Usahihi wa taarifa toka Nkasi

Usahihi wa taarifa toka Nkasi

Adrian Stepp

R I P
Joined
Jul 1, 2011
Posts
2,764
Reaction score
2,600
Wakuu,

Kuna Uzi umepandishwa jukwaani ukiwa na taarifa kwamba Mkuu wa Wilaya ya Nkasi amewaamuru askari kuwaadhibu wananchi.

Ufafanuzi wa taarifa hiyo ni kama ifuatavyo:

Jana, Wananchi, Mbunge na Mkuu wa Wilaya hiyo Ndg Said Mtanda walikubaliana kufanya kazi ya kujenga zahanati ya kijiji iliyokwama kwa takriban miaka 5 huku wananchi wakitembea umbali wa Km 20 kufuata huduma za afya.

Wakati huo huo kwenye kijiji cha Ntuchi (siku ya jana Jumamosi) kulikuwa na mnada ukiendelea hivyo baadhi ya vijana walitajwa kwenda kunywa pombe kinyume na makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja (Songambele).

Askari wa JKT ambao ni mafundi walikuja kusaidia ujenzi wa zahanati hiyo kwakuwa zana zote ( Mbao, bati, misumari) kwa miaka miwili vimekuwa vikioza.

Vijana waliokuwa wamekwenda mnadani walifuatwa wakaletwa ili kushiriki zoezi hilo (songambele).

Askari waliwaleta wananchi ili kufanikisha zoezi hilo na waliokaidi walirushwa kichura chura!

Wananchi kwa pamoja wamefurahi kwakuwa kazi iliyopangwa imefanyika.

Mpaka kufikia muda huu ( Leo jumapili 13, August) wananchi wameendelea kujitokeza kwa wingi kuendelea kushiriki zoezi hill.

Hakuna wanajeshi waliokuja kushiriki Bali ni service men waliojitokeza kujenga zahati kwa kushirikiana na wananchi.

Pia askari hao hao (service men) walishiriki shughuli za maendeleo katika kijiji cha Kasu.

Mtoa taarifa aliyejitanabaisha kama mwanahabari anapaswa kufuata misingi na weledi wa taaluma ya habari.

Ofisi ya mkuu wa wilaya Nkasi imesikitishwa na taarifa zilizotolewa mtandaoni za upotoshwaji!
 
Wakuu,

Kuna Uzi umepandishwa jukwaani ukiwa na taarifa kwamba Mkuu wa Wilaya ya Nkasi amewaamuru askari kuwaadhibu wananchi.

Ufafanuzi wa taarifa hiyo ni kama ifuatavyo:

Jana, Wananchi, Mbunge na Mkuu wa Wilaya hiyo Ndg Said Mtanda walikubaliana kufanya kazi ya kujenga zahanati ya kijiji iliyokwama kwa takriban miaka 5 huku wananchi wakitembea umbali wa Km 20 kufuata huduma za afya.

Wakati huo huo kwenye kijiji cha Ntuchi (siku ya jana Jumamosi) kulikuwa na mnada ukiendelea hivyo baadhi ya vijana walitajwa kwenda kunywa pombe kinyume na makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja (Songambele).

Askari wa JKT ambao ni mafundi walikuja kusaidia ujenzi wa zahanati hiyo kwakuwa zana zote ( Mbao, bati, misumari) kwa miaka miwili vimekuwa vikioza.

Vijana waliokuwa wamekwenda mnadani walifuatwa wakaletwa ili kushiriki zoezi hilo (songambele).

Askari waliwaleta wananchi ili kufanikisha zoezi hilo na waliokaidi walirushwa kichura chura!

Wananchi kwa pamoja wamefurahi kwakuwa kazi iliyopangwa imefanyika.

Mpaka kufikia muda huu ( Leo jumapili 13, August) wananchi wameendelea kujitokeza kwa wingi kuendelea kushiriki zoezi hill.

Hakuna wanajeshi waliokuja kushiriki Bali ni service men waliojitokeza kujenga zahati kwa kushirikiana na wananchi.

Pia askari hao hao (service men) walishiriki shughuli za maendeleo katika kijiji cha Kasu.

Mtoa taarifa aliyejitanabaisha kama mwanahabari anapaswa kufuata misingi na weledi wa taaluma ya habari.

