Usalama wa Taifa Someni hapa!

Status
Not open for further replies.

GAZETI

JF-Expert Member
Feb 24, 2011
5,278
6,673
Sijui kama ni watu mnaoshaurika, ingawa nafahamu wazi kuwa tunakuwa pamoja katika majukwaa mbalimbali.

Ndani ya nchi yetu kuna tishio la Al- Shababb.

Ninachokiona hapa ni kuwa tishio litakuwa kubwa zaidi iwapo mpango wa Odinga kuomba msaada wa Kijeshi kwa Israel utafanikiwa. Kuingia kwa Waisrael ndani ya Somalia eti kwa Lengo la kuwasaidia wakenya kitakuwa kivutio kwa maadui mbalimbali wa Israel ambao ni wengi sana na ni suala linalofahamika. Hiyo itakuwa ni moja ya sababu za kuiingiza nchi yetu kwenye machafuko hayo ambayo tusipokuwa makini yatasambaa A.Mashariki.

Tunachotakiwa kufanya ni kutokubali kabisa kujiingiza kwenye mzozo huo ambao tusipozingatia utatuingiza kwenye machafuko ambayo yatazidi kuharibu uchumi
wetu ambao tayari yamekwishaharibika pia ule wimbo wa Nchi yenye AMANI hautaimbwa tena.

WASIWASI WANGU
Kuna uwezekano mkubwa Mataifa ya Magharibi (Hususani Marekani) au Israel, wakalipua moja katika maeneo ya nchi yetu na kuwasingizia AL Shabab ili wapate kisingizio cha kuiingiza Tanzania kwenye mgogoro huo wa aina yake

USHAURI WANGU
Nafikiri ni wakati muafaka sasa kwa Idara kuunda kitengo maalum ambacho kitakuwa na kazi maalum ya kutafakari kwa kina jambo lolote linalotokea namna ya kuliendea n.k Kitengo hicho kiwe na watu wenye uwezo nzuri wa kufikiri na kushauri juu ya masuala nyeti ya nchi na si kuwaachia wanasiasa waamue wanavyotaka.

Mwambieni ndugu A.C aunde special department ya watu wenye akili ambao wataweza kutushauri pale Wamarekani na mataifa mengine korofi wanapotaka kuturubuni kwa jambo lolote.

GAZETI (P.I)
 
Naunga mkono hoja!

Niemeona vitu viwili hapa ... Ulinzi ni zaidi ya AKILI (Ulinzi wa Taifa Kiakili) na Ulinzi ni UTU na HEKIMA pia! (Ulinzi wa Taifa Ki Utu na Ki hekima)
 
Wazo zuri sana. Lakini kama hujagundua tatizo la taifa letu ni kutofuata ushauri wa kitaalam. Itaundwa tume, na kuja na mawazo mazuri tu. Mwisho wa siku wahusika watajifanyia madudu yao!
 
ni kweli kabisa!marekani wanaenda uganda na israel wanaenda kenya hao wote wauaji wakubwa tena wanaua kwa ndege zisizo na rubani.tanzania tunahitaji busara sana ktk kukabiliana nao
 
alshababu na maharamia wengine ni maadui na magaidi na wanapaswa kudhibitiwa at any cost.kama tulipeleka majeshi msumbiji kumsaidia rafiki sioni kwanini tusiwasaidie wana EAC wenzetu.maharamia hawa wanateka meli zenye madawa huwezi ukasema tuwaache eti kwa kuogopa mashambulizi ya mabomu.majangili wa kisomali waliwahi kutusumbua huko ngorongoro na jeshi letu liliweza kuwadhibiti tupunguze uwoga.
 
Nafikiri wewe ndio umegoma kuushirikisha ubongo wako, hatuhitaji kitengo maalum kwa hili kwani misikiti yote ambayo ni maficho ya Al shabaab inajulikani na tumeshairipoti na tumeweka thread hapa kuitaja wazi wazi misikiti hiyo kwa majina, kwahiyo sahau hilo unalopendekeza, usidhani Usalama wa Taifa hawafanyi kazi, wanafanya kazi sana hila tatizo pale magogoni hawashauriki.
 
alshababu na maharamia wengine ni maadui na magaidi na wanapaswa kudhibitiwa at any cost.kama tulipeleka majeshi msumbiji kumsaidia rafiki sioni kwanini tusiwasaidie wana EAC wenzetu.maharamia hawa wanateka meli zenye madawa huwezi ukasema tuwaache eti kwa kuogopa mashambulizi ya mabomu.majangili wa kisomali waliwahi kutusumbua huko ngorongoro na jeshi letu liliweza kuwadhibiti tupunguze uwoga.

