Richard irakunda
JF-Expert Member
- Oct 23, 2018
- 3,659
- 4,386
Nakubaliana na wewe kwa 14%
Hizo ndizo hoja na zinatakiwa kujibiwa.Lengo la Marekani huko mashariki ya kati ni kiuchumi zaidi na hawa Iran wanaonekana kumkera sana huyu Kiranja wa dunia kwa sababu ya misimamo yao ya kutaka na kutishia kufunga mlango bahari wa Hormuz(Strait of Hormuz)Kitu ambacho hakitaiumiza Marekani peke yake bali dunia nzima maana kwa njia hiyo karibu mafuta yote kama si mengi yanapitia hapo na pili kushambuliwa kwa tanker za mafuta yanayopita hapo na Iran ndiyo kuliko sababisha sekeseke hili linaloendelea.Marekani wanachofanya hapo ni SHOW OF FORCE tu wala hawawezi kuingia vitani kihasara namna hiyo,Nijuavyo mimi vita si lelemama inapaswa kujipanga hasa.chukulia vita vya Iraq vita hiyo iliandaliwa na BUSH Baba na alipoingia BUSH Mtoto alimaliza hiyo kazi kwa ushindi.Ukija hapa kwetu vita vya Kagera maandalizi yake yalianza 1977 waliokuwa jeshini wanajua hili lakini vita vilipiganwa kuanzia oct-1978 na kumalizika 1979 kwa ushindi mnono.Hapo nilikuwa naelezea tu umhimu wa kujipanga kabla ya kuingia vitani na nchi yoyote ile haijalishi ni dhaifu namna gani au ina nguvu kiasi gani.Hivyo kwa maoni yangu hakuna vita hapo maana Marekani hawezi kuingia vitani kichwakichwa hivyo lazima afanye maandalizi.Kuhusu Ground invasion anaweza sana tu kama atapata Proxy huko Iran Ukubwa wa eneo siyo tija pia ukubwa huo inaweza kuwa faida kwa adui!!!!.