PostGE2025 Yaliyomo kwenye muswada wa Marekani kuipa vikwazo Tanzania. Polisi, TISS na Wachina wametajwa

PostGE2025 Yaliyomo kwenye muswada wa Marekani kuipa vikwazo Tanzania. Polisi, TISS na Wachina wametajwa

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

McLaren

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2025
Posts
1,076
Reaction score
3,400

Kuhusu Demokrasia, Uchaguzi na kinachoendelea Tanzania, Muswada huu ambao umetengenezwa na Seneta Ted Cruz na Shaheen unasema yafuatayo:​


(1) Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo uchumi wake unakua kinoma Afrika, kukiwa na ukuaji thabiti wa kiuchumi katika kipindi cha miaka kumi iliyopita kutokana na kuimarika kwa sekta muhimu, ikiwemo kilimo, madini, na utalii.

(2) Uaminifu wa Tanzania kama mshirika wa Marekani unazidi kutiliwa shaka kutokana na ukandamizaji wa kisiasa unaoendelea, kuvunjwa kwa uhuru wa dini na uhuru wa kujieleza, na vizuizi vya kudumu dhidi ya uwekezaji wa Marekani.

(3) Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, uligubikwa na uingiliaji mkubwa wa kisiasa, ikiwemo uchezaji (wizi) na dosari kwenye kuhesabu kura, mambo yaliyombeba Rais aliyekuwepo madarakani Samia Suluhu Hassan na wagombea wengine wa chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM).

(4) Kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, matukio mengi ya utekaji nyara na kupotea kwa watu kisiasa yalifanyika Tanzania; la hivi karibuni likiwa ni kutekwa na kupotea kwa Balozi wa Tanzania Humphrey Polepole mnamo Oktoba 6, 2025.

(5) Hatua mbalimbali za CCM, chama cha kisiasa ambacho kimeshikilia wingi wa viti bungeni na kudhibiti serikali kuu tangu kuundwa kwake mwaka 1977, zimeharibu vibaya demokrasia nchini.

(6) Kesi ya uhaini inayoendelea dhidi ya kiongozi wa upinzani wa Chadema, Tundu Lissu, mashtaka ya ugaidi dhidi ya Naibu wa Chadema John Heche, na kukamatwa kwa wanachama wengine wa upinzani, vyote vina malengo ya kisiasa na vinakusudiwa kuwazuia viongozi wa upinzani wasigombee uchaguzi.

(7) Serikali ya Tanzania imejihusisha na ukiukaji wa uhuru wa kidini, ikiwemo kufuta usajili wa taasisi za dini, unyanyasaji, kukamatwa, na mashambulizi dhidi ya viongozi wa dini, na kuweka vizuizi kwenye ibada na kutoa maoni.

(8) Wakati wa maandamano makubwa ya raia kupinga uchaguzi huo wa uongo na haramu wa Oktoba 29, 2025, Polisi wa Tanzania na Jeshi la Ulinzi (JWTZ) waliua mamia ya Watanzania na kuhatarisha maisha ya raia wa Marekani na watalii waliokuwa nchini.

(9) Wakati waandamanaji wakishambuliwa na Vikosi vya Usalama, Serikali ya Tanzania ilizima intaneti, jambo lililoathiri mawasiliano, biashara, na mambo ya benki, na kuvuruga biashara ya kikanda huku nchi ikipoteza takriban dola $238,000,000.

(10) Kutokana na vurugu hizi ambazo hazijawahi kutokea, Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania ulitoa Tahadhari ya Usalama mnamo Oktoba 30, 2025, ukiwataka raia wa Marekani walioko nchini kujifungia ndani (shelter-in-place).

(11) Baada ya maandamano ya uchaguzi, tume ya uchaguzi ya Tanzania ilitoa matokeo yaliyopingwa, ikimtangaza Rais Samia Suluhu Hassan kama mshindi kwa asilimia 98 ya kura.

Msimamo wa Bunge (Sense of Congress)—

(1) Kwamba ni kwa maslahi ya usalama wa Marekani kusaidia kuzuia kufifia kwa demokrasia kwenye nchi washirika ambapo Marekani imetoa mabilioni ya dola za uwekezaji, maendeleo, na misaada;

(2) Kwamba hatua za Serikali ya Tanzania zimehujumu demokrasia, zimevunja wazi haki za binadamu, zimevuruga biashara, na kuhatarisha usalama wa Watanzania, watalii, na wanadiplomasia;

(3) Kwamba hatua hizi zinaweka maslahi ya Marekani hatarini na kutishia utulivu wa kikanda;

(4) Kuunga mkono uamuzi wa kusitisha mpango wa Millennium Challenge Corporation (MCC) kwa Tanzania; na

(5) Kuonyesha mshikamano na watu wa Tanzania na kuunga mkono wito wa uchunguzi huru wa kimataifa kuhusu ghasia za kabla na baada ya uchaguzi ili waliofanya ukatili wawajibishwe.

FUNGU LA 4. TATHMINI UPYA YA MAREKANI NA TANZANIA

(a) TATHMINI YA UHUSIANO: Waziri wa Mambo ya Nje, akishirikiana na Waziri wa Ulinzi na wakuu wa idara nyingine, watafanya tathmini ya kina kuhusu uhusiano kati ya Marekani na Tanzania.

(b) VIPENGELE: Tathmini hiyo itajumuisha -
  1. Uchambuzi wa mwelekeo wa demokrasia Tanzania;
  2. Mkakati wa mageuzi ya kidemokrasia yanayohitajika;
  3. Tathmini ya misaada ya usalama ili kuhakikisha Jeshi na Polisi wanaheshimu haki za binadamu na kulinda usalama wa raia na wageni;
  4. Tathmini ya jinsi ghasia na kuzimwa kwa intaneti kulivyoathiri biashara na uwekezaji wa Marekani;
  5. Tathmini ya uhusiano kati ya Serikali ya Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China, ikijumuisha

    (A) ushirikiano wa kijeshi na kiusalama, ikiwemo mafunzo, mazoezi, uuzaji na usambazaji wa silaha, na ushirikiano kati ya vyombo vya ulinzi, intelijensia, au vyombo vya doria na usalama;

    (B) ushirikiano wa kiuchumi, ikiwemo uwekezaji, mikopo, na ufadhili unaohusisha mashirika ya umma ya China au kampuni zilizounganishwa nayo, na athari za shughuli hizo kwenye fursa za masoko, uwezo wa kulipa madeni, na ushindani wa kampuni za Marekani; na

    (C) ushirikiano wa kisiasa na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China unaolenga kudhoofisha misingi ya kidemokrasia, kuimarisha mfumo wa chama kimoja, na kujenga chuki dhidi ya Marekani na mataifa ya Magharibi ndani ya nchi na kimataifa
(c) RIPOTI: Ndani ya siku 90 baada ya sheria hii kuanza, Waziri wa Mambo ya Nje atatoa ripoti ya matokeo ya tathmini hii kwa kamati za Bunge.

FUNGU LA 5. RIPOTI KUHUSU BAADHI YA VIONGOZI WA NCHINI TANZANIA

Ndani ya siku 180, Waziri wa Mambo ya Nje atatoa ripoti yenye orodha ya watu wa kigeni ambao:
  1. Wana vyeo vya juu Serikalini, CCM, Polisi, JWTZ, au Usalama wa Taifa (TISS); na
  2. Wanahusika na:
    • (A) Kuagiza au kusimamia utekaji na upoteaji wa watu au kukamata wapinzani na waandishi wa habari kiholela;
    • (B) Kunyanyasa, kutishia, au kutumia nguvu dhidi ya waandishi wa habari na wanaharakati;
    • (C) Udhibiti au kuzima intaneti na vyombo vya habari;
    • (D) Ukiukaji mkubwa wa uhuru wa dini;
    • (E) Kutumia mbinu za ukandamizaji wa kimataifa dhidi ya raia walioko nje ya nchi;
    • (F) Mauaji ya kiholela, utesaji, au uvunjifu wa haki za binadamu;
    • (G) Hatua nyingine zinazovunja Katiba ya Tanzania.

FUNGU LA 6. VIKWAZO

(a) KWA UJUMLA: Ndani ya siku 30 baada ya ripoti kutolewa, Rais anaweza kuweka vikwazo kwa watu waliotajwa.

(b) VIKWAZO HIVYO NI:
  1. KUZUIA MALI: Rais anaweza kuzuia miamala yote ya mali za watu hao zilizoko Marekani au chini ya udhibiti wa Wamarekani.
  2. KUNYIMWA VISA NA KUINGIA: Hawataruhusiwa kuingia Marekani, na visa zao za sasa zitafutwa mara moja.
(c) UTEKELEZAJI: Rais ana mamlaka ya kutumia sheria za kiuchumi (IEEPA) kutekeleza hili, na kutakuwa na adhabu kwa yeyote atakayevunja masharti haya.

(d) MAANA YA MANENO: Hapa inafafanua bidhaa za kilimo, vifaa vya tiba, na dawa.

(e) KUSITISHA VIKWAZO: Rais anaweza kuondoa vikwazo ikiwa atathibitisha kuwa mtu huyo ameacha vitendo hivyo na kuna uhakika hatafanya hivyo tena.

(f) MAMBO AMBAYO HAYAHUSIKI:

  1. Misaada ya kibinadamu (chakula, dawa, vifaa vya tiba).
  2. Makubaliano ya kimataifa (kama yale ya Umoja wa Mataifa) au mambo ya usalama (intelejensia).
  3. Uingizaji wa bidhaa za kawaida (isipokuwa data za kiufundi).

FUNGU LA 7. MARUFUKU YA MISAADA NA UWEKEZAJI WA MAREKANI KWA TANZANIA

(a) MARUFUKU: Hakuna fedha za Marekani zitakazotolewa kwa taasisi yoyote Tanzania kwa ajili ya:
  1. Misaada ya kiusalama;
  2. Mikopo, bima, au uwekezaji kutoka mashirika ya DFC, Export-Import Bank, au USTDA.
(b) SHARTI LA KUONDOA MARUFUKU: Marufuku itaisha siku 30 baada ya Waziri wa Mambo ya Nje kuthibitisha kuwa Serikali ya Tanzania imefanya yafuatayo:
  1. Mageuzi ya uchaguzi ili uwe huru na wa haki;
  2. Kufuta kesi za kisiasa na kuwaachia huru wapinzani;
  3. Kuchukua hatua dhidi ya viongozi na askari waliohusika na utekaji na vurugu;
  4. Kuacha kuwatishia na kuwabana waandishi wa habari na wanaharakati.
(c) VITU AMBAVYO HAVIJAZUILIWA: Misaada ya kibinadamu, misaada ya afya, na misaada ya kukuza demokrasia na haki za binadamu.

FUNGU LA 8. MARUFUKU YA FEDHA ZA MCC KWA TANZANIA

(a) MARUFUKU: Hakuna fedha za MCC zitakazotolewa kwa ajili ya miradi yoyote Tanzania.

(b) SHARTI: Marufuku hii itaisha tu ikiwa uongozi wa MCC utathibitisha kwa Bunge kuwa Serikali ya Tanzania imeonyesha dhamira ya dhati katika utawala wa kidemokrasia na haki.

FUNGU LA 9. KAMATI ZA BUNGE ZINAZOHUSIKA

Katika sheria hii, kamati hizo ni:
  1. Kamati ya Mambo ya Nje na Kamati ya Matumizi ya Fedha ya Seneti;
  2. Kamati ya Mambo ya Nje na Kamati ya Matumizi ya Fedha ya Baraza la Wawakilishi
 

Attachments

Kwenye huu muswada mpya ambao umetoka Marekani inasema Tanzania ilikuwa rafiki yao mkubwa, lakini sasa "imeanza kuleta zengwe."

kuhusika na ukatili.

