha yao kwa kuelekeza kila senti inayokusanywa katika shughuli zinazozalisha fursa mbalimbali za kiuchumi ikiwepo ajira kwa vijana,kuongezeka kwa mapato, kuchochea biashara na uwekezaji, kuongezeka kwa mzunguko wa pesa mitaani na mengine mengi tu.
Watanzania wengi ni wajinga kupita kiasi.
 
Tukianza na kugomea chaguzi zote, itakuwa ni mwanzo mzuri sana.
Gomea wewe na wajinga wenzio lakini nchi itakwenda na mambo yatasonga kama kawaida tu.watanzania wanajionea juhudi,uchapa kazi na ufanisi wa serikali yao katika kuwaletea maendeleo na kuweka mazingira wezeshi kwa kila mtu kuweza kutimiza ndoto zake. Hakuna maendeleo yatakayokuja kwako ikiwa hutakunjua mikono yako na kufanya kazi kwa bidii, juhudi na maarifa na kujituma kwa nguvu zako zote.kazi ya serikali ni kuweka mazingira wezeshi kama ambavyo imekuwa ikifanya kwa sasa ,.jambo ambalo limepelekea Watanzania wengi kuiunga mkono serikali yao.
 
Watanzania wengi ni wajinga kupita kiasi.
Wewe ndiye mjinga usiyejitambua . Lakini Watanzania wanajielewa na ndio maana hawawezi kuunga ujinga huo ulioupendekeza. Mtanzania gani aunge mkono mawazo ya kijinga kama hayo na yale yaliyotolewa na CHADEMA wakati anajuwa ni wasaka tonge na walafi wa madaraka? Nani aunge mkono ujinga wa CHADEMA wa kutaka kwa kila jimbo kuwe na wabunge wawili?
 
Namba 2 na 3 tayari , wengine unaowaona ni Chawa au wale watu wa misiba wanaojiita Mama ongea na Mwanao
Acha kujipa ukipofu wa akili na macho wewe. Watanzania wana imani kubwa na serikali yao ya CCM pamoja na viongozi wake.wataendelea kumiminika na kufurika kwa wingi katika mikutano na sherehe mbalimbali.hii ni kutokana na imani kubwa waliyonayo kwa Mheshimiwa Rais na serikali yake pamoja na chama cha Mapinduzi.hii inachagizwa na kuchochewa na kazi kubwa iliyofanywa na serikali katika kuwaletea maendeleo wananchi.watanzania wanaona namna serikali yao inavyowekeza mabilioni ya pesa katika miradi mbalimbali ya kimkakati na kiuchumi inayotoa na kuleta fursa mbalimbali.

Watanzania wanaona namna hali ya uchumi inavyoendelea kuimarika na kumgusa kila mtanzania.watu wanajionea mzunguko wa pesa mitaani ulivyo wenye afya na kuleta matumaini. Kikubwa ni wewe kufanya kazi na kujituma kwa nguvu zako zote na siyo kusubiri kuletewa kila kitu mezani pako huku wewe ukipiga porojo mitaani.
 
Huwezi ku negotiate na CCM hii mezani with smiling faces na vikombe vya kahawa ukafanikiwa! Kama Chadema wameamua wasirudi nyuma na wa mobilise wapenda mageuzi wote bila kujali tofauti za huko nyuma.

Mizizi ya CCM ni mizito kuikata kwa maneno maneno bila hatua kali za kisiasa.
Hukuna na hayupo wa kuwaungeni mkono maana ninyi mnachopigania ni maslahi yenu .mnachotaka ninyi ni upana wa njia itakayowawezesha kupata udiwani na ubunge na siyo maslahi ya wananchi.ninyi ni mafisi tu mnaotoka mate mdomoni kwa ajili ya kuvizia uongozi tu. Hamna uchungu wala kuguswa na maisha ya watanzania.ndio maana kwa ulafi wenu mmeona mpendekeze kuwe na wabunge wawili katika kila jimbo ili muwe na uhakika wa kupata chochote kile mkononi mwenu. Ninyi ni matapeli tu wa kisiasa.
 
Umetoa ushauri mzuri sana ! Chadema watangaze kutoshiriki chochote kinacho wapa meleage CCM …
Kuanzia kutoshiriki uchaguzi na chaguzi zote…. Na hata kuwahamsha watanzania wasusie kushangilia mambo ya tumu ya taifa na hata zoezi zima la kujiandikisha kupiga kura na hata kupiga kura…wahakikishe watanzania wanagomea kabisa chaguzi zote na hawqjitokezi
 
Tukianza na kugomea chaguzi zote, itakuwa ni mwanzo mzuri sana.
Naunga mkono hoja

Kushiriki katika chaguzi ambazo sheria zake hazina maana ni kuwahadaa wananchi hata kama wewe ni chama cha upinzani

Na hii inawahisu Chadema na ACT,hawa wanaonekana wanafiki kwasababu wanajua kabisa kwamba sheria zilizopo zinawanyima ushindi kwa asilima 100 lakini bado wanashiriki kila mwaka.

