Habari wana jamvi,
Nasikitika kusema watanzania walio wengi japo sio wote watakuwa wamelogwa na wala sio bure. Sasa naona hakuna cha wasomi wala wasio wasomi wenyekufikiri wapi tulipo na wapi tunatakiwa kwenda.
Wengi humu wanajifanya wachambuzi wa siasa wazuri kumbe ni washabiki na wenye chuki mioyoni mwao.
Nije kwenye hoja, Zitto Kabwe ni mbunge ambaye mara nyingi huibua na kujenga hoja zenye manufaa kwa watanzania, na ni mbunge wa mfano anayeisimamia na kuikosoa serikali naona kuliko hata wabunge wanaosifiwa kuwa ni wazalendo. Sasa kwanini watu wasichangie mawazo kwenye hoja hizi na kutoa ushauri kipi kifanyike ili twende mbele tunapopahitaji?
Mi nashangaa mtu mwenye akili timamu anaanza kumchambua zitto ni nani, na nijinsi gani alivyo msaliti na isitoshe anashauri jinsi ya kumpoteza kisiasa, sasa hapo mwananchi wa kawaida atafaidika nini?
Jamani siku zote wale mnaoendelea kutuhumu usaliti wa zitto kuwa katumika na ccm mbona sijaona ushahidi kamili? Watu mmejengwa kwa hisia? Ndani ya makosa 11 aliyotuhumiwa na chama mbona hakuna walipoonyesha kapokea hela kutoka ccm? Kwanini msimtuhumu kwa ule waraka tu wenye ushahidi?
Je na waliomtuhu nao sio binadamu wanaoweza kukosea na wakawa wana chuki zao?
Analeta hoja bungeni chama kinamnyima ushirikiano kama ilivyokuwa kipindi cha dr. Slaa, utegemee hoja itafika mwisho?
Hata kama anamaovu ni binadamu kama wengine ila hoja zake nzuri tuzipe uzito na ushikiano tusonge mbele. Tuache chuki za kijinga, tunalumbana wenyewe huku ccm wakiendelea kutafuna nguvu zetu.
Nasikitika kusema watanzania walio wengi japo sio wote watakuwa wamelogwa na wala sio bure. Sasa naona hakuna cha wasomi wala wasio wasomi wenyekufikiri wapi tulipo na wapi tunatakiwa kwenda.
Wengi humu wanajifanya wachambuzi wa siasa wazuri kumbe ni washabiki na wenye chuki mioyoni mwao.
Nije kwenye hoja, Zitto Kabwe ni mbunge ambaye mara nyingi huibua na kujenga hoja zenye manufaa kwa watanzania, na ni mbunge wa mfano anayeisimamia na kuikosoa serikali naona kuliko hata wabunge wanaosifiwa kuwa ni wazalendo. Sasa kwanini watu wasichangie mawazo kwenye hoja hizi na kutoa ushauri kipi kifanyike ili twende mbele tunapopahitaji?
Mi nashangaa mtu mwenye akili timamu anaanza kumchambua zitto ni nani, na nijinsi gani alivyo msaliti na isitoshe anashauri jinsi ya kumpoteza kisiasa, sasa hapo mwananchi wa kawaida atafaidika nini?
Jamani siku zote wale mnaoendelea kutuhumu usaliti wa zitto kuwa katumika na ccm mbona sijaona ushahidi kamili? Watu mmejengwa kwa hisia? Ndani ya makosa 11 aliyotuhumiwa na chama mbona hakuna walipoonyesha kapokea hela kutoka ccm? Kwanini msimtuhumu kwa ule waraka tu wenye ushahidi?
Je na waliomtuhu nao sio binadamu wanaoweza kukosea na wakawa wana chuki zao?
Analeta hoja bungeni chama kinamnyima ushirikiano kama ilivyokuwa kipindi cha dr. Slaa, utegemee hoja itafika mwisho?
Hata kama anamaovu ni binadamu kama wengine ila hoja zake nzuri tuzipe uzito na ushikiano tusonge mbele. Tuache chuki za kijinga, tunalumbana wenyewe huku ccm wakiendelea kutafuna nguvu zetu.