kama ni sisi wenyewe tutajilinda sawa lakini si usa au israel watusaidie
 
Nafikiri wewe ndio umegoma kuushirikisha ubongo wako, hatuhitaji kitengo maalum kwa hili kwani misikiti yote ambayo ni maficho ya Al shabaab inajulikani na tumeshairipoti na tumeweka thread hapa kuitaja wazi wazi misikiti hiyo kwa majina, kwahiyo sahau hilo unalopendekeza, usidhani Usalama wa Taifa hawafanyi kazi, wanafanya kazi sana hila tatizo pale magogoni hawashauriki.

kutoshaurika kwa magogoni hilo liko wazi kabisa.
 
Sijui kama ni watu mnaoshaurika, ingawa nafahamu wazi kuwa tunakuwa pamoja katika majukwaa mbalimbali.

Ndani ya nchi yetu kuna tishio la Al- Shababb.

Ninachokiona hapa ni kuwa tishio litakuwa kubwa zaidi iwapo mpango wa Odinga kuomba msaada wa Kijeshi kwa Israel utafanikiwa. Kuingia kwa Waisrael ndani ya Somalia eti kwa Lengo la kuwasaidia wakenya kitakuwa kivutio kwa maadui mbalimbali wa Israel ambao ni wengi sana na ni suala linalofahamika. Hiyo itakuwa ni moja ya sababu za kuiingiza nchi yetu kwenye machafuko hayo ambayo tusipokuwa makini yatasambaa A.Mashariki.

Tunachotakiwa kufanya ni kutokubali kabisa kujiingiza kwenye mzozo huo ambao tusipozingatia utatuingiza kwenye machafuko ambayo yatazidi kuharibu uchumi
wetu ambao tayari yamekwishaharibika pia ule wimbo wa Nchi yenye AMANI hautaimbwa tena.

WASIWASI WANGU
Kuna uwezekano mkubwa Mataifa ya Magharibi (Hususani Marekani) au Israel, wakalipua moja katika maeneo ya nchi yetu na kuwasingizia AL Shabab ili wapate kisingizio cha kuiingiza Tanzania kwenye mgogoro huo wa aina yake

USHAURI WANGU
Nafikiri ni wakati muafaka sasa kwa Idara kuunda kitengo maalum ambacho kitakuwa na kazi maalum ya kutafakari kwa kina jambo lolote linalotokea namna ya kuliendea n.k Kitengo hicho kiwe na watu wenye uwezo nzuri wa kufikiri na kushauri juu ya masuala nyeti ya nchi na si kuwaachia wanasiasa waamue wanavyotaka.

Mwambieni ndugu A.C aunde special department ya watu wenye akili ambao wataweza kutushauri pale Wamarekani na mataifa mengine korofi wanapotaka kuturubuni kwa jambo lolote.

GAZETI (P.I)

umeona mbali gazeti, lakini kama hatujaweza kutatua migogoro inayofukuta ndani ya nchiyetu kwa sababu ya katiba, sidhani kama hili la kwako litawezekana iwapo watu/mataifa mabaya yataamua kutufanyia kitu kibaya.

Kama viongozi wetu wanashindwa kuanzisha mchakoto huru ndani ya nchi, je nje ya nchi wataanzia wapi?
 
Tumekwisha kwa jinsi walivyokuwa na usongo na sisi hasa baada ya kukataa sera za kimagharibi sijui kama kutakuwa na usalama.
 
Tumekwisha kwa jinsi walivyokuwa na usongo na sisi hasa baada ya kukataa sera za kimagharibi sijui kama kutakuwa na usalama.
Hujui ulisemalo, ni sera gani tulizozikataa? hujui kwamba Uranium yetu tayari ni ya Wamaekani tumebadilishana nao kwa vyandaruwa? na unajifanya hujui kwamba Barrick ni kampuni ya nchi za Magharibi? hujui kinachoendelea kigamboni? na hujui gesi ya songosongo ananufaika nayo nani? na haujui kwamba Richmond sasa ndio inaitwa symbion power na inakula pesa zetu kama kawa?
 