Hii kwa kiasi kikubwa imefanya wananchi wavione vyama hivi vya upinzani viko kwa maslahi yao binafsi na si kwa ajili ya kutetea masilahi mapana ya taifa
 
Huwezi ku negotiate na CCM hii mezani with smiling faces na vikombe vya kahawa ukafanikiwa! Kama Chadema wameamua wasirudi nyuma na wa mobilise wapenda mageuzi wote bila kujali tofauti za huko nyuma.

Mizizi ya CCM ni mizito kuikata kwa maneno maneno bila hatua kali za kisiasa.
Ccm imeshakuwa mhimili wa 4 wa nchi, tena wenye mamlaka kuliko mihimili yote.

Katiba mpya pekee ndiye itakayoweza kusawazisha hilo.
 
Watanzania siyo wajinga kama unavyofikiria wewe kwa mawazo ya kijinga na yasiyo na mantiki wala mashiko. Ni nani na mtanzania yupi mwenye akili timamu na anayejitambua na anayefahamu na kutambua historia ya CHADEMA,matendo ya viongozi wa CHADEMA na kukosa kwao uzalendo kwa Taifa letu? Watanzania kwa mamilioni yao wanafahamu kuwa viongozi wa CHADEMA siku zote wamekuwa wakipigania maslahi yao.siki zote wamekuwa waumini wa kutafuta upenyo wa sheria au kanuni au mazingira yatakayowawezesha kupata nafasi za uongozi hasa ubunge ili wakapata pesa za kushibisha matumbo yao. Ni wapi katika muda wote umewahi kusikia viongozi wa CHADEMA wakikataa posho wakiwa bungeni au kusema wanaitisha maandamano ya kupinga posho za wabunge kipindi chote walipokuwa bungeni?

Kwanini hatujawahi kuona CHADEMA wakipinga kiinua mgongo kwa wabunge kisicho na kikokotoo kama ilivyo kwa watumishi wengine kama walimu na maaskari? CHADEMA hawajawahi kufanya haya kwa kuwa yalikuwa yanawanufaisha na kuwapa shibe ya matumbo yao na kutunisha akaunti zao kama ambavyo akina sugu wamekuwa wakijitapa kuwa na fedha nyingi kwenye akaunti zao benki.

Watanzania hawawezi kushiriki wala kuunga mkono huo ujinga uliouopendekeza kwa sababu CHADEMA hawana usafi wa kuwashawishi watanzania kufanya hayo. Watanzania wanaaelewa dhamira njema ya Rais wao na serikali yao katika kuwainua kiuchumi.wameona na kujionea namna ambavyo miradi mbalimbali imetekelezwa hapa nchini na kuwasogezea huduma karibu yao Watanzania wameona namna mabilioni ya fedha yalivyoelekezwa katika miradi mbalimbali iliyogusa maisha yao na kuleta matokeo bora na chanya.watanzania wanajionea namna Rais wao na serikali yao inavyopambana usiku na mchana kuboresha maisha yao kwa kuelekeza kila senti inayokusanywa katika shughuli zinazozalisha fursa mbalimbali za kiuchumi ikiwepo ajira kwa vijana,kuongezeka kwa mapato, kuchochea biashara na uwekezaji, kuongezeka kwa mzunguko wa pesa mitaani na mengine mengi tu.
Utakuta wewe naye ni baba wa familia.
Ujinga na unafiki uliopitiliza bado ni tatizo kubwa Tanzania
 
Ili uamini kwamba watanzania wengi ni wajinga na wanafiki unaona kabisa waliokomenti hapo juu wengi wamegeuza hoja kutoka kutetea maslahi ya nchi kama alivyoileta mleta mada kuwa uzi wa kuwasema CHADEMA

Kama nimeelewa vizuri sijaona popote pale ambapo mleta mada amesema hayo mambo aliyoshauri wafanye CHADEMA pekee.
 
Naunga mkono hoja

Kushiriki katika chaguzi ambazo sheria zake hazina maana ni kuwahadaa wananchi hata kama wewe ni chama cha upinzani

Na hii inawahisu Chadema na ACT,hawa wanaonekana wanafiki kwasababu wanajua kabisa kwamba sheria zilizopo zinawanyima ushindi kwa asilima 100 lakini bado wanashiriki kila mwaka.

Hii kwa kiasi kikubwa imefanya wananchi wavione vyama hivi vya upinzani viko kwa maslahi yao binafsi na si kwa ajili ya kutetea masilahi mapana ya taifa
CHADEMA wakishiriki tena chaguzi zozote kuanzia sasa kwenda mbele bila mabadiliko ya katiba na tume mpya huru ya uchaguzi, nitawaengua kabisa.
 
Back
Top Bottom