Usahihi: VAT kwenye escrow

Usahihi: VAT kwenye escrow

Mkuu, imekuwa vema umelileta hili katika namna hii. Ni vizuri pia kwa sababu kwa maelezo yako naona unao utaalamu wa kutosha kuweza kujadiliana suala hili katika mrengo wa kikodi (VAT).

Maelezo yako kwa sehemu kubwa yapo sawa kabisa. Lakini hapo mwishoni, kwa uelewa wangu, naona unapotosha.

Kwanza, ni kweli kuwa IPTL ndiye mwenye wajibu wa kukusanya VAT kutoka Tanesco (kwa niaba ya serikali/TRA) na kuiwasilisha kodi hiyo kwa TRA. Swali la msingi ni je pesa zilizowekwa escrow zilikuwa na VAT ndani yake. Kama jibu ni ndiyo, basi VAT hiyo ni mali ya serikali/TRA na siyo mali ya IPTL. Kwa misingi ya VAT, IPTL ni wakala wa serikali katika kukusanya kodi ya VAT. Labda kabla sijaendelea kuonesha ni kwa vipi Muhongo, AG and BOT pengine walivunja sheria, nataka uniambie kwanza mpaka hapa kama tunakubaliana kuwa pesa hizo ni mali ya umma.

Tukubaliane kwamba ni mali ya UMA kivipi wakati nimehitimisha kwa kusema sio mali ya UMA. Hoja ya VAT kwenye swala la ESCROW imelazimishwa bila sababu za msingi, na ndio maana nasema sababu zilizopelekea hilo zikijakujilikana kuna watu wanaweza kupondwa mawe mpaka wafe.

Labda uniambie kwamba, TRA waliielekeza BOT au TANESCO wasiilipe IPTL sababu IPTL wanadaiwa pesa nyingi sana na TRA walizozikusanya toka Tanesco alafu hawajaziwasilisha TRA.

Sheria za kodi, zinaipa mamlaka TRA kunyakua mali na pesa za mdaiwa wa kodi kokote inakoweza kuzifikia, kwa sababu hawakufanya hivyo ni wazi hawakuwa na issue na IPTL,
 
Naomba watanzania tusiwe na jazba.

Tanesco ni mfanyabiashara kama wengine tu

Tanesco ni wafanyabiashara ya kutuuzia umeme. Katika kuuza huo umeme wameweka VAT, ambayo wao wanawajibu wa moja kwa moja kuipeleka TRA. Kama Tanesco hawakupeleka VAT, TRA waibane Tanesco sio IPTL

Ili Tanesco wafanye hiyo biashara ya kutuuzia umeme, lazima wagharamie gharama za uzalishaji ikiwemo kuilipa IPTL (achilia mbali mkinzano wa viwango, ambalo hili ni u-pumbavu wa Tanesco).

Kama ilivyo kwa mlaji yeyote, yeye hulipa gharama ya bidhaa na VAT. Suala la muuzaji kuipeleka hiyo VAT TRA ni la huyo muuzaji sio mnunuzi. IPTL ni muuzaji na Tanesco ni mnunuzi. Hivyo wajibu wa kulipa VAT ya capacity charge TRA ni wa IPTL sio Tanesco.

ESCROW ACCOUNT
Kutokana na mzozo wa rates za capacity charge, ilifunguliwa ili kuhifadhi fedha kwa muda hadi hapo watakapo ridhiana kama Tanesco haibiwi, IPTL wachukue pesa zao, na kama wanaibiwa, basi kiasi walichoibiwa wakipunguze kutoka kwenye hii account na kinachobaki IPTL walipwe.

Suala la kulipa VAT kwa pesa hii lilikuwa na linabaki kuwa la IPTL. Nashangaa kwa nini TRA wameshindwa kuitekeleza sheria ya VAT. Naamini Tanesco walikuwa wanatenga hii pesa baada ya kupokea Tax invoices toka IPTL. IPTL kwa kutoa tax invoice, walitakiwa kulipa VAT (baada ya kujaza VAT return) bila kujali kama wamelipwa na Tanesco au la. Hapa TRA wanatakiwa wajibu, sio kukurupuka na kusema ndani ya fedha za Escrow kuna kodi ya serikali NO.

Kama IPTL hawakulipa VAT hadi leo, TRA wanatakiwa kuwajibika.

KULIPWA PESA HIZO IPTL
Kama Tanesco (mdaiwa wa capacity charge) aliridhika kuwa hakuibiwa ????? basi hakuna tatizo lolote kulipa IPTL pesa yote bila kupunguza kodi yeyote, laba ka TRA waliiagiza Tanesco kuwa wakara wa kuikusanyia kodi zote za IPTL, vinginevyo hakuna kosa.

UTARATIBU WA KUTOA PESA
Kila mkataba una utaratibu wake. Naamini hata wakati wa kufungua hii account, kulikuwa na utaratibu wa namna ya kuja kuifunga. Uangaliwe huo kama ulifuatwa au la. Kama haukufuatwa watu wawajibike kwa hilo na hapa wa kuwajibika ni GAVANA WA BENKI KUU.

MIGAWO
Pamoja na maelezo mazuri mengi ya kujitetea namna pesa ilivokuwa inatoka, hapa kuna tatizo kubwa. Sioni shida mtu kuamua kugawa pesa yake kwa anayemtaka, ila katika hili kuna shida, figure zinarandana???????

1. Inaonesha kuwa muda wa kuamua kulipa IPTL au kurudisha fedha Tanesco ulikuwa bado (na hili ndilo halisia), ila wajanja walitumia mwanya huu kujinufaisha au

2. Mtoaji alikuwa anatakatisha pesa chafu aliyonayo, sio ya IPTL tu bali ni Zaidi hizi. Money Laundering au

3. Wapokeaji ndio vinara wa kusuka mipango ya uchotaji huu, na inaonyesha wako wengi Zaidi ya walitajwa


CAPITAL GAINS

Hili sio suala la pesa hii, TRA, IPTL na wote kwenye mnyororo wa kubadilisha hati fungani (shares) wamechemka na wawajibike.


USHAURI

Tusipoteze uelekeo kwa kung’ang’ania kuwa ni za serikali au la.

a) Tujikite kuhoji , je kutoka kwake kulikuwa sahihi kwa maana ya wakati, maana bado kesi ya capacity haijaisha hivyo haikuwa sahihi kutoa hizo pesa, maana iliwekwa BOT kusubiri suluhu.

b) Gavana wa BOT ajibu kama terms of reference za kufungua hii account na namna zilivyotoka ni sahihi? Vinginevyo awajibike na waliomtuma au kumshinikiza

c) Mwanasheria Mkuu, alikuwa sahihi kusema pesa hii haina kodi ya serikali, lakini, kabla ya kutoa hayo maagizo, akiwa mtetezi wa haki za serikali, alitakiwa kujua je VAT ya hiyo fedha, IPTL walilipa kwa wakati TRA? Kama walilipa, ruksa kutoa (kama muda ulikuwa sahihi) kama walikuwa hawajalipa, hakuatakiwa kuruhusu kutoka wakati akijua fika kuwa IPTL iko ICU. Awajibike kwa kutokuwa makini

d) TRA: TRA wanakimbizana na vidagaa Kariakoo, wanaacha kukusanya mabilioni ya VAT (kama IPTL hawakulipa kila mwezi walipotoa invoice za kuidai Tanesco) toka IPTL. Watendaji (Kamishna wakuu na makamishan wa VAT) waliokuwepo toka Escrow account inafunguliwa hadi leo wajibu na kuchukuliwa hatua

e) Kamati ya Zitto, inatakiwa itende haki sio kutumia jazba na chuki binafsi. Wasituaminishe uongo, hasa kusema kulikuwa na pesa za serikali. Wao wangesema, kwa kuwa Tanesco ni shirika la umma, kama wakishinda kesi, itakuwa kazi sana kupata pesa yao toka IPTL. Waache haya maneno ya “inaweza kuwemo………..”

Nawasilisha

Nimeupenda uchambuzi wako. Nakubaliana no isipokuwa nadhani kuna makosa machache umefanya, labda sikuelewa vizuri nieleweshe zaidi.

Kama Tanesco hawakupeleka VAT, TRA waibane Tanesco sio IPTL

Nadhani hapa umechanganya mambo. Unazungumzia umeme unaouzwa na Tanesco au umeme unaouzwa na IPTL? Swala lililopo ni umeme unaouzwa na IPTL, Tanesco akiwa mnunuzi.

Kama unazungumzia umeme unaouzwa na IPTL basi kwa msimamo huo, kama Tanesco watakuja kwako kununua nguzo za umeme, na wewe ukawacharge VAT kama utashindwa kuwasilisha hivyo VAT basi wadaiwe Tanesco. Nikija mimi kununua mbao kwako ukanicharge VAT lakini ukashindwa kuwasilisha basi ni mimi wa kudaiwa? Wataniona wapi? Kuna wangapi wanaokuja kununua vitu kwako kwa siku moja - itakuwa rahii kuwafuatilia?

Vile vile sikubaliani na wewe kwenye sentensi ifuatayo: Naamini Tanesco walikuwa wanatenga hii pesa baada ya kupokea Tax invoices toka IPTL. Kwa kuwa mnunuaji siyo anayepeleka VAT bali muuzaji(mfanyabiashara, yaani ni IPTL)

Nakubaliana na wewe hapa:
basi hakuna tatizo lolote kulipa IPTL pesa yote bila kupunguza kodi yeyote, laba ka TRA waliiagiza Tanesco kuwa wakara wa kuikusanyia kodi zote za IPTL, vinginevyo hakuna kosa.



 
Hakuna fedha za umma kwenye escrow, IPTL kama ni wakala wa kodi basi kodi itatolewa full stop.
Sijakuelewa mkuu! Tanesco wanasema walikuwa wanalipa pesa escrow pamoja na VAT component yake. Kwa hivyo unasema hiyo VAT sio ya umma? IPTL ana uhalali gani wa kukusanya VAT na kuitumia katika matumizi yake?
 
Aliyekuwa akiweka fedha kwenye account ya ESCROW ni TANNESCO na TANNESCO ni shirika la umma na hadi fedha zinachukuliwa mgogolo uliokuwepo ulikuwa haujatatuliwa hivyo basi fedha hizo zilikuwa bado za TANNESCO hadi pale mgogolo ungeisha ndipo ingeweza kuwa vinginevyo.

Mgogoro ulitatuliwa kwa taratibu walizojiwekewa kwenye kikao kunduchi beach hoteli. wewe unapaswa kuwauliza Tanesco, kama walikuwa hawakubaliani na invoices ni kwa nini walikuwa wanapeleka hela escrow, Upumbavu wao uko hapo tu.

muda wote walikuwa wanalalamika na kuomba pesa serikali za kujiendesha lakini wanakwenda kuweka pesa in deposit bot, hizo ni akili au matope? wao hawakuwa na accounts za kuweka hizo pesa? au walikuwa na excess liquidity?
 
Naomba kuuliza kama pesa za VAT ni mali ni mali ya nani .TRA ni executive agency ya wizara ya fedha .Wizara ni sehemu ya serikali.Serikali ni sehemu ya umma.Kama sio mali ya umma na kama taasis inaweza kwenda kudai tu basi kwa hasara aliyosababisha Mh Mramba miaka ile aachiwe tu halafu TRA ikaidai allex Stewarts hizo hela B 11.7 yaishe na mzee wa watu aendelee na Precision air na ubunge wake
 
Sijakuelewa mkuu! Tanesco wanasema walikuwa wanalipa pesa escrow pamoja na VAT component yake. Kwa hivyo unasema hiyo VAT sio ya umma? IPTL ana uhalali gani wa kukusanya VAT na kuitumia katika matumizi yake?

Ukiambiwa leo kwamba IPTL inaidai TRA pesa za VAT, utajisikiaje?
 
TANESCO KASAJILIWA.
Si tu ni mnunuzi mkubwa bali pia ni muuzaji mkubwa wa Umeme.Alitakiwa a-withold tax na kupeleka TRA

Sheria ya VAT inasemaje? Nijuavyo mimi kua sheria kadhaa za kodi zinazomtaka mlipaji "to withhod tax payable", mojawapo ni ya PAYE. Kama hakuna sheria kama hiyo kwenye swala la VAT lisitupotezee muda wetu. Tujifunze kuona sheria kama zilivyo.
 
Kuna madhara ya watu kuwa wataalamu wa vitu wasivyovijua......

VAT inakatwa katika jumla kuu ya malipo. Tanesco wangewezaje kujua VAT kama bado hawakuwa na hakika ya kiwango cha pesa walichotakiwa kulipa IPTL? Kumbuka kodi ni ''percentage ya total amount'' na wala sio flat rate!!!
Kwa kifupi hata kama TANESCO wangelipa shilingi 10 kwa IPTL ndani yake ipo kodi ya V.A.T

Jambo la pili, kwa kuruhusu pesa kutoka ina maana kuwa TANESCO wanakubaliana na kiwango cha capacity charge walichotozwa na wanachotozwa, kwa hiyo wameamua kesi wenyewe kwa hasara yao.

Bado huoni kuwa hapo kuna hujuma imefanyika?

Ninachoweza kusema ni kuwa huitaji kuwa vyama vya upinzani kuona hili. Hii ganji iliyotoka ni faida ambayo iptl wameipata kwa kutoza capacity charge kubwa.
Hela ya biashara inapogawiwa kama gawio la faida kwa wanahisa wenye akili lazima wahoji?
 
Upo sahihi kabisa, kuwa ndani ya ile pesa iliyokuwa ndani ya Escrow account, kulikuwa na VAT iliyolipwa na TANESCO. VAT ile ni pesa ya serikali, ni pesa umma. Na hiyo ilifafanuliwa vizuri sana kwenye PAC ripoti.

Mkuu, imekuwa vema umelileta hili katika namna hii. Ni vizuri pia kwa sababu kwa maelezo yako naona unao utaalamu wa kutosha kuweza kujadiliana suala hili katika mrengo wa kikodi (VAT).

Maelezo yako kwa sehemu kubwa yapo sawa kabisa. Lakini hapo mwishoni, kwa uelewa wangu, naona unapotosha.

Kwanza, ni kweli kuwa IPTL ndiye mwenye wajibu wa kukusanya VAT kutoka Tanesco (kwa niaba ya serikali/TRA) na kuiwasilisha kodi hiyo kwa TRA. Swali la msingi ni je pesa zilizowekwa escrow zilikuwa na VAT ndani yake. Kama jibu ni ndiyo, basi VAT hiyo ni mali ya serikali/TRA na siyo mali ya IPTL. Kwa misingi ya VAT, IPTL ni wakala wa serikali katika kukusanya kodi ya VAT. Labda kabla sijaendelea kuonesha ni kwa vipi Muhongo, AG and BOT pengine walivunja sheria, nataka uniambie kwanza mpaka hapa kama tunakubaliana kuwa pesa hizo ni mali ya umma.
 
Nimeupenda uchambuzi wako. Nakubaliana no isipokuwa nadhani kuna makosa machache umefanya, labda sikuelewa vizuri nieleweshe zaidi.