nadhani imefika wakati Tanzania ikachagua upande wa kuwa nao mshirika kati ya pande za magharibi au upande wa mashariki ambao unaongozwa na china na mataifa mengine ya Asia . kuendelea kuwa katika kundi lisilofungamana ni kitu cha kupoteza muda tu
 
alshababu na maharamia wengine ni maadui na magaidi na wanapaswa kudhibitiwa at any cost.kama tulipeleka majeshi msumbiji kumsaidia rafiki sioni kwanini tusiwasaidie wana EAC wenzetu.maharamia hawa wanateka meli zenye madawa huwezi ukasema tuwaache eti kwa kuogopa mashambulizi ya mabomu.majangili wa kisomali waliwahi kutusumbua huko ngorongoro na jeshi letu liliweza kuwadhibiti tupunguze uwoga.

:A S 13::A S 13::A S 13:....................................Napita tu,
 
Mkuu GAZETI. Kwa mtu makini anaposoma hoja yako anagundua wewe siyo kwamba unaipenda sana Tanzania na haupendi ishambuliwe na magaidi wa Al shabab bali wewe una chuki dhidi ya Marekani na Israel.
 
nadhani imefika wakati Tanzania ikachagua upande wa kuwa nao mshirika kati ya pande za magharibi au upande wa mashariki ambao unaongozwa na china na mataifa mengine ya Asia . kuendelea kuwa katika kundi lisilofungamana ni kitu cha kupoteza muda tu

king11 katika dunia hii mataifa karibia yote hayana urafiki wa kudumu. Tena haya makubwa yakiwemo hayo ya mashariki wanaangalia maslahi ya kiuchumi,biashara na wakati fulani ulinzi(kijeshi)
 
Sijui kama ni watu mnaoshaurika, ingawa nafahamu wazi kuwa tunakuwa pamoja katika majukwaa mbalimbali.

Ndani ya nchi yetu kuna tishio la Al- Shababb.

Ninachokiona hapa ni kuwa tishio litakuwa kubwa zaidi iwapo mpango wa Odinga kuomba msaada wa Kijeshi kwa Israel utafanikiwa. Kuingia kwa Waisrael ndani ya Somalia eti kwa Lengo la kuwasaidia wakenya kitakuwa kivutio kwa maadui mbalimbali wa Israel ambao ni wengi sana na ni suala linalofahamika. Hiyo itakuwa ni moja ya sababu za kuiingiza nchi yetu kwenye machafuko hayo ambayo tusipokuwa makini yatasambaa A.Mashariki.

Tunachotakiwa kufanya ni kutokubali kabisa kujiingiza kwenye mzozo huo ambao tusipozingatia utatuingiza kwenye machafuko ambayo yatazidi kuharibu uchumi
wetu ambao tayari yamekwishaharibika pia ule wimbo wa Nchi yenye AMANI hautaimbwa tena.

WASIWASI WANGU
Kuna uwezekano mkubwa Mataifa ya Magharibi (Hususani Marekani) au Israel, wakalipua moja katika maeneo ya nchi yetu na kuwasingizia AL Shabab ili wapate kisingizio cha kuiingiza Tanzania kwenye mgogoro huo wa aina yake

USHAURI WANGU
Nafikiri ni wakati muafaka sasa kwa Idara kuunda kitengo maalum ambacho kitakuwa na kazi maalum ya kutafakari kwa kina jambo lolote linalotokea namna ya kuliendea n.k Kitengo hicho kiwe na watu wenye uwezo nzuri wa kufikiri na kushauri juu ya masuala nyeti ya nchi na si kuwaachia wanasiasa waamue wanavyotaka.

Mwambieni ndugu A.C aunde special department ya watu wenye akili ambao wataweza kutushauri pale Wamarekani na mataifa mengine korofi wanapotaka kuturubuni kwa jambo lolote.

GAZETI (P.I)
Jamhuri ya watu wa Kenya tofauti na JMT (URT) ina uhusiano na mataifa hayo miaka nenda rudi, hivyo tuwaache wafanye kile wanachoona kitanufauisha taifa lao. Nasi tuendeleeni na sera zetu bila kusahau kulinda mipaka yetu kuzuia wahalifu majangili wa kupora maliasili zetu ( kama wanyama pori ) maeneo ambayo tumeonyesha udhaifu mkubwa kama hatuna uwezo wa kudhibiti vitu kama hivi basi ni vyema tukaomba moja ya nchi marafiki zetu yenye uwezo katika hizo nyanja na isiyo na maadui wengi duniani ije itusaidie .
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom