Kuna mzee mmoja ana umri wa miaka 70 hivi. Ni mstaafu wa Idara ya usalama wa Taifa.
Mimi sifahamu vitengo vilivyo ndani ya idara hii, kwahiyo sijui ni kitengo gani ndani ya idara alichokuwa anafanya kazi lakini alikuwa humo.
Alikuwa ni Land lord wangu miaka kama minne iliyopita. Ni mzee lakini anaonekana ana nguvu.
Huyu mzee ni mchawi kupita maelezo. Ni mchawi konkodi.
Nyumba yake ina mauza uza. Usiku watu wanatembea juu ya bati, hulali ndani vurugu na vioja. Nilikuwa naota mandoto ya ajabu ajabu mara makaburi mara majoka.
Wakati mwingine mida ya usiku anatoka anachinja kuku, ama anaita watu wanajadili mambo fulani fulani kama wanateta. Mara unasikia kama kuna mtu anapandisha mapepo?
Baadae "wataalamu" wakanitonya kwamba mzee ni mchawi. Nilihama sikugeuka nyuma wala sikumuaga.
Hivi inawezekanaje watu muhimu wanaoshikilia moyo wa nchi wanakuwa wachawi?
Ama kwenye hiyo idara kuna kitengo cha uchawi?
Hebu
Mshana Jr njoo utupe ufafanuzi hapa...
Mpaka leo nimepigwa na butwaa!!