Urusi yatumia kombora la kisasa la hypersonic, huko Ukraine

profesawaaganojipya

JF-Expert Member
Apr 21, 2015
1,484
3,127
Russia imetumia kombora la kisasa kabisa lisilozuilika la hypersonic, kuharibu ghala la silaha nchini Ukraine.

USA NA NATO hawana mfumo wa kuweza kulizuia au kuliangusha kombora hilo, NATO wote tumbo joto, USA anajipendekeza kwa mchina ili amgeuke Russia, na Mchina kakomaa na swahiba wake Russia.

====

Waziri wa Ulinzi wa Urusi amethibitisha kuwa nchi yake imetumia bomu hatari la hypersonic kwa mara ya kwanza kulishambulia na kuliteketeza ghala la silaha nchini Ukraine.

Bomu aina ya Hypersonic lina uwezo wa kusafiri kwa kasi ya kilomita 4,900 kwa saa na kuongeza kasi hadi kufikia kilomita 12,350 kwa saa, likiwa pia na uwezo wa kubeba kichwa cha mzinga wa nyuklia chenye uzito wa kilo 480 ambayo ni mara 33 ya bomu lililoshushwa na Marekani katika ardhi ya Hiroshima na Nagasaki nchini Japan wakati wa vita kuu ya pili ya dunia.

Putin amelielezea bomu hilo kama silaha muhimu kwenye mapigano na kuinadi kuwa inaweza kusafiri mara kumi zaidi ya spidi ya sauti na kwamba hakuna nchi ya Magharibi hata moja yenye teknolojia ya kuzuia bomu hilo kupitia mfumo wa usalama wa anga.

Bomu hilo lina uwezo wa kusafiri umbali (range) wa kilometa takribani 2011 huku likiwa na uwezo wa kusababisha madhara makubwa mahali litakapotua ambapo kwa miaka mingi, Urusi imekuwa ikipinga matumizi ya silaha za masafa marefu aina ya hypersonic.

Meja Jenerali wa jeshi la Urusi, Igo Konashenkov amesema licha ya bomu hilo, Urusi pia ilitumia makombora kusambaratisha ngome ya majeshi ya Ukraine iliyopo karibu na bandari ya bahari nyeusi ya Odesa.

Naye msemaji wa vikosi vya anga vya majeshi ya Ukraine Yuri Ignat amethibitisha kuwa ni kweli ngome yao imeshambuliwa lakini hakuwa na taarifa ni aina gani ya makombora yalitumika kushambulia eneo hilo.

Global Publishers
 
Russia imetumia kombora la kisasa kabisa lisilozuilika la hypersonic,kuharibu ghala la silaha nchini ukraine.
USA NA NATO hawana mfumo wa kuweza kulizuia au kuliangusha kombora hilo,NATO wote tumbo joto,USA anajipendekeza kwa mchina ili amgeuke russia,na mchina kakomaa na swahiba wake russia.View attachment 2157149View attachment 2157150
Ukiona mrusi amelazimika kutumia mabomu kama haya ni wazi ameshindwa vita, na usikae mbali atajibiwa vigorously,

Haya ni mabomu ya maangamizi ambayo hupigwa kutoka nchi na nchi au kutoka bara moja hadi bara jengine yenye mfano wa nuclear

Ni wazi vita ya kawaida ameshindwa putini aliyekuwa akisifika na kupambwa ni kila uchao, ngoma bado mbichi, stay tuned.
 
Hii vita wanatakiwa waimalize mapema. kama kuna mtu ana makombora ya aina hii, aangalie tu mahali ambapo hakuna raia kuan wanajeshi tu, apige haraka ili wanaosalenda wasalende wanaokutana nalo wakutane nalo ili vita iishe tuanze maisha mapya. Kwani kama una silaha nzuri namna hii unasubiri nini kumaliza biashara mapema?
 
Hii vita wanatakiwa waimalize mapema. kama kuna mtu ana makombora ya aina hii, aangalie tu mahali ambapo hakuna raia kuan wanajeshi tu, apige haraka ili wanaosalenda wasalende wanaokutana nalo wakutane nalo ili vita iishe tuanze maisha mapya.kwani kama una silaha nzuri namna hii unasubiri nini kumaliza biashara mapema?
Kuyapiga haya mabomu, utaua na watu waliokua Askari wake. Na pia ameshajitengenezea uasi mkubwa kwa watu wa Ukraine. Kwa iyo hata akiichukua Ukraine. Kutakuwa na machafuko mengi sana

Sent from my Nokia 1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Kwa Mara ya kwanza Russia wametumia KINZHAL HYPERSONIC missile Nchi Ukraine na Ni kwa Mara ya kwanza siraha ya aina hii kutumika duniani.

Urusi wametumia siraha hii kushambulia mabomu na makombora yaliyokuwa yamefichwa chini ya ardhi huko Magharibi mwa UKRAINE kwenye Kijiji Cha Deliatyn kwenye eneo la Ivano-Frankivsk alithibitisha waziri waulinzi wa Urusi, Huku ikiwa karibu na mpaka wa Romania moja ya washirika wa NATO.

Kwa muda Sasa tangu Vita ianze Urusi imekuwa ikitumia siraha kwa asilimia kubwa zilizoundwa kipindi Cha usovieti (Soviet era).

Ikumbukwe Urusi ndyo nchi pekee iliyofanikiwa kuwa na siraha hizi, China na Marekani zikiwa mbioni kufanikisha uundaji wa siraha hizo(zikiwa Bado kwenye majaribio), zenye ufanisi mkubwa Huku Kasi yake ikiwa Mara 6-10 zaidi ya Kasi ya sauti (sound speed) hivyo kufanya kutodhibitika na aina yoyote ya kiulinzi angani (air defense system) or (anti-aircraft systems) zilizopo duniani kwa Sasa.

View attachment 2157516View attachment 2157517View attachment 2157518View attachment 2157520
View attachment 2157528
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom