Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,271
Bunge la Urusi jana lilipiga kura kuuunga mkono muswada wenye utata ambao wanaharakati wanahofia utaanzisha udhibiti wa mtandao wa mawasiliano wa intaneti kwa kuorodhesha tovuti zinazoonekana kuwa hazifai. Siku moja kabla ya uamuzi huo, tovuti ya Wikipedia ya lugha ya Kirusi iligoma ili kupinga muswada huo, ambao unatangaza operesheni dhidi ya picha za watoto wakiwa uchi. Sheria hiyo mpya itawezesha kuanzishwa kwa daftari yenye rekodi kuhusu tovuti za mambo machafu na kuwataka wamiliki wa tovuti hizo kuzifunga.