Kama Tanesco hawakupeleka VAT, TRA waibane Tanesco sio IPTL

Nadhani hapa umechanganya mambo. Unazungumzia umeme unaouzwa na Tanesco au umeme unaouzwa na IPTL? Swala lililopo ni umeme unaouzwa na IPTL, Tanesco akiwa mnunuzi.

Kama unazungumzia umeme unaouzwa na IPTL basi kwa msimamo huo, kama Tanesco watakuja kwako kununua nguzo za umeme, na wewe ukawacharge VAT kama utashindwa kuwasilisha hivyo VAT basi wadaiwe Tanesco. Nikija mimi kununua mbao kwako ukanicharge VAT lakini ukashindwa kuwasilisha basi ni mimi wa kudaiwa? Wataniona wapi? Kuna wangapi wanaokuja kununua vitu kwako kwa siku moja - itakuwa rahii kuwafuatilia?

Vile vile sikubaliani na wewe kwenye sentensi ifuatayo: Naamini Tanesco walikuwa wanatenga hii pesa baada ya kupokea Tax invoices toka IPTL. Kwa kuwa mnunuaji siyo anayepeleka VAT bali muuzaji(mfanyabiashara, yaani ni IPTL)

Nakubaliana na wewe hapa:
basi hakuna tatizo lolote kulipa IPTL pesa yote bila kupunguza kodi yeyote, laba ka TRA waliiagiza Tanesco kuwa wakara wa kuikusanyia kodi zote za IPTL, vinginevyo hakuna kosa.




Uko huru.

Ngoja niendelee na shughuri zangu.
 
Mkuu SMU. kuna madhara ya watu kuwa wataalamu wa vitu wasivyovijua......

VAT inakatwa katika jumla kuu ya malipo. Tanesco wangewezaje kujua VAT kama bado hawakuwa na hakika ya kiwango cha pesa walichotakiwa kulipa IPTL? Kumbuka kodi ni ''percentage ya total amount'' na wala sio flat rate!!!
Kwa kifupi hata kama TANESCO wangelipa shilingi 10 kwa IPTL ndani yake ipo kodi ya V.A.T

Jambo la pili, kwa kuruhusu pesa kutoka ina maana kuwa TANESCO wanakubaliana na kiwango cha capacity charge walichotozwa na wanachotozwa, kwa hiyo wameamua kesi wenyewe kwa hasara yao.

Bado haoni kuwa hapo kuna hujuma imefanyika?

Ninachoweza kusema ni kuwa huitaji kuwa vyama vya upinzani kuona hili. Hii ganji iliyotoka ni faida ambayo iptl wameipata kwa kutoza capacity charge kubwa.
Hela ya biashara inapogawiwa kama gawio la faida kwa wanahisa wenye akili lazima wahoji?


Mkuu, imekuwa vema umelileta hili katika namna hii. Ni vizuri pia kwa sababu kwa maelezo yako naona unao utaalamu wa kutosha kuweza kujadiliana suala hili katika mrengo wa kikodi (VAT).

Maelezo yako kwa sehemu kubwa yapo sawa kabisa. Lakini hapo mwishoni, kwa uelewa wangu, naona unapotosha.

Kwanza, ni kweli kuwa IPTL ndiye mwenye wajibu wa kukusanya VAT kutoka Tanesco (kwa niaba ya serikali/TRA) na kuiwasilisha kodi hiyo kwa TRA. Swali la msingi ni je pesa zilizowekwa escrow zilikuwa na VAT ndani yake. Kama jibu ni ndiyo, basi VAT hiyo ni mali ya serikali/TRA na siyo mali ya IPTL. Kwa misingi ya VAT, IPTL ni wakala wa serikali katika kukusanya kodi ya VAT. Labda kabla sijaendelea kuonesha ni kwa vipi Muhongo, AG and BOT pengine walivunja sheria, nataka uniambie kwanza mpaka hapa kama tunakubaliana kuwa pesa hizo ni mali ya umma.
 
Tukubaliane kwamba ni mali ya UMA kivipi wakati nimehitimisha kwa kusema sio mali ya UMA. Hoja ya VAT kwenye swala la ESCROW imelazimishwa bila sababu za msingi, na ndio maana nasema sababu zilizopelekea hilo zikijakujilikana kuna watu wanaweza kupondwa mawe mpaka wafe.
Nimekuelewa, ndio sababu sikutaka kuendelea mpaka kwanza tukubaliana kuwa ni za umma ama siyo za umma. Je unakubali kuwa IPTL katika transaction hii alikuwa ni wakala wa kukusanya VAT kutoka Tanessco?

Labda uniambie kwamba, TRA waliielekeza BOT au TANESCO wasiilipe IPTL sababu IPTL wanadaiwa pesa nyingi sana na TRA walizozikusanya toka Tanesco alafu hawajaziwasilisha TRA.
Yes, soma report ya CAG/PAC. Kwa ushauri wa AG, BOT an wengine waliohusika kuzitoa pesa hizo walikataa kutii matakwa ya TRA. Walivunja sheria ya VAT (soma sura 32 yote ya Cap 148).

Sheria za kodi, zinaipa mamlaka TRA kunyakua mali na pesa za mdaiwa wa kodi kokote inakoweza kuzifikia, kwa sababu hawakufanya hivyo ni wazi hawakuwa na issue na IPTL,
Waliomba BOT wazuie kodi hiyo kabla ya kullipwa IPTL lakini AG kinyume na sheria akakaidi/akaisamehe.
 
Tukubaliane kwamba ni mali ya UMA kivipi wakati nimehitimisha kwa kusema sio mali ya UMA. Hoja ya VAT kwenye swala la ESCROW imelazimishwa bila sababu za msingi, na ndio maana nasema sababu zilizopelekea hilo zikijakujilikana kuna watu wanaweza kupondwa mawe mpaka wafe.

Labda uniambie kwamba, TRA waliielekeza BOT au TANESCO wasiilipe IPTL sababu IPTL wanadaiwa pesa nyingi sana na TRA walizozikusanya toka Tanesco alafu hawajaziwasilisha TRA.

Sheria za kodi, zinaipa mamlaka TRA kunyakua mali na pesa za mdaiwa wa kodi kokote inakoweza kuzifikia, kwa sababu hawakufanya hivyo ni wazi hawakuwa na issue na IPTL,

Sikubaliani na wewe labda uniambie kuwa katika kila invoice waliyokuwa wanawapelekea TANESCO kila mwezi hamkuwepo swala la VAT. Kama kulikuwepo na VAT, basi kiasi hicho cha pesa siyo mali ya IPTL bali cha serikali (TRA). Nashangaa kwa nini hadi leo hii TRA hawajadai pesa zao kutoka IPTL na kuchkua hatua inayotakiwa kama wanavyofanya kwa kampuni zozote zile.
 
Ndugu watanzania wote (in the voice of profesa Muhongo)

Tuache Jaziba, tuache kulazimisha mapenzi yetu kutimia,tuwe na subra, tujipe nafasi ya kutafakari na kupima mambo haya, tujiweke katika nafasi ya kuwatendea maadui zetu vile ambavyo sisi tungependa kutendewa.

Na zaidi, tufuate ushauri alioutoa Mheshimwa Lusinde jana jioni bungeni, kwamba, "TUSEME KWELI ILI TUFANYE MAAMUZI YA HAKI"

KUHUSU PESA ZA ESCROW KUWA NI ZA UMA ETI KWA SABABU KULIKUWA NA KODI YA VAT NDANI YAKE
Ndugu watanzania wote.

Huu ni upotoshaji, ni uongo na uzushi ambao tunapaswa kuukataa, jambo lolote linalofanywa kwa uovu mwisho wake huwa sio mwema.

Report iliyowasilishwa na PAC katika bunge letu, japo ilitegemewa kuwa msingi wa kulipatia haki Taifa letu, imekuwa ni chanzo cha aibu kwa Taifa zima, hutuwezi kupigania maslahi ya Taifa letu kwa kusema uongo, kuficha ukweli kwa wingi wa meneno yaliyopindishwa pindishwa na kupambwa kwa lugha za ghirba.

UKWELI NI HUU
Kama ambavyo mahusiano ya IPTL na TANESCO yanajurikana, hawa walikuwa na bado wanaendelea kufanya biashara pamoja, IPTL akiwa muuzaji na TANESCO Mnunuzi.

Bila kuzingatia namna wanavyofikia bei ya bidhaa husika, ni wazi IPTL imekuwa ikiipatia INVOICES Tanesco, Ili Tanesco Iilipe IPTL.

Sheria yetu ya kodi ya VAT ya mwaka 1997, imetoa maelekezo yanayowapa wafanyabishara FURSA ya kukusanya kodi ya VAT kutoka kwa wanunuzi wa bidhaa zao, kwa niaba ya TRA.

Kutokana na vigezo vilivyowekwa katika sheria husika, IPTL nao ni wakara wa TRA katika kukusanya kodi ya VAT kutoka Tanesco.

Kutokana na mahusiano ya kibishara kati ya TANESCO NA IPTL, TANESCO Haina mamlaka mpaka leo ya kuchukua maamuzi ya kutoilipa IPTL VAT eti ipeleke VAT hiyo TRA yenyewe.

Hivyo basi, hata katika PESA zilizokuwa kwenye ACCOUNT YA ESCROW, TANESCO walitekeleza wajibu wao wa kisheria na kibiasha kuziweka hela hizo kwenye account hiyo zote za IPTL pamoja na VAT (Ambazo kimsingi zote ni za IPTL), Na wakati malipo yanafanyika kutoka account hiyo, YALIFANYIKA KWA USAHIHI KABISA Kwa PESA zote KULIPWA kwa IPTL. Kwa sababu ni wajibu wa IPTL kukusanya VAT kutoka Tanesco.

TRA walipaswa kuidai IPTL pesa hiyo ndani ya mwezi mmoja baada ya IPTL kuipatia INVOICES Tanesco, bila kujali kama IPTL wanaubishani na Tanesco juu ya usahihi wa INVOICE AMOUNTS au la?.

Huu ndio utaratibu, sio mpya, na wote tunaufahamu, jana nimetoa mfano ambao haukueleweka, ukienda dukani kununua bidhaa, unaambiwa bei ya bidhaa ambayo ndani yake kuna VAT, ukifanya maamuzi ya kununua unamlipa muuzaji pesa zote, NA KUANZIA HAPO ZINAKUWA ZAKE na wewe bidhaa inakuwa yako rasmi.
Swala la wafanyabishara kutopeleka makusanyo ya VAT TRA ni tatizo lingine.

HIVYO BASI
Kama sababu ya msingi ya kudai kwamba zile pesa ni za UMA ni sababu ya VAT COMPONENT KWA ZILE HELA, HUO NI UONGO NI UPOTOSHAJI.

Nawasilisha.

= ghilba
= yanajulikana
= wakala

Hayo uliyosema ni sawa na si sawa, Jee, unawea kutuonesha invoice zilizotumika tuone kama zina VAT?

Kuna uwezekano TANESCO walisema wako VAT exempted kwenye mradi huu na wakapeleka pesa bila VAT, uwezekano huo upo kwa kuwa huu mradi mkataba wa IPTL ulianza kabla ya sheria ya VAT.

Lazima kuna technicalities na hilo si tatizo kubwa kwani mitambo ipo, TRA ipo, Mikataba ipo, IPTL hawajalipwa pesa zote wanazodai, ni jambo la kukaa chini TRA na wakala wake na kulitatua. Si jambo la kusema pesa zilizowekwa escrow ni za umma. Hapana, hayo yalikuwa malipo rasmi ya huduma waliyopewa TANESCO na hizo pesa ni za IPTL.
 