Ofisi ya mkuu wa wilaya Nkasi imesikitishwa na taarifa zilizotolewa mtandaoni za upotoshwaji!
Safi sana.
Mleta mada umefafanua vizuri sana.
Waaibike na walegee.
 
Sasa wewe mleta ufafanuzi hapa ndio umeharibu kabisa. Yaani una kiri kulikuwa na kulazimishwa na kuteswa kwenda kujenga hicho kituo, lakini ukaharibu kwa kuleta ushabiki wa kumtetea mkuu wa wilaya kishamba. Kwa mfano...

1/Yaani taarifa nzima imejichanganya. Mara vijana wamekwenda kunywa pombe, mara watu wamechukuliwa Gulioni, mara Askari (service men!), Mara hawajapigwa lakini wamerushwa vichura chura nk. Ni mchanganyiko kuliko usahihisho.

2/Mleta ufafanuzi hapa husemi wewe ni nani katika ufafanuzi huu. Wewe ni mkuu wa wilaya hiyo? Wewe ni msemaji wake? Wewe ni shuhuda? Wewe ni mleta mada tu lakini una source?

3/Taarifa hii ya ufafanuzi imetolewa na upande wa mkuu wa wilaya ambayo ndio inayodaiwa kutesa watu. Nini maana ya story kuwa balanced?

4/Kama shughuli ilikuwa ni ya kujitolea, kwanini watu wasakwe, warushwe rushwe kichura, wakimbizwe masokoni, Wahukumiwe kwa kwenda kilabuni?

5/Hivi ukaidi ni nini katika tukio hili? Kama suala ni kuombwa kujitolea, na mtu akakataa kujitolea ili aendelee na shughuli zake za kutafuta pesa, kuna kosa gani hapo?
 
weweweeeeeeeeee waweke ndani masaaa 48,wakikataa katafute babu zao uwachape vibokooo,hapa kazi tu,hakuna kuchekakucheka,,hahahahahahahahahaha sirikali ya wanyonge oyeeeeeeee.
 
Wewe ungekuwa mkuu wa wilaya, hapo ungefanya nini?

usitembee juu ya ardhi kwa majivuno

Katiba ipo hivi
8.-(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -

(b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi; (c) Serikali itawajibika kwa wananchi;

wache wale bata wana nchi ilimradi wanalipa kodi ,Mkuu wa wilaya na timu yake watafute fund huko hazina wajenge
 
Sawa mkuu. Watanzania tuna mambo mengi sana. Wakati fulani bila ka ubabe flani mambo hayaendi

usitembee juu ya ardhi kwa majivuno

Mkuu hii nchi ina vituko, unaweza ukaona huyu kaleta taarifa ya usahihi kumbe ni muwamba ngoma.

Usishangae mwingine akaja na kusema taarifa sahihi zaidi, kwamba vijana walikwenda kunywa pombe kwa hela zao na hawakuona umuhimu wa kwenda kwenye huo ujenzi kwani hela za ujenzi zimeshatolewa na kuliwa na viongozi.

Hii ni nchi yetu na udhaifu wetu tunaujua, ila kama ni kweli lilikuwa ni zoezi la kujitolea na watu wakakwepa basi kichura sio mbaya ni sehemu ya msisitizo wa kujali kazi.
 
HII NINA HAKIKA UMEICHUJA NA UMETUMWA KUMUOKOA MKUU WA WILAYA. MBUNGE WA NKASI TUNAJUA TABIA YAKE HASHINWDI KUMSHAURI MKUU WA WILAYA WATU WAPIGWE
Mbunge wa Nkasi ipi? Kumbuka kuna Nkasi Kaskazini ambako Mbunge ni Ally Kessy (nahisi unamaanisha huyu sababu ndio maarufu sana) pia kuna Nkasi Kusini ambako kuna mbunge mwingine na Kijiji cha Ntuchi (kilichotajwa) kinapatikana huko

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mbunge hajielewi yule!

brain is the beautiful part of the body.
Ikiwa wewe ambaye hata jiografia ya nchi yako huijui unasemaje mbunge hamuelewi. Yani ukisikia Nkasi unadhani Mbunge ni Ally Kessy pekee, kumbe Nkasi ni wilaya na ina majimbo Mawili, Nkasi Kusini (huko mleta uzi anakozungumzia) na Nkasi Kaskazini kwa Ally Kesy huyo unayemaanisha wewe.

Ku-conclude jambo usilolijua huoni kama kutojielewa pia

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom