Keyboard_Warrior
JF-Expert Member
- Oct 10, 2015
- 6,108
- 10,480
Heshima kwenu wakongwe..!
Nilishawahi kuangalia series fulani ya Wamarekani, kwenye hiyo series kuna askari mmoja ambaye alikuwa ni Pilot wa ndege zisizokuwa na rubani ndani yake (Drones), kuna siku huyo askari alipewa kazi ya kumlipua mtu mmoja aliyedhaniwa kuwa ni gaidi, alifanya kama alivyoagizwa na wakuu wake akarusha bomu kutoka kwenye drone akamlipua mtu yule. Lakini kumbe kulikuwa na makosa, yule mtu aliyelipuliwa hakuwa gaidi, hivyo aliuawa kimakosa.
Leo nilikuwa naangalia series ya Homeland, niko season ya 4 episode ya kwanza, kwenye hii episode CIA wanafanikiwa kumuona gaidi wanayemuwinda muda mrefu, huyo gaidi yupo ndani ya jengo, kuna tukio la kifamilia lilimfikisha pale. CIA wanaamua kulipua jengo ili kumuua yule gaidi, lakini ndani ya jengo kulikuwa na watu wengine wasio na hatia, hivyo watu wasio na hatia wanalipuliwa pamoja na gaidi yule.
Kwenye jengo kulikuwa na watoto wadogo na wakina mama pia.
Nakuja kwenye lengo la uzi huu:
1) Hivi ni kweli USA huwa wanafanya mission za namna hii?
Au ni maigizo tu hamna kitu kama hiki?
2) Kama ni kweli, huwa wanawajibishwa kwa matatizo yanayojitokeza baada ya kukamilika mission za namna hii?, kwenye matatizo namaanisha madhara ya missions za namna hii kwa watu wasio na hatia.
3) Je, kuna sera au taratibu zozote zilizowekwa na UN juu ya matumizi ya drones za kivita kwa nchi zinazomiliki drones hizo?
Nilishawahi kuangalia series fulani ya Wamarekani, kwenye hiyo series kuna askari mmoja ambaye alikuwa ni Pilot wa ndege zisizokuwa na rubani ndani yake (Drones), kuna siku huyo askari alipewa kazi ya kumlipua mtu mmoja aliyedhaniwa kuwa ni gaidi, alifanya kama alivyoagizwa na wakuu wake akarusha bomu kutoka kwenye drone akamlipua mtu yule. Lakini kumbe kulikuwa na makosa, yule mtu aliyelipuliwa hakuwa gaidi, hivyo aliuawa kimakosa.
Leo nilikuwa naangalia series ya Homeland, niko season ya 4 episode ya kwanza, kwenye hii episode CIA wanafanikiwa kumuona gaidi wanayemuwinda muda mrefu, huyo gaidi yupo ndani ya jengo, kuna tukio la kifamilia lilimfikisha pale. CIA wanaamua kulipua jengo ili kumuua yule gaidi, lakini ndani ya jengo kulikuwa na watu wengine wasio na hatia, hivyo watu wasio na hatia wanalipuliwa pamoja na gaidi yule.
Kwenye jengo kulikuwa na watoto wadogo na wakina mama pia.
Nakuja kwenye lengo la uzi huu:
1) Hivi ni kweli USA huwa wanafanya mission za namna hii?
Au ni maigizo tu hamna kitu kama hiki?
2) Kama ni kweli, huwa wanawajibishwa kwa matatizo yanayojitokeza baada ya kukamilika mission za namna hii?, kwenye matatizo namaanisha madhara ya missions za namna hii kwa watu wasio na hatia.
3) Je, kuna sera au taratibu zozote zilizowekwa na UN juu ya matumizi ya drones za kivita kwa nchi zinazomiliki drones hizo?