Sikubaliani na wewe labda uniambie kuwa katika kila invoice waliyokuwa wanawapelekea TANESCO kila mwezi hamkuwepo swala la VAT. Kama kulikuwepo na VAT, basi kiasi hicho cha pesa siyo mali ya IPTL bali cha serikali (TRA). Nashangaa kwa nini hadi leo hii TRA hawajadai pesa zao kutoka IPTL na kuchkua hatua inayotakiwa kama wanavyofanya kwa kampuni zozote zile.

sasa kama unajua Tanesco walipaswa kudai kodi IPTL kwa nini unasema zile pesa ni za UMA? Kumbuka ukisema ni za UMA unamaanisha kwamba hazikupaswa kulipwa kwa IPTL.

Msiongelee mambo ya hela kinadharia nadharia, ndio maana tunakuwa masikini. Hela ni Hela. Hela iliyopaswa kwenda IPTL hata kama kuna VAT ni hela ya IPTL.

Wewe unalazimisha eti ni za uma kwa sababu tu neno VAT linatajwa nazo?
 
Ukiambiwa leo kwamba IPTL inaidai TRA pesa za VAT, utajisikiaje?
Nitataka kujua ni kwa vipi? Najua zipo sababu za kampuni kuwa kwenye VAT refund position. Kama zipo na zinaeleweka sina tatizo. Lakini VAT refund najua inao utaratibu wake na katika huo utaratibu ni lazima madai hayo yathibitishwe na CPA-PP.
 
Upotoshaji wako uko hapa: Muuzaji ndiye anayelipa vat pale tra na wala sio mmununzi. iptl ni wauzaji wa umeme kwa tanesco,na tanesco ni mununuzi tu. Sasa kama vat haikulipwa kwani fedha za vat ni za nani??? ninachofahamu fedha za escro sio zote za umma bali kuna sehemu ya fedha za umma ndani ya fedha za escro, sagarara na wewe nipe zako

Unapoteza muda wako huyo Sangarara ana lake jambo sio wa kutokuelewa.
 
= ghilba
= yanajulikana
= wakala

Hayo uliyosema ni sawa na si sawa, Jee, unawea kutuonesha invoice zilizotumika tuone kama zina VAT?

Kuna uwezekano TANESCO walisema wako VAT exempted kwenye mradi huu na wakapeleka pesa bila VAT, uwezekano huo upo kwa kuwa huu mradi mkataba wa IPTL ulianza kabla ya sheria ya VAT.

Lazima kuna technicalities na hilo si tatizo kubwa kwani mitambo ipo, TRA ipo, Mikataba ipo, IPTL hawajalipwa pesa zote wanazodai, ni jambo la kukaa chini TRA na wakala wake na kulitatua. Si jambo la kusema pesa zilizowekwa escrow ni za umma. Hapana, hayo yalikuwa malipo rasmi ya huduma waliyopewa TANESCO na hizo pesa ni za IPTL.

I agree with you.
siwezi kuonyesha kama invoice zilikuwa na VAT, labda Mkurugenzi wa TRA asaidie sababu ndo aliwaambia PAC kwamba kuna VAT humo, mi najidili taarifa iliyo mezani.

Huo usahihisho wako wa rugha, nitauhakiki kwenye kamusi nikirudi nyumbani reo jioni.

Tatizo langu ni moja tu.
Lugemalila alikuwa amechanganyikiwa hadi kuanza kutapanya mipesa mingi kiasi kile namna hile?
 
Nitataka kujua ni kwa vipi? Najua zipo sababu za kampuni kuwa kwenye VAT refund position. Kama zipo na zinaeleweka sina tatizo. Lakini VAT refund najua inao utaratibu wake na katika huo utaratibu ni lazima madai hayo yathibitishwe na CPA-PP.

with all this understanding, what makes you think those funds were public funds? peer pressure?
 
Back
Top Bottom