Usalama wa watoto wakati wa mvua wakiwa shule za serikali ni mdogo sana

Usalama wa watoto wakati wa mvua wakiwa shule za serikali ni mdogo sana

Think2

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2025
Posts
2,193
Reaction score
3,957
Habari zenu ,it's my again

Ndugu zangu kama una mtoto au watoto wanasoma shule hizi kayumba usalama wao wakati wa mvua ni mchache sana radi zinapiga kila pahala , nimeona habari hapa Dar Kivule watoto wamepigwa radi . Hivi walimu wanaruhusu watoto watoke nje wakati mvua ikinyesha ?

Walimu wanajifungia staff wanaacha watoto wadogo wanakimbia kimbia nje au kwasababu sio watoto wao hawana uchungu mzazi unapokeaje taarifa ya kifo cha mwanao kapigwa radi akicheza shule wakati wa mvua ni uchungu.

Wazazi mvua ukiona dalili za mvua kimbilia mtoto wako

Mwisho, huu ni uzembe wa walimu unapelekea kifo cha watoto

----
Wanafunzi watatu wa Shule ya Msingi Msongola, iliyopo Kivule wilayani Ilala jijini Dar es Salaam, wamefariki dunia kutokana na kupigwa na radi.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amethibitisha tukio hilo na amesema tukio hilo limetokea leo Jumatano Machi 18, 2026.

“Ni kweli wanafunzi wetu watano walikuwa wakicheza shuleni wamepigwa na radi watatu wakafariki papo hapo, hawa wengine wanaendeleana matibabu,” amesema Muliro huku akiongeza kuwa wanafunzi wawili wamekimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu.

Chanzo: Mwananchi
 
Nafikiri ni watoto 3 waliopigwa radi mpaka kupelekea umauti wao.
Muda ule mvua inanyesha&radi ulikuwa ni wakati wa mapumziko na watoto walikuwa nje,hapo unawalaumu bure walimu.
Kama umesomesha shule zetu za msingi wakati wa mapumziko ni ngumu sana kuwarudisha watoto darasani
 
Nafikiri ni watoto 3 waliopigwa radi mpaka kupelekea umauti wao.
Muda ule mvua inanyesha&radi ulikuwa ni wakati wa mapumziko na watoto walikuwa nje,hapo unawalaumu bure walimu
Uzembe hao waalimu hawakuona dalili za mvua mapema?
 
Habari zenu ,it's my again
Ndugu zangu kama una mtoto au watoto wanasoma shule hizi kayumba usalama wao wakati wa mvua ni mchache sana radi zinapiga kila pahala , nimeona habari hapa dar kivule watoto wamepigwa radi . Ivi waalimu wanaruhusu watoto watoke nje wakati mvua ikinyesha ?
Waalimu wanajifungia staff wanaacha watoto wadogo wanakimbia kimbia nje au kwasababu sio watoto wao hawana uchungu mzazi unapokeaje taarifa ya kifo cha mwanao kapigwa radi akicheza shule wakati wa mvua ni uchungu.

Wazazi mvua ukiona dalili za mvua kimbilia mtoto wako

Mwisho, huu ni uzembe wa waalimu unapelekea kifo cha watoto
Very Tragedy ! Walimu ujumbe uwafikie.
 
Yaani wewe umeng'ang'ana na walimu tu hadi wapatikane na makosa. Kwanza ungeuuliza je, shule ina vikinga radi halafu ndipo tuje kwenye hoja zingine. Unaambiwa walikuwa kwenye muda wa mapumziko, sasa hapo kosa la walimu ni lipi? Je, kuna walimu wa kutosha katika hiyo shule?
 
Yaani wewe umeng'ang'ana na walimu tu hadi wapatikane na makosa. Kwanza ungeuuliza je, shule ina vikinga radi halafu ndipo tuje kwenye hoja zingine. Unaambiwa walikuwa kwenye muda wa mapumziko, sasa hapo kosa la walimu ni lipi? Je, kuna walimu wa kutosha katika hiyo shule?
Hatua zichukuliwe hao waalimu wazembe sana hakuna kona kona
 
Ni sahihi kudai uwajibikaji na viwango bora vya usalama shuleni, lakini madai ya uzembe lazima yajengwe juu ya ushahidi, si hisia.

Njia sahihi ni kuitaka mamlaka husika kufanya uchunguzi wa kina na kuweka miongozo madhubuti ya usalama wakati wa hali ya hewa hatarishi.

Si sahihi kutoa hukumu ya jumla kuwa “walimu ni wazembe” bila uchunguzi maalum wa tukio husika.

Radi ni tukio la kiasili lisilotabirika kwa uhakika (act of God), na kisheria, si kila madhara yanayotokana na tukio la asili yanabebeshwa lawama taasisi au mtu, isipokuwa pale ambapo tahadhari zinazotarajiwa hazikuchukuliwa.
 
Back
Top Bottom