Someni muswada wote hapa
Wale wote waliohusika na utekaji, kutesa watu, au kuzima internet, Marekani inasema: "No Visa kwenu!" Mali zao zilizoko kule Marekani zitakamatwa na familia zao hazitakanyaga kule.
 
Sijawahi tamani kuishi marekani au ulaya,nchi hazina wali nazi za nini?

Anyways shida ipo kwa urusi na uranium,ushawishi wa china

Uchaguzi wa 2024 marekani Elon musk alijua matokeo saa nne kabla hata ya tume kujua,hii ni kwa kuwa alitumia maelfu ya satellite zake kuiba kura,so wadili na Hilo kwanza
 
Sijawahi tamani kuishi marekani au ulaya,nchi hazina wali nazi za nini?

Anyways shida ipo kwa urusi na uranium,ushawishi wa china

Uchaguzi wa 2024 marekani Elon musk alijua matokeo saa nne kabla hata ya tume kujua,hii ni kwa kuwa alitumia maelfu ya satellite zake kuiba kura,so wadili na Hilo kwanza
Unakuta Mpuuzi kama huyu anaonekana Bora Tanzania!!
 
Watakavyoamua kufanya watafanya
-tanzania ni nchi ya maamzi magumu, nayo ikibidi itajibu kwa mwendo huo huo

Wasitutishe
 
Hayo yote Tzn ilishajiandaa nayo sidhani kama Kuna jipya.

Kina Bashite walishapigwa marufuku lakini maisha yanaendelea so wanajua ila baada ya mda utawala ukija mwingine wa Tzn na USA mambo yatakuwa poa tena.

Mwisho itaishia kwenye siasa hivyo hivyo ila kwenye biashara USA hawezi gusa maana anashindana na Russia/China.
 
Hebu tafakarini hoja zao kwa umakini na kwa maslahi mapana ya kiuchumi kati yetu na wao.
Marekani ni dude kubwa kiuchumi na kushindana naye sisi tutaumia mno. China anaangalia faida tu na hajawahi kujali maisha ya watu popote alipo.
Nashauri, tuwe wapole na kurekebisha kasoro zinazopigiwa kelele haraka sana tuepuke kadhia hii ya kufungiwa kila aina ya msaada kwani hatuwezi kujidanganya hapa kuwa hatuwahitaji.
Mnaobeza hatua za marekani nadhani ni wale waliozaliwa 2020 but siye wa enzi za mwalimu tunakijua nje ndani kibano cha marekani kwani hakuna rangi tuliacha kuiona! Tukatae kurudishwa enzi za sokoine na magwanji!
 
Kwenye huu muswada mpya ambao umetoka Marekani inasema Tanzania ilikuwa rafiki yao mkubwa, lakini sasa "imeanza kuleta zengwe."

Wanasem

Ukipitishwa, utapelekwa kwa Rais wa Marekani ili ausaini uwe sheria kamili. Baada ya hapo, ndani ya miezi 3 hadi 6, Marekani inaweza kutoa majina ya vigogo wa Polisi, JWTZ, TISS na CCM watakaobainika kuhusika na ukatili.

Someni muswada wote hapa
Na iwe hivyo..
Maaana hiyo misaada wanayotupa cccm wanaitumia kama nyenzo zao za kututesa na kutuua..
Bora wasitishe
 
Kwenye huu muswada mpya ambao umetoka Marekani inasema Tanzania ilikuwa rafiki yao mkubwa, lakini sasa "imeanza kuleta zengwe."

WanasemaJWTZ, TISS na CCM watakaobainika kuhusika na ukatili.

Someni muswada wote hapa
mbona wamewasahau WAARABI UAE kuingiza Silaha kupitia GOUTOROV?
 
Porojo tu kila siku. Let it be now or never!!

Trump afanye kilekile alichokifanya Venezuela!!
 
Back
Top Bottom