Sibonike
JF-Expert Member
- Dec 23, 2010
- 17,297
- 18,045
Inaelekea msimu huu kutakuwa na vute nikuvute kuhusu usajili wa mchazaji Mrisho Ngasa.
Maadam yeye anasema kasajili Yanga tu, hapa kuna mambo mawili tu. Ama Ngasa kasaini timu zote mbili au viongozi wa Simba wamefoji usajili wake ili kumkomoa.
Safari hii hili suala lisimalizwe eti kwa kutumia busara. Kama kasaini mara mbili apate adhabu yake ya kufungiwa, lakini kama watu wamefoji usajili wake waadhibiwe. Tena bahati nzuri sasa kuna kamati ya maadili. Suala liende huko wahusika wafungiwe kujihusisha na mpira.
Lolote katika hayo, kuna kosa la jinai. Ama utapeli kwa upande wa Ngasa au viongozi waliofoji usajili wake. Pamoja na kamati ya maadili kufanya kazi yake, sheria zichukue mkondo wake ili upumabvu huu usirudiwe tena katika soka la Tanzania.
Maadam yeye anasema kasajili Yanga tu, hapa kuna mambo mawili tu. Ama Ngasa kasaini timu zote mbili au viongozi wa Simba wamefoji usajili wake ili kumkomoa.
Safari hii hili suala lisimalizwe eti kwa kutumia busara. Kama kasaini mara mbili apate adhabu yake ya kufungiwa, lakini kama watu wamefoji usajili wake waadhibiwe. Tena bahati nzuri sasa kuna kamati ya maadili. Suala liende huko wahusika wafungiwe kujihusisha na mpira.
Lolote katika hayo, kuna kosa la jinai. Ama utapeli kwa upande wa Ngasa au viongozi waliofoji usajili wake. Pamoja na kamati ya maadili kufanya kazi yake, sheria zichukue mkondo wake ili upumabvu huu usirudiwe tena katika soka la Tanzania.